< Yeremia 28 >
1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
And it cometh to pass, in that year, in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, in the fourth year, in the fifth month, spoken unto me hath Hananiah son of Azur the prophet, who [is] of Gibeon, in the house of Jehovah, before the eyes of the priests, and all the people, saying,
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
'Thus spake Jehovah of Hosts, God of Israel, saying, I have broken the yoke of the king of Babylon;
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Within two years of days I am bringing back unto this place all the vessels of the house of Jehovah that Nebuchadnezzar king of Babylon hath taken from this place, and doth carry to Babylon,
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
And Jeconiah son of Jehoiakim, king of Judah, and all the removed of Judah, who are entering Babylon, I am bringing back unto this place — an affirmation of Jehovah; for I do break the yoke of the king of Babylon.'
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
And Jeremiah the prophet saith unto Hananiah the prophet, before the eyes of the priests, and before the eyes of all the people who are standing in the house of Jehovah,
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
Yea, Jeremiah the prophet saith, 'Amen! so may Jehovah do; Jehovah establish thy words that thou hast prophesied, to bring back the vessels of the house of Jehovah and all the removal from Babylon, unto this place.
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
'Only, hear, I pray thee, this word that I am speaking in thine ears, and in the ears of all the people.
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
The prophets who have been before me, and before thee, from of old, even they prophesy concerning many lands, and concerning great kingdoms, of battle, and of evil, and of pestilence.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
The prophet who doth prophesy of peace — by the coming in of the word of the prophet, known is the prophet that Jehovah hath truly sent him.'
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
And Hananiah the prophet taketh the yoke from off the neck of Jeremiah the prophet, and breaketh it,
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
And Hananiah speaketh before the eyes of all the people, saying, 'Thus said Jehovah, Thus I break the yoke of Nebuchadnezzar king of Babylon, within two years of days, from off the neck of all the nations;' and Jeremiah the prophet goeth on his way.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
And there is a word of Jehovah unto Jeremiah after the breaking, by Hananiah the prophet, of the yoke from off the neck of Jeremiah the prophet, saying,
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
'Go, and thou hast spoken unto Hananiah, saying, Thus said Jehovah, Yokes of wood thou hast broken, and I have made instead of them yokes of iron;
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
For thus said Jehovah of Hosts, God of Israel, A yoke of iron I have put on the neck of all these nations to serve Nebuchadnezzar king of Babylon, and they have served him, and also the beast of the field I have given to him.'
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
And Jeremiah the prophet saith unto Hananiah the prophet, 'Hear, I pray thee, O Hananiah; Jehovah hath not sent thee, and thou hast caused this people to trust on falsehood.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
Therefore thus said Jehovah, Lo, I am casting thee from off the face of the ground; this year thou diest, for apostasy thou hast spoken concerning Jehovah.'
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
And Hananiah the prophet dieth in that year, in the seventh month.