< Yeremia 26 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Bwana:
Au commencement du règne de Joakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole du Seigneur me fut adressée, disant:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo: Simama katika ua wa nyumba ya Bwana na useme na watu wote wa miji ya Yuda wanaokuja kuabudu katika nyumba ya Bwana. Waambie kila kitu nitakachokuamuru, usipunguze neno.
Voici ce que dit le Seigneur: Tiens-toi dans le parvis de la maison du Seigneur, et tu diras à toutes les cités de Juda d’où l’on vient afin d’adorer dans la maison du Seigneur, tous les discours que moi je t’ai commandé de leur adresser; ne retranche pas une parole,
3 Huenda watasikiliza, na kila mmoja akageuka kutoka njia yake mbaya. Kisha nitawahurumia na kuacha kuwaletea maafa niliyokuwa ninapanga kwa sababu ya maovu waliyofanya.
Pour voir si par hasard ils écouteront, et s’ils se convertiront, chacun de sa voie mauvaise, et je me repentirai du mal que je pense leur faire, à cause de la malice de leurs œuvres.
4 Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ikiwa hamtanisikiliza na kuifuata sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu,
Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur: Si vous ne m’écoutez pas, quand j’ordonne que vous marchiez dans ma loi que je vous ai donnée,
5 nanyi ikiwa hamtayasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao nimewatuma kwenu tena na tena (ijapokuwa hamkuwasikiliza),
Et que vous entendiez les paroles de mes serviteurs les prophètes, que moi j’ai envoyés vers vous, me levant durant la nuit et les dirigeant, et que vous n’avez pas écoutés,
6 ndipo nitaifanya nyumba hii kama Shilo na mji huu kuwa kitu cha kulaaniwa na mataifa yote ya dunia.’”
Je rendrai cette maison comme Silo, et je livrerai cette ville en malédiction à toutes les nations de la terre.
7 Makuhani, manabii na watu wote wakamsikia Yeremia akiyasema maneno haya ndani ya nyumba ya Bwana.
Et les prêtres et les prophètes et tout le peuple entendirent Jérémie disant ces paroles dans la maison du Seigneur.
8 Lakini mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu kila kitu Bwana alichomwamuru kukisema, basi makuhani, manabii na watu wote walimkamata wakisema, “Ni lazima ufe!
Et lorsque Jérémie eut achevé de dire tout ce que le Seigneur lui avait ordonné de dire à tout le peuple, les prêtres et les prophètes et tout le peuple le saisirent, disant: Qu’il meure de mort.
9 Kwa nini unatoa unabii katika jina la Bwana kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa na kuachwa tupu?” Nao watu wote wakamkusanyikia na kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Bwana.
Pourquoi a-t-il prophétisé au nom du Seigneur, disant: Comme Silo, ainsi sera cette maison; et cette ville sera désolée, pour qu’il n’y ait pas d’habitant? Et tout le peuple s’assembla contre Jérémie dans la maison du Seigneur.
10 Maafisa wa Yuda waliposikia kuhusu mambo haya, wakapanda kutoka jumba la kifalme, wakaenda katika nyumba ya Bwana na kushika nafasi zao kwenye ingilio la Lango Jipya la nyumba ya Bwana.
Et les princes de Juda entendirent ces paroles; et ils montèrent de la maison du roi dans la maison du Seigneur, et ils s’assirent à l’entrée de la porte neuve de la maison du Seigneur.
11 Kisha makuhani na manabii wakawaambia maafisa pamoja na watu wote, “Mtu huyu anastahili ahukumiwe kifo kwa sababu ametoa unabii mbaya dhidi ya mji huu. Mmesikia kwa masikio yenu wenyewe!”
Et les prêtres et les prophètes parièrent aux princes et à tout le peuple, disant: Un jugement de mort est dû à cet homme, parce qu’il a prophétisé contre cette cité, comme vous l’avez entendu de vos oreilles.
12 Kisha Yeremia akawaambia maafisa wote na watu wote: “Bwana amenituma kutoa unabii dhidi ya nyumba hii na mji huu mambo yote mliyoyasikia.
Et Jérémie parla à tous les princes et à tout le peuple, disant: Le Seigneur m’a envoyé, afin de prophétiser à cette maison et à cette cité toutes les choses que vous avez entendues.
13 Sasa tengenezeni njia zenu na matendo yenu, na kumtii Bwana Mungu wenu. Ndipo Bwana atawahurumia na kuacha kuleta maafa aliyokuwa ameyatamka dhidi yenu.
Maintenant donc rendez droites vos voies et vos œuvres, et écoutez la voix du Seigneur votre Dieu; et le Seigneur se repentira du mal qu’il a annoncé contre vous.
14 Lakini kwa habari yangu mimi, niko mikononi mwenu, nifanyieni lolote mnaloona kuwa ni jema na la haki.
Pour moi, voici que je suis entre vos mains; faites-moi ce qui paraît bon et juste à vos yeux;
15 Hata hivyo, jueni kwa hakika, ikiwa mtaniua, mtakuwa mmejipatia dhambi kwa damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe, na juu ya mji huu na wote wanaoishi ndani yake, kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu ili niseme maneno haya yote masikioni mwenu.”
Mais cependant, sachez et apprenez bien que, si vous me faites mourir, vous répandrez un sang innocent contre vous et contre cette cité et ses habitants; car, en vérité, le Seigneur m’a envoyé vers vous, pour que je fisse entendre à vos oreilles toutes ces choses.
16 Kisha maafisa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii, “Mtu huyu asihukumiwe kifo! Amesema nasi katika jina la Bwana, Mungu wetu.”
Et les princes et tout le peuple dirent aux prêtres et aux prophètes: Un jugement de mort n’est pas dû à cet homme, parce que c’est au nom du Seigneur, notre Dieu, qu’il nous a parlé.
17 Baadhi ya wazee wa nchi wakasogea mbele, wakaliambia kusanyiko lote la watu,
Des hommes donc, d’entre les anciens du pays, se levèrent, et ils dirent à toute l’assemblée du peuple, en prenant la parole:
18 “Mika Mmoreshethi alitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “‘Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.’
Michée de Morasthie fut prophète dans les jours d’Ezéchias, roi de Juda, et parla à tout le peuple de Juda, disant: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Sion, comme un champ, sera labourée, et Jérusalem sera réduite en un monceau de pierres, et la montagne de la maison en une haute forêt.
19 Je, Hezekia mfalme wa Yuda au mtu mwingine yeyote katika Yuda alimhukumu Mika kufa? Je, Hezekia hakumcha Bwana na kuhitaji msaada wake? Je, Bwana hakuwahurumia na akaacha kuleta maafa aliyokuwa ametamka dhidi yao? Tunakaribia sana kujiletea maangamizo ya kutisha sisi wenyewe!”
Est-ce qu’Ezéchias, roi de Juda, et tout Juda l’ont condamné à mort? Est-ce qu’ils ne craignirent pas le Seigneur, et ne supplièrent-ils pas la face du Seigneur, et le Seigneur ne se repentit-il pas des maux qu’il avait annoncés contre eux? C’est pourquoi nous faisons un grand mal contre nos âmes.
20 (Wakati huu, Uria mwana wa Shemaya kutoka mji wa Kiriath-Yearimu alikuwa mtu mwingine aliyetoa unabii kwa jina la Bwana. Alitoa unabii juu ya mambo yaliyofanana na haya dhidi ya mji huu na nchi hii kama alivyofanya Yeremia.
Il y eut aussi un homme prophétisant au nom du Seigneur, Urie, fils de Séméi, de Cariathiarim; et il prophétisa contre cette cité, et contre cette terre, selon toutes les paroles de Jérémie.
21 Mfalme Yehoyakimu na wakuu wake wote na maafisa waliposikia maneno yake, mfalme alitafuta kumuua. Lakini Uria alipata habari, na kwa kuogopa akakimbilia Misri.
Et le roi Joakim, et tous les puissants et ses princes entendirent ces paroles; et le roi chercha à le tuer. Et Urie l’apprit, et il craignit, et s’enfuit, et il entra en Egypte.
22 Hata hivyo, Mfalme Yehoyakimu alimtuma Elnathani mwana wa Akbori huko Misri, pamoja na watu wengine ili kwenda kumkamata Uria.
Et le roi Joakim envoya des hommes en Egypte, Elnathan, fils d’Achabor, et des hommes avec lui en Egypte.
23 Wakamrudisha Uria kutoka Misri na kumpeleka kwa Mfalme Yehoyakimu, ambaye alimuua kwa upanga, na mwili wake kutupwa kwenye eneo la makaburi ya watu wasio na cheo.)
Et ils tirèrent Urie d’Egypte, et ils l’amenèrent au roi Joakim, et il le frappa du glaive, et il jeta son cadavre dans les sépulcres des derniers du peuple.
24 Zaidi ya hayo, Ahikamu mwana wa Shafani akamuunga mkono Yeremia, kwa hiyo hakutiwa tena mikononi mwa watu ili auawe.
Donc la main d’Ahicam, fils de Saphan, fut avec Jérémie, afin qu’il ne fût pas livré aux mains du peuple, et qu’on ne le tuât pas.

< Yeremia 26 >