< Yeremia 27 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Au commencement du règne de Joakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole fut adressée à Jérémie par le Seigneur, disant:
2 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi.
Voici ce que me dit le Seigneur: Fais-toi des liens, et des chaînes, et tu les mettras à ton cou.
3 Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda.
Et tu les enverras au roi d’Edom, et au roi de Moab, et au roi des enfants d’Ammon, et au roi de Tyr, et au roi de Sidon, par la main des ambassadeurs qui sont venus à Jérusalem vers Sédécias, roi de Juda.
4 Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu:
Et tu leur ordonneras de parler ainsi à leurs maîtres: Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Vous direz ceci à vos maîtres:
5 Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo.
C’est moi qui ai fait la terre, et les hommes et les hôtes qui sont sur la face de la terre, par ma grande puissance et par mon bras étendu; et j’ai donné la terre à celui qui a plu à mes yeux.
6 Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie.
Et c’est pourquoi moi j’ai maintenant mis toutes ces terres dans la maison de Nabuchodonosor, roi de Babylone, mon serviteur; de plus, je lui ai donné les bêtes de la campagne, afin qu’elles lui soient soumises.
7 Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.
Et toutes les nations lui seront soumises, à lui et à son fils, et au fils de son fils, jusqu’à ce que vienne le temps de son royaume et son propre temps, et beaucoup de nations et de grands rois lui seront soumis.
8 “‘“Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake.
Mais la nation et le royaume qui ne se soumettra pas à Nabuchodonosor, roi de Babylone, et quiconque ne courbera pas son cou sous le joug du roi de Babylone, c’est par le glaive, par la faim, et par la peste, que je visiterai cette nation, jusqu’à ce que je les aie consumés par sa main.
9 Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli.
Vous donc, n’écoutez pas vos prophètes, et vos devins et vos rêveurs, vos augures et vos magiciens, qui vous disent: Vous ne serez pas soumis au roi de Babylone.
10 Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia.
Parce qu’ils vous prophétisent un mensonge, afin de vous envoyer loin de votre terre, et de vous en chasser, et de vous faire périr.
11 Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.”’”
Or la nation qui mettra son cou sous le joug du roi de Babylone, et se soumettra à lui, je la laisserai dans sa terre, dit le Seigneur; et elle la cultivera, et elle y habitera.
12 Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi.
Et à Sédécias, roi de Juda, dans les mêmes termes j’ai parlé, disant: Mettez vos cous sous le joug du roi de Babylone, et soumettez-vous à lui et à son peuple, et vous vivrez.
13 Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli?
Pourquoi mourrez-vous, vous et votre peuple, par le glaive, et par la famine, et par la peste, comme l’a dit le Seigneur de la nation qui n’aura pas voulu se soumettre au roi de Babylone?
14 Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo.
N’écoutez pas les paroles des prophètes qui vous disent: Vous ne serez pas soumis au roi de Babylone; parce que c’est un mensonge qu’eux vous disent.
15 ‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’”
Parce que je ne les ai pas envoyés, dit le Seigneur, et ils prophétisent en mon nom faussement, afin de vous chasser de votre terre et de vous faire périr, vous et les prophètes qui vous prédisent l’avenir.
16 Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo.
Et j’ai parlé aux prêtres et à ce peuple, disant: Voici ce que dit le Seigneur: N’écoutez pas les paroles de vos prophètes qui vous prophétisent, disant: Voilà que les vases du Seigneur seront bientôt rapportés de Babylone; car c’est un mensonge qu’ils vous prophétisent.
17 Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu?
Ne les écoutez donc pas; mais soumettez-vous au roi de Babylone, afin que vous viviez; pourquoi cette cité sera-t-elle réduite en une solitude?
18 Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli.
Que s’ils sont prophètes et que la parole du Seigneur soit en eux, qu’ils s’opposent au Seigneur des armées, afin que les vases laissés dans la maison du Seigneur, et dans la maison du roi de Juda, et à Jérusalem, ne soient pas transférés à Babylone.
19 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu,
Parce que voici ce que dit le Seigneur des armées relativement aux colonnes, et à la mer, et aux bases, et aux restes des vases qui ont été laissés dans cette cité,
20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu.
Que n’emporta pas Nabuchodonosor, roi de Babylone, lorsqu’il transféra Jéchonias, fils de Joakim, roi de Juda, de Jérusalem à Babylone, et tous les grands de Juda et de Jérusalem;
21 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu:
Parce que, dis-je, voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël, relativement aux vases qui ont été laissés dans la maison du roi de Juda et dans Jérusalem:
22 ‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’”
Ils seront transportés à Babylone, et ils y seront jusqu’au jour de leur visite, dit le Seigneur; et je les ferai rapporter et rétablir en ce lieu.

< Yeremia 27 >