< Yeremia 27 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
In the bigynnyng of the rewme of Joachym, the sone of Josie, kyng of Juda, this word was maad of the Lord to Jeremye, and seide,
2 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi.
The Lord seith these thingis to me, Make thou to thee boondis and chaynes, and thou schalt putte tho in thi necke;
3 Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda.
and thou schalt sende tho to the kyng of Edom, and to the kyng of Moab, and to the kyng of the sones of Amon, and to the kyng of Tyre, and to the kyng of Sidon, bi the hond of messangeris that camen to Jerusalem, and to Sedechie, kyng of Juda.
4 Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu:
And thou schalt comaunde to hem, that thei speke to her lordis, The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Ye schulen seie these thingis to youre lordis,
5 Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo.
Y made erthe, and man, and beestis that ben on the face of al erthe, in my greet strengthe, and in myn arm holdun forth; and Y yaf it to hym that plesyde bifore myn iyen.
6 Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie.
And now therfor Y yaf alle these londis in the hond of Nabugodonosor, my seruaunt, the kyng of Babiloyne; ferthermore and Y yaf to hym the beestis of the feeld, that thei serue hym.
7 Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.
And alle folkis schulen serue hym, and his sone, and the sone of his sone, til the tyme of his lond and of hym come; and many folkis and grete kyngis schulen serue hym.
8 “‘“Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake.
Forsothe the folk and rewme that serueth not Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, and whoeuer bowith not his necke vndur the yok of the kyng of Babiloyne, Y schal visite on that folk in swerd, and hungur, and pestilence, seith the Lord, til Y waaste hem in his hond.
9 Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli.
Therfor nyle ye here youre profetis, and false dyuynouris, and dremeris, and dyuyneris bi chiteryng and fleyng of briddis, and witchis, that seien to you, Ye schulen not serue the kyng of Babiloyne;
10 Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia.
for thei profesien a lessyng to you, that thei make you fer fro youre lond, and caste out you, and ye perische.
11 Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.”’”
Certis the folk that makith suget her nol vndur the yok of the kyng of Babiloyne, and serueth hym, Y schal dismytte it in his lond, seith the Lord; and it schal tile that lond, and schal dwelle therynne.
12 Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi.
And Y spak bi alle these wordis to Sedechie, kyng of Juda, and Y seide, Make ye suget youre neckis vndur the yok of the kyng of Babiloyne, and serue ye hym, and his puple, and ye schulen lyue.
13 Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli?
Whi schulen ye die, thou and thi puple, bi swerd, and hungur, and pestilence, as the Lord spak to the folk, that nolde serue to the kyng of Babiloyne?
14 Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo.
Nyle ye here the wordis of profetis seiynge to you, Ye schulen not serue the kyng of Babiloyne; for thei speken leesyng to you, for Y sente not hem, seith the Lord;
15 ‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’”
and thei profesien falsly in my name, that thei caste out you, and that ye perische, bothe ye and the profetis that profesien to you.
16 Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo.
And Y spak to the preestis, and to this puple, and Y seide, The Lord God seith these thingis, Nyle ye here the wordis of youre profetis, that profesien to you, and seien, Lo! the vessels of the Lord schulen turne ayen now soone fro Babiloyne; for thei profesien a leesyng to you.
17 Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu?
Therfor nyle ye here hem, but serue ye to the kyng of Babiloyne, that ye lyue; whi is this citee youun in to wildirnesse?
18 Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli.
And if thei ben profetis, and if the word of God is in hem, renne thei to the Lord of oostis, that the vessels whiche weren left in the hous of the Lord, and in the hous of the kyng of Juda, and in Jerusalem, come not in to Babiloyne.
19 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu,
For the Lord of oostis seith these thingis to the pilers, and to the see, that is, a greet waischyng vessel, and to the foundementis, and to the remenauntis of vessels, that weren left in this citee,
20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu.
whiche Nabugodonosor, king of Babiloyne, took not, whanne he translatide Jeconye, the sone of Joachim, king of Juda, fro Jerusalem in to Babiloyne, and alle the principal men of Juda and of Jerusalem.
21 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu:
For the Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis to the vessels that ben left in the hous of the Lord, and in the hous of the king of Juda, and in Jerusalem, Tho schulen be translatid in to Babiloyne,
22 ‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’”
and schulen be there `til to the dai of her visitacioun, seith the Lord; and Y schal make tho to be brouyt, and to be restorid in this place.

< Yeremia 27 >