< Yeremia 29 >
1 Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
Profet Jeremiah ni Jerusalem vah san lah kaawm rae kacuenaw, vaihma hoi profet, Nebukhadnezar ni Jerusalem hoi Babilon lah a ceikhai e naw thung dawk hoi kaawm rae naw koe ca a patawn e teh,
2 (Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
siangpahrang Jekoniah hoi siangpahrangnu, tuenlanaw, Judah tami, Jerusalem kaukkung, kutsakkathoumnaw hoi sumdeinaw ni Jerusalem a tâco takhai awh hnukkhu.
3 Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
Saphan capa Eleasah hoi Hilkiah capa Gemariah tinaw e kut dawk a patawn. Hotnaw teh Judah siangpahrang Hezekiah ni Babilon ram lah Babilon siangpahrang Nebukhadnezar koe a patoun e naw doeh.
4 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
Ransahu BAWIPA, Isarel Cathut ni san lah ceikhai e naw pueng, Jerusalem hoi Babilon lah san lah a ceisak e naw pueng koe hettelah a dei.
5 “Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
Im sak awh nateh haw vah khosak awh. Takha sak awh nateh a pawnaw cat awh.
6 Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
Yu lat awh nateh canunaw capanaw tawn awh. Hottelah canu capa tawn thai nahanlah na capanaw hanlah yu paluen pouh awh, haw vah takangnae awm laipalah pungdaw awh.
7 Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
San lah na osaknae khopui hanelah roumnae tawng awh nateh BAWIPA koe het awh. Bangkongtetpawiteh roumnae koe roumnae na hmu awh han.
8 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
Ransahu BAWIPA, Isarel Cathut ni hettelah a dei, nangmouh thung e profetnaw hoi camkathoumnaw ni na dumyen hanh naseh. mangkamangnaw yuem pouh hanh awh.
9 Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
Bangkongtetpawiteh, kaie min hno lahoi laithoe a dei awh, kai ni ka patounnaw nahoeh, telah BAWIPA ni a dei.
10 Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
Bangkongtetpawiteh, BAWIPA ni hettelah a dei, Babilon teh kum 70 touh akuep toteh ka hloe vaiteh, nangmouh koevah kahawi e ka lawk kakuep sak vaiteh hete hmuen koe boutbout na bankhai awh han.
11 Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
Bangkongtetpawiteh, nangmae kong dawk ka lungpouk teh ka panue. Nangmouh ngaihawinae apout toteh ngaihawinae poe hane hawihoehnae laipalah hawinae koe lah doeh ka pouk, teh lah BAWIPA ni a dei.
12 Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Hattoteh nangmouh ni kai na tawng awh han, na tho awh vaiteh kai koe na ratoum awh vaiteh kai ni na thai pouh han.
13 Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Nangmouh ni kai na tawng awh vaiteh na lungthin buemlah hoi na tawng awh toteh na hmu awh han.
14 Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
Na hmu awh e lah ka o han, telah BAWIPA ni dei. San lah na o awh hmuen koehoi na bankhai awh han, miphun tangkuem dawk na kâkaheisaknae hmuen koehoi na pâkhueng awh han, telah BAWIPA ni a dei. San lah na mansaknae hmuen koe roeroe vah na hrawi han.
15 Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
Bangkongtetpawiteh, BAWIPA ni Babilon ram dawk hai profet na ta pouh telah na ti awh.
16 lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
Hatdawkvah, BAWIPA ni Devit bawitungkhung dawk ka tahung e siangpahrang e kong hoi hete khopui dawk kho ka sak e taminaw kong hoi san lah hrawi hoeh e na hmaunawnghanaw e kong dawk hettelah a dei.
17 Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
Ransabawi, BAWIPA ni hettelah a dei. Khenhaw! ahnimae lathueng vah tahloi, takang hoi lacik ka pha sak vaiteh, thaibunglung paw ca han kahawihoehe patetlah ka coungsak han.
18 Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
Hahoi tahloi, takang lacik hoi ka pâlei awh han. Ahnimouh ru sak hanelah tailai uknaeram pueng koe ka poe han, ahnimouh koe ka patawnnae miphunnaw e rahak vah thoebo e tami, kângairu e, pacekpahlek e, hoi dudam e taminaw lah ka o sak han.
19 Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
Bangkongtetpawiteh, ahnimouh koe ka patoun e ka san profetnaw hno lahoi ka lawk banglahai ngâi awh hoeh, telah BAWIPA ni ati. Amom ka thaw teh ka pâtam ei na thai ngai kalawn awh hoeh, telah BAWIPA ni ati.
20 Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
Hatdawkvah, nangmouh Jerusalem hoi Babilon lah ka patoun teh san lah kaawmnaw pueng, BAWIPA e lawk thai awh haw.
21 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
Ransahu BAWIPA, Isarel Cathut ni Kolaiah capa Ahab hoi Maaseiah capa Zedekiah e min lahoi nangmouh koe laithoe ka dei e kong dawk hettelah a dei. Khenhaw! Babilon siangpahrang Nebukhadnezar e kut dawk ka poe vaiteh nangmae mithmu roeroe vah a man awh han.
22 Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
Ahnimae kong dawk, Babilon ram e Judah tami san lah kaawmnaw pueng ni, Babilon siangpahrang ni hmai dawk pâeng e Zedekiah hoi Ahab patetlah BAWIPA ni nangmae lathueng vah sak naseh, tie thoebonae lawk dawk, a pâkuem awh han.
23 Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
Bangkongtetpawiteh, Isarel ram dawk hnokathout a sak awh teh, a imri e yu koe a uicuk awh teh kaie min hno laihoi kâ ka poe hoeh e laithoe lawknaw a dei awh. Kai kama doeh kapanuekkung hoi kapanuekkhaikung lah ka o, telah BAWIPA ni ati.
24 Mwambie Shemaya Mnehelami,
Nehelam tami Shemaiah kong dawk hai nang ni hettelah na dei han.
25 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
Isarel Cathut, ransahu BAWIPA ni hettelah a dei, Jerusalem e taminaw pueng koe hai thoseh, nang namae min roeroe lahoi ca na patawn, tet pouh.
26 ‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
Tamipathunaw hoi profet lah kakâsaknaw pueng thongim thung na paung teh hlawngbuet sak hanelah BAWIPA ni vaihma Jehoiada e yueng lah vaihma lah na o sak teh, BAWIPA e im khenyawnkung lah na o.
27 Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
Hatdawkvah, bangkongmaw Anathoth tami Jeremiah nang koevah profet ka kâtet e na yue hoeh.
28 Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
Bangkongtetpawiteh, Babilon vah kai koevah ca na patawn teh santoungnae teh asaw han rah, im sak awh, haw vah khosak awh, takhanaw sak awh nateh, a pawnaw cat awh telah ati.
29 Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
Hahoi vaihma Zephaniah ni hote ca teh profet Jeremiah thainae koe a touk.
30 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Hahoi, Jeremiah koe BAWIPA e lawk a pha.
31 “Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
Sankatoungnaw pueng koe Nehelam tami Shemaiah kong dawk BAWIPA ni hettelah a dei, kai ni ka patoun hoeh e Shemaiah ni nang koe lawk a dei telah laithoe lawknaw na yuem sak awh.
32 hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”
Hatdawkvah, BAWIPA ni hettelah a dei. Khenhaw! Nehelam tami Shemaiah hoi a imthungnaw ka rek han. Hete hmuen koe khokasaknaw rahak vah tami buet touh hai tawn mahoeh. Ka taminaw hanlah ka sak hane hnokahawi hah hmawt van mahoeh. Bangkongtetpawiteh BAWIPA taranlahoi taranthawnae a cangkhai.