< Yeremia 26 >

1 Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Bwana:
I Begyndelsen af Jojakims, Josias's Søns, Judas Konges Regering kom dette Ord fra Herren saalunde:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo: Simama katika ua wa nyumba ya Bwana na useme na watu wote wa miji ya Yuda wanaokuja kuabudu katika nyumba ya Bwana. Waambie kila kitu nitakachokuamuru, usipunguze neno.
Saa siger Herren: Stil dig i Herrens Hus's Forgaard, og tal til alle Judas Stæder, som komme for at tilbede i Herrens Hus, alle de Ord, som jeg har befalet dig at tale til dem, du skal ikke tage et Ord derfra.
3 Huenda watasikiliza, na kila mmoja akageuka kutoka njia yake mbaya. Kisha nitawahurumia na kuacha kuwaletea maafa niliyokuwa ninapanga kwa sababu ya maovu waliyofanya.
Maaske de vilde høre og omvende sig, hver fra sin onde Vej, og jeg maatte angre det onde, som jeg tænker at gøre imod dem, for deres Idrætters Ondskabs Skyld.
4 Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ikiwa hamtanisikiliza na kuifuata sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu,
Og du skal sige til dem: Saa siger Herren: Dersom I ikke høre mig om at vandre i min Lov, som jeg har sat for eders Ansigt,
5 nanyi ikiwa hamtayasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao nimewatuma kwenu tena na tena (ijapokuwa hamkuwasikiliza),
og om at høre paa mine Tjeneres, Profeternes Ord, som jeg sender til eder, baade tidligt og ideligt, uden at I have villet høre dem:
6 ndipo nitaifanya nyumba hii kama Shilo na mji huu kuwa kitu cha kulaaniwa na mataifa yote ya dunia.’”
Saa vil jeg gøre dette Hus ligt med Silo og gøre denne Stad til en Forbandelse for alle Folkefærd paa Jorden.
7 Makuhani, manabii na watu wote wakamsikia Yeremia akiyasema maneno haya ndani ya nyumba ya Bwana.
Og Præsterne og Profeterne og alt Folket hørte, at Jeremias talte disse Ord i Herrens Hus.
8 Lakini mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu kila kitu Bwana alichomwamuru kukisema, basi makuhani, manabii na watu wote walimkamata wakisema, “Ni lazima ufe!
Og det skete, der Jeremias var færdig med at tale alt det, som Herren havde befalet ham at tale til alt Folket, da grebe Præsterne og Profeterne og alt Folket ham og sagde: Du skal visselig dø!
9 Kwa nini unatoa unabii katika jina la Bwana kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa na kuachwa tupu?” Nao watu wote wakamkusanyikia na kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Bwana.
Hvorfor spaaede du i Herrens Navn og sagde: Dette Hus skal blive ligesom Silo, og denne Stad skal ødelægges, saa at ingen skal bo der? Og alt Folket samlede sig imod Jeremias i Herrens Hus.
10 Maafisa wa Yuda waliposikia kuhusu mambo haya, wakapanda kutoka jumba la kifalme, wakaenda katika nyumba ya Bwana na kushika nafasi zao kwenye ingilio la Lango Jipya la nyumba ya Bwana.
Og Judas Fyrster hørte disse Ord, og de gik op fra Kongens Hus og til Herrens Hus, og de satte sig ved Indgangen til Herrens nye Port.
11 Kisha makuhani na manabii wakawaambia maafisa pamoja na watu wote, “Mtu huyu anastahili ahukumiwe kifo kwa sababu ametoa unabii mbaya dhidi ya mji huu. Mmesikia kwa masikio yenu wenyewe!”
Og Præsterne og Profeterne sagde til Fyrsterne og til alt Folket saaledes: Dødsdom over denne Mand! thi han har spaaet imod denne Stad, saaledes som I have hørt med eders Øren.
12 Kisha Yeremia akawaambia maafisa wote na watu wote: “Bwana amenituma kutoa unabii dhidi ya nyumba hii na mji huu mambo yote mliyoyasikia.
Men Jeremias sagde til alle Fyrsterne og til alt Folket saaledes: Herren har sendt mig til at spaa imod dette Hus og imod denne Stad og til at forkynde alle de Ord, som I have hørt.
13 Sasa tengenezeni njia zenu na matendo yenu, na kumtii Bwana Mungu wenu. Ndipo Bwana atawahurumia na kuacha kuleta maafa aliyokuwa ameyatamka dhidi yenu.
Saa bedrer nu eders Veje og eders Idrætter, og hører Herren eders Guds Røst, saa skal Herren angre det onde, som han har talt imod eder.
14 Lakini kwa habari yangu mimi, niko mikononi mwenu, nifanyieni lolote mnaloona kuwa ni jema na la haki.
Og jeg, se! jeg er i eders Haand; gører imod mig, som det er godt, og som det er ret for eders Øjne.
15 Hata hivyo, jueni kwa hakika, ikiwa mtaniua, mtakuwa mmejipatia dhambi kwa damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe, na juu ya mji huu na wote wanaoishi ndani yake, kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu ili niseme maneno haya yote masikioni mwenu.”
Kun det skulle I vide, at dersom I dræbe mig, da ville I bringe uskyldigt Blod over eder og over denne Stad og over dens Indbyggere; thi i Sandhed, Herren har sendt mig til eder for at tale alle disse Ord for eders Øren.
16 Kisha maafisa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii, “Mtu huyu asihukumiwe kifo! Amesema nasi katika jina la Bwana, Mungu wetu.”
Da sagde Fyrsterne og alt Folket til Præsterne og til Profeterne: Der bør ingen Dødsdom fældes over denne Mand; thi har han talt til os i Herren vor Guds Navn.
17 Baadhi ya wazee wa nchi wakasogea mbele, wakaliambia kusanyiko lote la watu,
Og nogle Mænd af de Ældste i Landet stode op, og de sagde til hele Folkets Forsamling saaledes:
18 “Mika Mmoreshethi alitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “‘Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.’
Morasktiten Mika spaaede i Ezekias's, Judas Konges Dage, og sagde til alt Judas Folk: Saa siger den Herre Zebaoth: Zion skal pløjes som en Ager og Jerusalem blive til Stenhobe og Husets Bjerg til Skovhøje.
19 Je, Hezekia mfalme wa Yuda au mtu mwingine yeyote katika Yuda alimhukumu Mika kufa? Je, Hezekia hakumcha Bwana na kuhitaji msaada wake? Je, Bwana hakuwahurumia na akaacha kuleta maafa aliyokuwa ametamka dhidi yao? Tunakaribia sana kujiletea maangamizo ya kutisha sisi wenyewe!”
Mon Ezekias, Judas Konge, og al Juda straks dræbte ham? frygtede han ikke Herren og bad ydmygt for Herrens Ansigt, saa at Herren angrede det onde, som han havde talt imod dem? og vi, vi bringe en stor Ulykke over vore Sjæle.
20 (Wakati huu, Uria mwana wa Shemaya kutoka mji wa Kiriath-Yearimu alikuwa mtu mwingine aliyetoa unabii kwa jina la Bwana. Alitoa unabii juu ya mambo yaliyofanana na haya dhidi ya mji huu na nchi hii kama alivyofanya Yeremia.
Der var ogsaa en Mand, som spaaede i Herrens Navn, Urias, Semajas's Søn, fra Kirjath-Jearim; og han spaaede imod denne Stad og imod dette Land, aldeles som Jeremias's Ord vare.
21 Mfalme Yehoyakimu na wakuu wake wote na maafisa waliposikia maneno yake, mfalme alitafuta kumuua. Lakini Uria alipata habari, na kwa kuogopa akakimbilia Misri.
Og Kong Jojakim og alle hans vældige og alle Fyrsterne hørte hans Ord, og Kongen søgte at dræbe ham; men Urias hørte det og frygtede og flyede og kom til Ægypten.
22 Hata hivyo, Mfalme Yehoyakimu alimtuma Elnathani mwana wa Akbori huko Misri, pamoja na watu wengine ili kwenda kumkamata Uria.
Men Kong Jojakim sendte Mænd til Ægypten, nemlig Elnatan, Akbors Søn, og nogle Mænd med ham til Ægypten.
23 Wakamrudisha Uria kutoka Misri na kumpeleka kwa Mfalme Yehoyakimu, ambaye alimuua kwa upanga, na mwili wake kutupwa kwenye eneo la makaburi ya watu wasio na cheo.)
Og de førte Urias fra Ægypten og bragte ham til Kong Jojakim, og denne slog ham ihjel med Sværdet og lod hans døde Krop kaste i de meniges Grave.
24 Zaidi ya hayo, Ahikamu mwana wa Shafani akamuunga mkono Yeremia, kwa hiyo hakutiwa tena mikononi mwa watu ili auawe.
Kun Ahikams, Safans Søns, Haand var med Jeremias, saa at man ikke gav ham i Folkets Haand til at dræbes.

< Yeremia 26 >