< Yeremia 28 >

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
Kong Zedekias af Judas fjerde regeringsår i den femte måned sagde Profeten Hananja, Azzurs Søn, fra Gibeon til mig i HERRENs Hus i Præsternes og alt Folkets Nærværelse:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
"Så siger Hærskarers HERRE, Israels Gud: Jeg har sønderbrudt Babels Konges Åg.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Om to År fører jeg tilbage hertil alle HERRENs Huss Kar, som Kong Nebukadnezar af Babel tog herfra og førte til Babel;
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
og Jojakims Søn, Kong Jekonja af Juda, og alle de landflygtige fra Juda, som kom til Babel, fører jeg tilbage hertil, lyder det fra HERREN; thi jeg sønderbryder Babels Konges Åg."
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Profeten Jeremias svarede Profeten Hananja i Nærværelse af Præsterne og alt Folket, som stod i HERRENs Hus,
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
således: "Amen! Måtte HERREN gøre således og stadfæste, hvad du har profeteret, og føre HERRENs Huss Kar og alle de landflygtige fra Babel tilbage hertil!
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
Men hør dog dette Ord, som jeg vil tale til dig og alt Folket:
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
De Profeter, som levede før mig og dig fra Fortids Dage, profeterede mod mange Lande og mægtige Riger om krig, Hunger og Pest;
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
men når en Profet profeterer om Fred, kendes den Profet, HERREN virkelig har sendt, på at hans Ord går i Opfyldelse."
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Så rev Profeten Hananja Ågstængerne af Profeten Jeremiass Hals og sønderbrød dem;
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
og Hananja sagde i alt Folkets Nærværelse: "Så siger HERREN: Således sønderbryder jeg om to År Kong Nebukadnezar af Babels Åg og tager det fra alle Folkenes Hals." Men Profeten Jeremias gik sin Vej.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
Men efter at Profeten Hananja havde sønderbrudt Ågstængerne og revet dem af Profeten Jeremiass Hals, kom HERRENs Ord til Jeremias således:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
"Gå hen og sig til Hananja: Så siger HERREN: Du har sønderbrudt Ågstænger af Træ, men jeg vil lave Ågstænger af Jern i Stedet.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
Thi så siger Hærskarers HERRE, Israels Gud: Et Jernåg lægger jeg på alle disse Folks Hals, at de må trælle for Kong Nebukadnezar af Babel; de skal trælle for ham, selv Markens Vildt har jeg givet ham."
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Så sagde Profeten Jeremias til Profeten Hananja: "Hør, Hananja! HERREN har ikke sendt dig, og du har fået dette Folk til at slå Lid til Løgn.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
Derfor, så siger HERREN: Se, jeg slænger dig bort fra Jordens Flade; du skal dø i År, thi du har prædiket Frafald fra HERREN."
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
Og Profeten Hananja døde samme År i den syvende Måned.

< Yeremia 28 >