< Yeremia 27 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Na začetku kraljevanja Jojakíma, Jošíjevega sina, Judovega kralja, je prišla Jeremiju ta beseda od Gospoda, rekoč:
2 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi.
»Tako mi govori Gospod: ›Naredi si vezi in jarme in si jih položi na svoj vrat
3 Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda.
in jih pošlji edómskemu kralju, moábskemu kralju, amónskemu kralju, tirskemu kralju in k sidónskemu kralju, po roki poslancev, ki so prišli v Jeruzalem k Judovemu kralju Sedekíju
4 Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu:
in jim zapovej, da rečejo svojim gospodarjem: ›Tako govori Gospod nad bojevniki, Izraelov Bog: ›Tako boste rekli svojim gospodarjem:
5 Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo.
›Jaz sem naredil zemljo, človeka in živali, ki so na zemlji, s svojo veliko močjo in s svojim razširjenim laktom in izročil sem jo, komur se je meni zdelo primerno.
6 Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie.
Sedaj sem vse te dežele dal v roko svojega služabnika, babilonskega kralja Nebukadnezarja in tudi živali polja sem mu izročil, da mu služijo.
7 Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.
Vsi narodi bodo služili njemu, njegovemu sinu in sinu njegovega sina, dokler ne pride pravi čas njegove dežele, potem pa ga bodo zasužnjili mnogi narodi in veliki kralji.
8 “‘“Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake.
In zgodilo se bo, da narodi in kraljestva, ki ne bodo služili istemu babilonskemu kralju Nebukadnezarju in ki svojega vratu ne bodo položili pod jarem babilonskega kralja, da bom ta narod kaznoval, ‹ govori Gospod, ›z mečem in z lakoto in s kužno boleznijo, dokler jih ne použijem s svojo roko.
9 Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli.
Zato ne prisluhnite niti svojim prerokom, niti vedeževalcem, niti sanjačem, niti uročevalcem, niti svojim čarodejem, ki vam govorijo, rekoč: ›Ne boste služili babilonskemu kralju, ‹
10 Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia.
kajti prerokujejo vam laž, da bi vas odstranili daleč od vaše dežele; in da bi vas jaz izgnal in bi se vi pogubili.
11 Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.”’”
Toda narodi, ki svoj vrat privedejo pod jarem babilonskega kralja in mu služijo, tiste bom pustil ostati mirne v njihovi lastni deželi, ‹ govori Gospod; ›in obdelovali jo bodo in prebivali v njej.
12 Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi.
Tudi Judovemu kralju Sedekíju sem spregovoril glede na vse te besede, rekoč: ›Privedi vaše vratove pod jarem babilonskega kralja in služite njemu in njegovemu ljudstvu in živite.
13 Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli?
Zakaj bi umirali ti in tvoje ljudstvo, pod mečem, z lakoto in kužno boleznijo, kakor je Gospod govoril zoper narod, ki ne bo služil babilonskemu kralju?
14 Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo.
Zato ne prisluhnite besedam prerokov, ki vam govorijo, rekoč: ›Ne boste služili babilonskemu kralju, ‹ kajti laž vam prerokujejo.
15 ‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’”
Kajti jaz jih nisem poslal, ‹ govori Gospod, ›vendar v mojem imenu prerokujejo laž; da bi vas jaz lahko izgnal ven in bi se pogubili, vi in preroki, ki vam prerokujejo.‹«
16 Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo.
Govoril sem tudi duhovnikom in vsemu temu ljudstvu, rekoč: »Tako govori Gospod: ›Ne prisluhnite besedam svojih prerokov, ki vam prerokujejo, rekoč: ›Glejte, posode Gospodove hiše bodo sedaj v kratkem ponovno privedene nazaj iz Babilona, ‹ kajti prerokujejo vam laž.
17 Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu?
Ne prisluhnite jim. Služite babilonskemu kralju in živite. Zakaj bi bilo to mesto opustošeno?
18 Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli.
Toda če bi bili preroki in bi bila Gospodova beseda z njimi, naj sedaj naredijo posredovanje h Gospodu nad bojevniki, da posode, ki so ostale v Gospodovi hiši in v hiši Judovega kralja in v Jeruzalemu, ne gredo v Babilon.
19 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu,
Kajti tako govori Gospod nad bojevniki glede stebrov, glede morja, glede podnožij in glede preostanka posod, ki preostajajo v tem mestu,
20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu.
ki jih babilonski kralj Nebukadnezar ni vzel, ko je odvedel proč v ujetništvo Jehoníja, Jojakímovega sina, Judovega kralja, iz Jeruzalema v Babilon in vse plemiče iz Juda in Jeruzalema.
21 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu:
Da, tako govori Gospod nad bojevniki, Izraelov Bog, glede posod, ki so ostale v Gospodovi hiši in v hiši Judovega in jeruzalemskega kralja:
22 ‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’”
odnesene bodo v Babilon in tam bodo do dneva, ko jih obiščem, ‹ govori Gospod, ›potem jih bom privedel gor in jih ponovno vrnil na ta kraj.‹«

< Yeremia 27 >