< Yeremia 28 >
1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
This is what happened in the beginning of the reign of King Zedekiah of Judah, in the fifth month of that same year, the fourth year. The prophet Hananiah, son of Azzur, who was from Gibeon, told me in the Lord's Temple in front of the priests and all the people:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
“This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: I have broken the yoke of the king of Babylon.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Before two years have passed I'm going to bring back to Jerusalem all the Temple objects that Nebuchadnezzar king of Babylon removed and took to Babylon.
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
I will also bring back to Jerusalem Jehoiachin, son of Jehoiakim, king of Judah, together with all the exiles from Judah who were taken to Babylon, declares the Lord, because I'm going to break the yoke of the king of Babylon.”
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Then the prophet Jeremiah responded to the prophet Hananiah in front of the priests and all the people who were standing in the Lord's Temple.
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
“Amen!” said Jeremiah. “I wish the Lord would do just that! I wish the Lord would fulfill your prophetic words and bring back Temple objects and all the exiles back to Jerusalem from Babylon.
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
But even so, pay attention to this message I'm going to tell you and everyone here.
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
The prophets of long ago who came before you and me prophesied war, disaster, and disease against many countries and great kingdoms.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
When it comes to a prophet who prophesies peace, see if their prophecies come true. Only that will prove they are really sent by the Lord.”
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Then the prophet Hananiah removed the yoke from the prophet Jeremiah's neck and broke it.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
Hananiah announced in front of everyone, “This is what the Lord says: Just like this, before two years have passed I will break the yoke of Nebuchadnezzar king of Babylon from the neck of all the nations.” Jeremiah the prophet left.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
However, right after Hananiah the prophet had broken the yoke from his neck, a message of the Lord came to Jeremiah:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
“Go and tell Hananiah that this is what the Lord says: You may have broken a wooden yoke of wood, but you have replaced it with an iron yoke.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: I have tied iron yokes on the necks of all these nations to force them to serve Nebuchadnezzar king of Babylon, and they will serve him. I have even given him control over the wild animals.”
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Then the prophet Jeremiah said to the prophet Hananiah, “Listen to this, Hananiah! The Lord didn't send you, but you have convinced these people to believe in a lie.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
So this is what the Lord says: I'm going to get rid of you from the earth. You will die this year because you have promoted rebellion against the Lord.”
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
The prophet Hananiah died in the seventh month of that very year.