< Yeremia 25 >

1 Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
Yahuda Kralı Yoşiya oğlu Yehoyakim'in döneminin dördüncü yılında, RAB Yahuda halkıyla ilgili olarak Yeremya'ya seslendi. Nebukadnessar'ın Babil Kralı oluşunun birinci yılıydı bu.
2 Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
Peygamber Yeremya Yahuda halkına ve Yeruşalim'de yaşayanlara RAB'bin sözünü aktararak şöyle dedi:
3 Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
Yirmi üç yıldır, Yahuda Kralı Amon oğlu Yoşiya'nın döneminin on üçüncü yılından bugüne dek, RAB bana sesleniyor. Ben de RAB'bin sözünü defalarca size aktardım, ama dinlemediniz.
4 Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
RAB peygamber kullarını defalarca size gönderdi, ama dinlemediniz, kulak asmadınız.
5 Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
Sizi uyardılar, “Şimdi herkes kötü yolundan, kötü işlerinden dönsün ki, RAB'bin sonsuza dek size ve atalarınıza verdiği toprakta yaşayasınız” dediler,
6 Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
“Kulluk etmek, tapınmak için başka ilahların ardınca gitmeyin; elinizle yaptığınız putlarla beni öfkelendirmeyin ki, ben de size zarar vermeyeyim.”
7 “Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
“Ama beni dinlemediniz” diyor RAB, “Sonuç olarak elinizle yaptığınız putlarla beni öfkelendirip kendinizi zarara soktunuz.”
8 Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
Bunun için Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Madem sözlerimi dinlemediniz,
9 nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
ben de bütün kuzeydeki halkları ve kulum Babil Kralı Nebukadnessar'ı çağırtacağım” diyor RAB, “Onları bu ülkeye de burada yaşayanlarla çevresindeki bütün uluslara da karşı getireceğim. Bu halkı tamamen yok edeceğim, ülkelerini dehşet ve alay konusu edip sonsuz bir viraneye çevireceğim.
10 Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
Sevinç ve neşe sesini, gelin güvey sesini, değirmen taşlarının sesini, kandil ışığını onlardan uzaklaştıracağım.
11 Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
Bütün ülke bir virane, dehşet verici bir yer olacak. Bu uluslar Babil Kralı'na yetmiş yıl kulluk edecekler.
12 “Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
“Ama yetmiş yıl dolunca” diyor RAB, “Suçları yüzünden Babil Kralı'yla ulusunu, Kildan ülkesini cezalandıracak, sonsuz bir viranelik haline getireceğim.
13 Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
O ülke için söylediklerimin hepsini, Yeremya'nın uluslara ettiği bu kitapta yazılı bütün peygamberlik sözlerini ülkenin başına getireceğim.
14 Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
Pek çok ulus, büyük krallar onları köle edinecek. Yaptıklarına ve ellerinden çıkan işe göre karşılık vereceğim onlara.”
15 Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
İsrail'in Tanrısı RAB bana şöyle dedi: “Elimdeki öfke şarabıyla dolu kâseyi al, seni göndereceğim bütün uluslara içir.
16 Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
Şarabı içince sendeleyecek, üzerlerine göndereceğim kılıç yüzünden çıldıracaklar.”
17 Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
Böylece kâseyi RAB'bin elinden alıp beni gönderdiği bütün uluslara içirdim:
18 Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
Bugün olduğu gibi viranelik, dehşet ve alay konusu, lanetlik olsunlar diye Yeruşalim'e, Yahuda kentlerine, krallarıyla önderlerine;
19 pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
Firavunla görevlilerine, önderlerine ve halkına,
20 pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
Mısır'da yaşayan bütün yabancılara; Ûs krallarına, Filist krallarına –Aşkelon'a, Gazze'ye, Ekron'a, Aşdot'tan sağ kalanlara–
21 Edomu, Moabu na Amoni;
Edom'a, Moav'a, Ammon'a;
22 wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
bütün Sur ve Sayda krallarına, deniz aşırı ülkelerin krallarına;
23 Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
Dedan'a, Tema'ya, Bûz'a, zülüflerini kesen bütün halklara;
24 wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
Arabistan krallarına, çölde yaşayan yabancı halkın krallarına;
25 wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
Zimri, Elam, Med krallarına;
26 na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
sırasıyla uzak yakın bütün kuzey krallarına, yeryüzündeki bütün ulusların krallarına içirdim. Hepsinden sonra Şeşak Kralı da içecektir.
27 “Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
“Sonra onlara de ki, ‘İsrail'in Tanrısı, Her Şeye Egemen RAB şöyle diyor: Üzerinize salacağım kılıç yüzünden sarhoş olana dek için, kusun, düşüp kalkmayın.’
28 Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
Eğer kâseyi elinden alır, içmek istemezlerse, de ki, ‘Her Şeye Egemen RAB şöyle diyor: Kesinlikle içeceksiniz!
29 Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
Bana ait olan kentin üzerine felaket getirmeye başlıyorum. Cezasız kalacağınızı mı sanıyorsunuz? Sizi cezasız bırakmayacağım. İşte dünyada yaşayan herkesin üzerine kılıcı çağırıyorum. Her Şeye Egemen RAB böyle diyor.’
30 “Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
“Bütün bu peygamberlik sözlerini onlara ilet: “‘Yükseklerden kükreyecek RAB, Kutsal konutundan gürleyecek, Ağılına şiddetle kükreyecek. Dünyada yaşayanların tümüne Üzüm ezenler gibi bağıracak.
31 Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
Gürültü yeryüzünün dört yanında yankılanacak. Çünkü RAB uluslara dava açacak; Herkesi yargılayacak Ve kötüleri kılıca teslim edecek’” diyor RAB.
32 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “İşte felaket ulustan ulusa yayılıyor! Dünyanın dört bucağından büyük kasırga kopuyor.”
33 Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
O gün RAB dünyayı bir uçtan bir uca öldürülenlerle dolduracak. Onlar için yas tutulmayacak, toplanıp gömülmeyecekler. Toprağın üzerinde gübre gibi kalacaklar.
34 Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
Haykırın, ey çobanlar, Acı acı bağırın! Toprakta yuvarlanın, ey sürü başları! Çünkü boğazlanma zamanınız doldu, Değerli bir kap gibi düşüp parçalanacaksınız.
35 Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
Çobanlar kaçamayacak, Sürü başları kurtulamayacak!
36 Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
Duy çobanların haykırışını, Sürü başlarının bağırışını! RAB onların otlaklarını yok ediyor.
37 Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
RAB'bin kızgın öfkesi yüzünden Güvenlikte oldukları ağıllar yok oldu.
38 Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.
İnini terk eden genç aslan gibi, RAB inini bıraktı. Zorbanın kılıcı Ve RAB'bin kızgın öfkesi yüzünden Ülkeleri viraneye döndü.

< Yeremia 25 >