< Yeremia 27 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
In the beginning of the reign of Jehoiakim, the son of Josiah, the king of Judah, this word came to Jeremiah from the Lord, saying:
2 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi.
“Thus says the Lord to me: Make bands and chains for yourself. And you shall place them on your neck.
3 Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda.
And you shall send them to the king of Edom, and to the king of Moab, and to the king of the sons of Ammon, and to the king of Tyre, and to the king of Sidon, by the hand of the messengers who came to Jerusalem, to Zedekiah, the king of Judah.
4 Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu:
And you shall instruct them to say to their masters: Thus says the Lord of hosts, the God of Israel: You shall say these things to your masters:
5 Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo.
I made the earth, and the men and beasts which are upon the face of the earth, by my great strength and by my outstretched arm. And I have given it to whomever it was pleasing in my eyes.
6 Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie.
And now, therefore, I have given all these lands into the hand of Nebuchadnezzar, the king of Babylon, my servant. Moreover, I have given to him also the beasts of the field, so that they may serve him.
7 Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.
And all the nations will serve him, and his son, and his son’s son. Many nations and great kings will serve him, until the time arrives for him and his land.
8 “‘“Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake.
But the nation or kingdom that will not serve Nebuchadnezzar, the king of Babylon, and whoever will not bend his neck under the yoke of the king of Babylon, I will visit upon that nation with the sword, and with famine, and with pestilence, says the Lord, until I consume them by his hand.
9 Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli.
Therefore, you should not choose to listen to your own prophets, and diviners, and dreamers, and soothsayers, and sorcerers, who say to you: ‘You shall not serve the king of Babylon.’
10 Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia.
For they prophesy lies to you, so that they may cause you to be far from your own country, and may cast you out, and may cause you to perish.
11 Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.”’”
Furthermore, the nation which will bend its neck under the yoke of the king of Babylon, and which will serve him, I will permit them to remain in their own land, says the Lord. And they will cultivate it, and they will live in it.”
12 Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi.
And I spoke to Zedekiah, the king of Judah, according to all these words, saying: “Subject your necks under the yoke of the king of Babylon, and serve him and his people, and you will live.
13 Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli?
Why should you suffer death, you and your people, by the sword, and famine, and pestilence, just as the Lord has spoken against any nation that refuses to serve the king of Babylon?
14 Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo.
Do not choose to listen to the words of the prophets, saying to you: ‘You will not serve the king of Babylon.’ For they are speaking a lie to you.
15 ‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’”
For I have not sent them, says the Lord. And they prophesy falsely in my name, so that they may cast you out, and so that you may perish, both you and the prophets who make predictions for you.”
16 Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo.
I spoke also to the priests and to this people, saying: “Thus says the Lord: Do not choose to listen to the words of your prophets, who prophesy to you, saying: ‘Behold, the vessels of the Lord will now quickly be returned from Babylon.’ For they are prophesying to you a lie.
17 Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu?
Therefore, do not choose to listen to them, but instead, serve the king of Babylon, so that you may live. Why should this city be given over into desolation?
18 Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli.
But if they are prophets, and if the word of the Lord is in them, then let them intercede before the Lord of hosts, so that the vessels that were left behind in the house of the Lord, and in the house of the king of Judah, and in Jerusalem, may not go to Babylon.
19 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu,
For thus says the Lord of hosts to the pillars, and to the sea of brass, and to the bases, and to the remainder of the vessels that have been left behind in this city,
20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu.
which Nebuchadnezzar, the king of Babylon, did not take when he carried away Jeconiah, the son of Jehoiakim, the king of Judah, from Jerusalem into Babylon, with all the nobility of Judah and Jerusalem:
21 Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu:
For thus says the Lord of hosts, the God of Israel, to the vessels that were left behind in the house of the Lord and in the house of the king of Judah and Jerusalem:
22 ‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’”
They shall be carried away to Babylon, and there they shall be, until the day of their visitation, says the Lord. And then I will cause them to be carried back, and to be restored to this place.

< Yeremia 27 >