< Yeremia 28 >
1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
Et cette même année, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, la quatrième année, le cinquième mois, Ananias, fils de Hazzur, prophète, de Gabaon, me dit dans la maison de l'Éternel, en présence des sacrificateurs et de tout le peuple, ces paroles:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
Ainsi parle l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Je brise le joug du roi de Babel.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Encore deux années, et je ramène en ce lieu tous les meubles de la maison de l'Éternel, que Nébucadnézar, roi de Babel, a enlevés de ce lieu, et qu'il a transportés à Babel.
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
Et Jéchonias, fils de Jéhojakim, roi de Juda, et tous les captifs de Juda, qui sont allés à Babel, je les ramènerai en ce lieu, dit l'Éternel, car je briserai le joug du roi de Babel.
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Alors Jérémie, le prophète, parla à Ananias, le prophète, en présence des sacrificateurs et en présence de tout le peuple qui se tenait dans la maison de l'Éternel;
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
et Jérémie, le prophète, dit: Ainsi soit-il! ainsi fasse l'Éternel! que l'Éternel donne effet aux paroles que tu as prophétisées, en ramenant les meubles de la maison de l'Éternel et tous les captifs de Babel en ce lieu!
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
Seulement écoute cette parole que je prononce à tes oreilles, et aux oreilles de tout le peuple!
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
Les prophètes qui parurent avant moi et avant toi dès les anciens temps, ont dans leurs prophéties menacé beaucoup de pays, et de grands royaumes, de la guerre, et du désastre et de la peste.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
Le prophète qui prophétise le salut, est, quand la parole de ce prophète se réalise, reconnu comme le prophète que l'Éternel envoie véritablement.
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Alors Ananias, le prophète, ôta le joug du col de Jérémie, le prophète, et le brisa.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
Et Ananias parla en présence de tout le peuple en disant: Ainsi parle l'Éternel: De même je briserai le joug de Nébucadnézar, roi de Babel, dans deux ans, l'ôtant du col de tous les peuples. Et le prophète Jérémie alla son chemin.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
Et la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie, après que Ananias, le prophète, eut brisé le joug qu'il avait ôté du col de Jérémie, le prophète, en ces mots:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
Va, et parle à Ananias, et lui dis: Ainsi parle l'Éternel: Tu as brisé un joug de bois, et tu l'as remplacé par un joug de fer.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
Car ainsi parle l'Éternel des armées, Dieu d'Israël: Je mets un joug de fer sur le col de tous ces peuples, pour qu'ils soient asservis à Nébucadnézar, roi de Babel; et ils lui seront asservis; et les bêtes des champs, je les lui donne aussi.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Et Jérémie, le prophète, dit à Ananias, le prophète: Écoute, Ananias! l'Éternel ne t'a point envoyé, et tu as fait que ce peuple se fie au mensonge;
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
c'est pourquoi ainsi parle l'Éternel: Voici, je t'ôterai de la terre; cette année tu mourras; car tu as prêché la révolte contre l'Éternel.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
Et Ananias, le prophète, mourut cette année-là, dans le septième mois.