< Yeremia 28 >

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
И бысть в четвертое лето, царствующу Седекии царю Иудину, в пятый месяц, рече ми Ананиа сын Азоров лживый пророк Гаваонитский в дому Господни, пред очима жерцев и всех людий, глаголя:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
тако рече Господь Вседержитель Бог Израилев: сокруших ярем царя Вавилонска:
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
еще два лета дний, возвращу Аз на место сие вся сосуды дому Господня, яже взя Навуходоносор царь Вавилонский от места сего и пренесе я до Вавилона,
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
и Иехонию сына Иоакимова царя Иудина, и все преселение Иудино вшедшее в Вавилон возвращу в место сие, глаголет Господь, яко сокрушу ярем царя Вавилонска.
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
И рече Иеремиа пророк ко Анании лжепророку пред очима жерцев и пред очима всех людий стоящих в дому Господни,
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
и рече Иеремиа: поистинне тако да сотворит Господь, да утвердит Господь слово твое, еже ты прорицаеши, еже возвратити сосуды дому Господня и вся преселенныя из Вавилона на место сие:
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
обаче слышите слово сие, еже аз глаголю во ушы ваши и во ушы всех людий:
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
пророцы, бывшии прежде мене и прежде вас от века, прорекоша на многи земли и на царства велика о рати и о погублении и о гладе:
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
пророк прорекий мир, пришедшу слову познают пророка, егоже посла им Господь в вере.
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
И взя Ананиа пред очима всех людий клады от выи Иеремиины и сокруши я.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
И рече Ананиа пред очима всех людий глаголя: сице рече Господь: тако сокрушу ярем Навуходоносора царя Вавилонска еще два лета дний со выи всех языков. И отиде Иеремиа на путь свой.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
И бысть слово Господне ко Иеремии, по сокрушении Ананиине клад со выи его, глаголя:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
иди и рцы ко Анании глаголя: тако рече Господь: клады древяныя сокрушил еси и сотвориши вместо тех клады железны,
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
яко тако рече Господь: ярем железен возложих на выи всех языков, служити Навуходоносору царю Вавилонску, и послужат ему: ктому и звери земныя дах ему.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
И рече Иеремиа пророк ко Анании: слыши, Анание: не посла тебе Господь, ты же сотворил еси людий сих уповати на неправду.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
Того ради сице рече Господь: се, Аз отпущу тя от лица земли, в сем лете умреши, яко на Господа (Бога) глаголал еси.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
И умре Ананиа лжепророк в сем лете месяца седмаго.

< Yeremia 28 >