< Yeremia 28 >

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
And it came about in that year, when Zedekiah first became king of Judah, in the fourth year, in the fifth month, that Hananiah, the son of Azzur the prophet, who came from Gibeon, said to Jeremiah in the house of the Lord, before the priests and all the people,
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
These are the words of the Lord of armies, the God of Israel: By me the yoke of the king of Babylon has been broken.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
In the space of two years I will send back into this place all the vessels of the Lord's house which Nebuchadnezzar, king of Babylon, took away from this place to Babylon:
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
And I will let Jeconiah, the son of Jehoiakim, king of Judah, come back to this place, with all the prisoners of Judah who went to Babylon, says the Lord: for I will have the yoke of the king of Babylon broken.
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Then the prophet Jeremiah said to the prophet Hananiah, before the priests and all the people who had come into the house of the Lord,
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
The prophet Jeremiah said, So be it: may the Lord do so: may the Lord give effect to the words which you have said, and let the vessels of the Lord's house, and all the people who have been taken away, come back from Babylon to this place.
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
But still, give ear to this word which I am saying to you and to all the people:
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
The prophets, who were before me and before you, from early times gave word to a number of countries and great kingdoms about war and destruction and disease.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
The prophet whose words are of peace, when his words come true, will be seen to be a prophet whom the Lord has sent.
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Then Hananiah the prophet took the yoke from the neck of the prophet Jeremiah and it was broken by his hands.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
And before all the people Hananiah said, The Lord has said, Even so will I let the yoke of the king of Babylon be broken off the necks of all the nations in the space of two years. Then the prophet Jeremiah went away.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
Then after the yoke had been broken off the neck of the prophet Jeremiah by Hananiah the prophet, the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
Go and say to Hananiah, This is what the Lord has said: Yokes of wood have been broken by you, but in their place I will make yokes of iron.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
For the Lord of armies, the God of Israel, has said: I have put a yoke of iron on the necks of all these nations, making them servants to Nebuchadnezzar, king of Babylon; and they are to be his servants: and in addition I have given him the beasts of the field.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Then the prophet Jeremiah said to Hananiah the prophet, Give ear, now, Hananiah; the Lord has not sent you; but you are making this people put their faith in what is false.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
For this reason the Lord has said, See, I will send you away from off the face of the earth: this year death will overtake you, because you have said words against the Lord.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
So death came to Hananiah the prophet the same year, in the seventh month.

< Yeremia 28 >