< Yeremia 29 >

1 Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
Or ce sont ici les paroles des Lettres que Jérémie le Prophète envoya de Jérusalem au reste des Anciens de ceux qui avaient été transportés, et aux Sacrificateurs, et aux Prophètes, et à tout le peuple que Nébucadnetsar avait transporté de Jérusalem à Babylone;
2 (Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
Après que le Roi Jéchonias fut sorti de Jérusalem, avec la Régente, et les Eunuques, et les principaux de Juda et de Jérusalem, et les charpentiers, et les serruriers.
3 Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
Par Elhasa fils de Saphan, et Guémarja fils de Hilkija, lesquels Sédécias Roi de Juda envoyait à Babylone vers Nébucadnetsar Roi de Babylone; [et ces Lettres] étaient de telle teneur:
4 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
Ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël, à tous ceux qui ont été transportés, [et] que j'ai fait transporter de Jérusalem à Babylone.
5 “Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
Bâtissez des maisons, et [y] demeurez; plantez des jardins, et en mangez les fruits.
6 Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
Prenez des femmes, et engendrez des fils et des filles; prenez aussi des femmes pour vos fils, et donnez vos filles à des hommes, et qu'elles enfantent des fils et des filles, et multipliez là, et ne soyez point diminués.
7 Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
Et cherchez la paix de la ville dans laquelle je vous ai fait transporter, et priez l'Eternel pour elle; parce qu'en sa paix vous aurez la paix.
8 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
Car ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: que vos prophètes qui sont parmi vous, et vos devins, ne vous séduisent point, et ne croyez point à vos songes que vous songez.
9 Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
Parce qu'ils vous prophétisent faussement en mon Nom; je ne les ai point envoyés, dit l'Eternel.
10 Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
Car ainsi a dit l'Eternel: lorsque les soixante-dix ans seront accomplis à Babylone, je vous visiterai, et je mettrai en exécution ma bonne parole sur vous, pour vous faire retourner en ce lieu-ci.
11 Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
Car je sais que les pensées que j'ai sur vous, dit l'Eternel, sont des pensées de paix, et non pas d'adversité, pour vous donner une fin telle que vous attendez.
12 Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Alors vous m'invoquerez pour vous en retourner; et vous me prierez, et je vous exaucerai.
13 Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Vous me chercherez, et vous me trouverez, après que vous m'aurez recherché de tout votre cœur.
14 Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
Car je me ferai trouver à vous, dit l'Eternel, je ramènerai vos captifs, et je vous rassemblerai d'entre toutes les nations, et de tous les lieux où je vous aurai dispersés, dit l'Eternel, et je vous ferai retourner au lieu dont je vous aurai transportés.
15 Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
Parce que vous aurez dit: l'Eternel nous a suscité des Prophètes qui ont [prophétisé que nous viendrions] à Babylone.
16 lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel, touchant le Roi qui est assis sur le trône de David, et touchant tout le peuple qui habite dans cette ville, [c'est-à-dire], touchant vos frères qui ne sont point allés avec vous en captivité;
17 Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
Ainsi a dit l'Eternel des armées: voici, je m'en vais envoyer sur eux l'épée, la famine, et la mortalité, et je les ferai devenir comme des figues qui sont étrangement mauvaises, [et] qu'on ne peut manger, tant elles sont mauvaises.
18 Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
Et je les poursuivrai avec l'épée, par la famine, et par la mortalité; et je les abandonnerai à être agités par tous les Royaumes de la terre, et pour être en exécration, en étonnement, en raillerie, et en opprobre à toutes les nations parmi lesquelles je les aurai dispersés.
19 Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
Parce qu'ils n'ont point écouté mes paroles, dit l'Eternel, qui leur ai envoyé mes serviteurs Prophètes, en me levant dès le matin, et les envoyant; et vous n'avez point écouté, dit l'Eternel.
20 Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
Vous tous donc qui avez été transportés, [et] que j'ai renvoyés de Jérusalem à Babylone, écoutez la parole de l'Eternel.
21 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
Ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël, touchant Achab fils de Kolaja, et touchant Sédécias fils de Mahaséja, qui vous prophétisent faussement en mon Nom: voici, je m'en vais les livrer en la main de Nébucadnetsar Roi de Babylone, et il les frappera devant vos yeux.
22 Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
Et on prendra d'eux un formulaire de malédiction parmi tous ceux qui ont été transportés de Juda, qui [sont] à Babylone, en disant: l'Eternel te mette en tel état qu'il a mis Sédécias et Achab, lesquels le Roi de Babylone a grillés au feu.
23 Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
Parce qu'ils ont commis des impuretés en Israël, et qu'ils ont commis adultère avec les femmes de leurs prochains, et qu'ils ont dit en mon Nom des paroles fausses, que je ne leur avais pas commandées, et je le sais, et j'en suis témoin, dit l'Eternel.
24 Mwambie Shemaya Mnehelami,
Parle aussi à Sémahia Néhélamite, en disant:
25 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
Ainsi a dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël: parce que tu as envoyé en ton Nom des Lettres à tout le peuple qui [est] à Jérusalem, et à Sophonie fils de Mahaséja Sacrificateur, et à tous les Sacrificateurs, en disant:
26 ‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
L'Eternel t'a établi pour Sacrificateur en la place de Jéhojadah le Sacrificateur, afin que vous ayez la charge de la maison de l'Eternel sur tout homme agité par l'esprit, et faisant du Prophète, pour les mettre en prison et aux fers:
27 Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
Et maintenant, pourquoi n'as-tu pas réprimé Jérémie de Hanathot, qui vous prophétise?
28 Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
Car à cause de cela il nous a envoyé dire à Babylone: la [captivité] sera longue: bâtissez des maisons, et [y] demeurez; plantez des jardins, et mangez-en les fruits.
29 Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
(Or Sophonie le Sacrificateur avait lu ces Lettres-là, Jérémie le Prophète l'entendant, )
30 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
C'est pourquoi la parole de l'Eternel fut [adressée] à Jérémie, en disant:
31 “Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
Mande à tous ceux qui ont été transportés, et leur dis: ainsi a dit l'Eternel touchant Sémahia Néhélamite: parce que Sémahia vous a prophétisé, quoique je ne l'aie point envoyé, et vous a fait confier au mensonge;
32 hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”
A cause de cela l'Eternel a dit ainsi: voici, je m'en vais punir Sémahia Néhélamite et sa postérité, [et] il n'y aura personne de sa race qui habite parmi ce peuple, et il ne verra point le bien que je m'en vais faire à mon peuple, dit l'Eternel; parce qu'il a parlé de révolte contre l'Eternel.

< Yeremia 29 >