< Yeremia 25 >

1 Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
La palabra que vino a Jeremías acerca de todo el pueblo de Judá en el cuarto año de Joacim, hijo de Josías, rey de Judá; Este fue el primer año de Nabucodonosor, rey de Babilonia.
2 Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
Esta palabra Jeremías repartió a todo el pueblo de Judá y a los que viven en Jerusalén, diciendo:
3 Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
Desde el año trece de Josías, hijo de Amón, rey de Judá, hasta el día de hoy, durante veintitrés años, la palabra del Señor ha venido a mí, levantándose temprano, y te la he dado y he hablado con ustedes; pero no le has dado oído.
4 Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
Y el Señor te envió a todos sus siervos los profetas, levantándose temprano y hablándoles; pero no han prestado atención y su oído no ha estado abierto para escuchar;
5 Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
Diciendo: Regresen ahora, todos, de su mal camino y del mal de sus obras, y guarden su lugar en la tierra que el Señor les ha dado a ustedes y a sus padres, desde tiempos remotos, incluso para siempre:
6 Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
No vayas tras otros dioses para ser sus sirvientes y darles adoración, y no me hagan enojar con la obra de sus manos, y no les haré ningún mal.
7 “Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
Pero no me han oído, dice el Señor; así que me han hecho enojar con la obra de sus manos, causando el mal a ustedes mismos.
8 Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos: Porque no has escuchado mis palabras,
9 nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
Mira, enviaré y tomaré a todas las familias del norte, dice el Señor, y Nabucodonosor, rey de Babilonia, mi siervo, y haré que vengan contra esta tierra, y contra su pueblo, y contra todas estas naciones por todos lados; y los entregaré a la destrucción completa, y los convertiré en una causa de espanto, burla y desolación y para siempre.
10 Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
Y más que esto, tomaré de ellos el sonido de voces de gozo, la voz de alegría, la voz del hombre recién casado y la voz de la novia, el sonido de las piedras aplastando el grano, y el brillo de las luces.
11 Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
Toda esta tierra será ruinas y desolación; y estas naciones serán los siervos del rey de Babilonia por setenta años.
12 “Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
Y después de que hayan transcurrido setenta años, sucederá que enviaré castigo al rey de Babilonia y a esa nación, dice el Señor, por su maldad y sobre la tierra de los caldeos; Y lo haré una desolación para siempre.
13 Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
Y haré que esa tierra se someta a todo lo que he dicho en contra, incluso a todo lo que figura en este libro, que el profeta Jeremías dijo contra todas las naciones.
14 Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
Porque varias naciones y grandes reyes harán de ellos sirvientes, incluso de ellos; y les daré la recompensa de sus actos, incluso la recompensa de la obra de sus manos.
15 Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
Porque esto es lo que el Señor, el Dios de Israel, me ha dicho: Toma de la mano la copa del vino de esta ira, y haz que tomen de ella todas las naciones a las que te envío.
16 Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
Y después de beberlo, se moverán violentamente, y se enloquecerán, a causa de la espada que enviaré entre ellas.
17 Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
Entonces tomé la copa de la mano del Señor, y di de ella una bebida a todas las naciones a quienes el Señor me envió;
18 Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
Jerusalén y los pueblos de Judá y sus reyes y sus príncipes, para convertirlos en un lugar desolado, causa de horror, burla y espanto como una maldición, como lo es este día;
19 pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
Faraón, rey de Egipto, y sus siervos y sus príncipes y todo su pueblo;
20 pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
Y todas las personas mixtas y todos los reyes de la tierra de Uz, y todos los reyes de la tierra de los filisteos, y Ascalón y Gaza y Ecrón y el resto de Asdod;
21 Edomu, Moabu na Amoni;
Edom y Moab y los hijos de Amón,
22 wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
Y todos los reyes de Tiro, y todos los reyes de Sidón, y los reyes de las tierras al otro lado del mar;
23 Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
Dedán y Tema y Buz, y hasta lo más recóndito de la tierra;
24 wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
Y todos los reyes de Arabia, y todos los reyes de las diversas razas que viven en el desierto;
25 wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
Y todos los reyes de Zimri, y todos los reyes de Elam, y todos los reyes de los medos;
26 na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
Y todos los reyes del norte, lejanos y cercanos, unos con otros; y todos los reinos del mundo sobre la faz de la tierra. por último beberá él rey de babilonia.
27 “Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
Y debes decirles: Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos, el Dios de Israel: Tomen de esta copa y emborráchense, vomiten, y que caigan al suelo para no levantarse; por la espada que enviaré en medio de ustedes.
28 Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
Y será que si no toman la copa en tu mano, entonces debes decirles: Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos: Ciertamente la beberás.
29 Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
Para ver, estoy empezando a enviar el mal a la ciudad que se llama por Mí nombre, ¿y estarás sin castigo? No estarás sin castigo, porque enviaré una espada a todas las personas que viven en la tierra, dice el Señor de los ejércitos.
30 “Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
Entonces, como profeta, di estas palabras entre ellos y diles: La voz del Señor sonará como un rugido de león de lo alto; enviará su voz desde su lugar santo, como él rugir de un león, contra su rebaño; Él dará un grito, como los que están triturando las uvas, contra todas las personas de la tierra.
31 Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
Un ruido vendrá hasta el fin de la tierra; porque el Señor tiene una causa contra las naciones, él dará su decisión contra toda carne; En cuanto a los que hacen el mal, los entregará a la espada, dice el Señor.
32 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
Esto es lo que dijo el Señor de los ejércitos: mira, el mal está saliendo de nación en nación, y una gran tormenta subirá desde las partes más internas de la tierra.
33 Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
Y en ese día, los cuerpos de aquellos a quienes el Señor ha dado muerte serán vistos desde un extremo de la tierra hasta el otro extremo de la tierra; no habrá llanto para ellos, nadie recogerá sus cadáveres para enterrarlos; serán como estiércol sobre la faz de la tierra.
34 Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
Den gritos de dolor, pastores de ovejas; Griten pidiendo ayuda, revuélquense en la ceniza, guías del rebaño, porque han llegado los días de su destrucción y matanza; los enviaré en todas direcciones, y su caída será como vaso preciado.
35 Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
No habrá forma de huir para los poseedores de ovejas, ni camino para que los jefes del rebaño escapen sanos y salvos.
36 Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
¡Voz del clamor de los pastores de las ovejas, y el amargo llanto de los mayorales del rebaño! porque el Señor ha hecho perder sus verdes campos.
37 Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
Y no hay sonido en los campos apacibles, a causa de la ira ardiente del Señor.
38 Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.
El león ha salido de su lugar secreto, porque la tierra se ha convertido en desolación debido a la espada opresora y al calor de su ira.

< Yeremia 25 >