< Yeremia 28 >

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
Et il arriva en cette année-là, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, en la quatrième année, au cinquième mois, qu’Hananias, fils d’Azur, prophète de Gabaon, me parla dans la maison du Seigneur, devant les prêtres et tout le peuple, disant:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël; J’ai brisé le joug du roi de Babylone.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Encore deux ans de jours, et moi je ferai rapporter ici tous les vases de la maison du Seigneur, que Nabuchodonosor, roi de Babylone, a enlevés de ce lieu-ci, et qu’il a transportés à Babylone,
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
Et je ferai revenir, dit le Seigneur, Jéchonias, fils de Joakim, roi de Juda, et tous les fils de la transmigration de Juda qui sont entrés à Babylone, car je briserai le joug du roi de Babylone.
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Et Jérémie le prophète dit à Hananias le prophète, sous les yeux des prêtres et sous les yeux de tout le peuple qui se tenait dans la maison du Seigneur;
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
Jérémie, le prophète, dit donc: Amen, qu’ainsi fasse le Seigneur; que le Seigneur réalise tes paroles que tu as prophétisées, afin que les vases soient rapportés dans la maison du Seigneur, et que tous les fils de la transmigration de Babylone reviennent en ce lieu.
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
Mais cependant écoute cette parole que moi, je dis à tes oreilles et aux oreilles de tout le peuple:
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
Les prophètes qui ont été avant moi et avant toi dès le commencement, ont prophétisé dans beaucoup de pays et dans de grands royaumes, la guerre, et l’affliction, et la famine.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
Le prophète qui prédit la paix, lorsque sa parole s’accomplira, sera reconnu pour le prophète que le Seigneur a envoyé véritablement.
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Et Hananias le prophète enleva la chaîne du cou de Jérémie, le prophète, et la brisa.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
Et Hananias parla en présence de tout le peuple, disant: Voici ce que di t le Seigneur: Ainsi je briserai après deux années de jours le joug de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et je l’ôterai du cou de toutes les nations.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
Et Jérémie, le prophète, reprit son chemin. Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie, après qu’Hananias, le prophète, eut brisé la chaîne, l’ayant ôtée du cou de Jérémie, le prophète, disant:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
Va, et tu diras à Hananias: Voici ce que dit le Seigneur: Tu as brisé des chaînes de bois, et tu feras en leur place des chaînes de fer.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
Car voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: J’ai posé un joug de fer sur le cou de toutes les nations, afin qu’elles se soumettent à Nabuchodonosor, roi de Babylone, et elles se soumettront à lui; de plus je lui ai même donné les bêtes de la terre.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Et Jérémie le prophète dit à Hananias le prophète: Ecoute, Hananias; le Seigneur ne t’a pas envoyé, et tu as fait que ce peuple s’est confié dans un mensonge.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
C’est pourquoi, voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je te chasserai de la face de la terre; cette année tu mourras; car tu as parlé contre le Seigneur.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
Et Hananias mourut cette année-là, au septième mois.

< Yeremia 28 >