< Yeremia 25 >

1 Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
La parole qui fut adressée à Jérémie sur tout le peuple de Juda, la quatrième année de Jojakim, fils de Josias, roi de Juda (c'était la première année de Nabuchodonosor, roi de Babylone),
2 Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
parole que Jérémie, le prophète, adressa à tout le peuple de Juda et à tous les habitants de Jérusalem:
3 Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
Depuis la treizième année de Josias, fils d'Amon, roi de Juda, jusqu'à ce jour, c'est-à-dire depuis vingt-trois ans, la parole de Yahvé m'a été adressée, et je vous ai parlé, me levant de bonne heure et parlant; mais vous n'avez pas écouté.
4 Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
L'Éternel vous a envoyé tous ses serviteurs, les prophètes, en se levant de bonne heure et en les envoyant (mais vous n'avez pas écouté ni prêté l'oreille pour entendre),
5 Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
en disant: « Que chacun revienne maintenant de sa mauvaise voie et de la méchanceté de ses actions, et qu'il habite dans le pays que l'Éternel a donné à vous et à vos pères, depuis toujours et à jamais.
6 Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
N'allez pas après d'autres dieux pour les servir ou vous prosterner devant eux, et ne m'irritez pas par l'œuvre de vos mains; alors je ne vous ferai aucun mal. »
7 “Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
« Mais vous ne m'avez pas écouté, dit l'Éternel, afin de m'irriter par l'ouvrage de vos mains, pour votre propre malheur. »
8 Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
C'est pourquoi Yahvé des armées dit: « Parce que vous n'avez pas écouté mes paroles,
9 nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
voici, j'enverrai prendre toutes les familles du nord, dit Yahvé, et j'enverrai mon serviteur Nebucadnetsar, roi de Babylone, et je les ferai venir contre ce pays, contre ses habitants et contre toutes ces nations d'alentour. Je les détruirai par interdit, et j'en ferai un objet d'étonnement, de sifflement et de désolation perpétuelle.
10 Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
Je leur enlèverai la voix de la joie et la voix de l'allégresse, la voix du fiancé et la voix de la fiancée, le bruit des meules et la lumière de la lampe.
11 Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
Tout ce pays sera une désolation et un objet d'épouvante, et ces nations serviront le roi de Babylone pendant soixante-dix ans.
12 “Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
« Quand soixante-dix ans seront accomplis, je punirai le roi de Babylone et cette nation, dit Yahvé, à cause de leur iniquité. Je réduirai le pays des Chaldéens en désolation pour toujours.
13 Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
Je ferai venir sur ce pays toutes les paroles que j'ai prononcées contre lui, tout ce qui est écrit dans ce livre, et que Jérémie a prophétisé contre toutes les nations.
14 Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
Car beaucoup de nations et de grands rois en feront des esclaves, même d'eux. Je leur rendrai selon leurs actes et selon l'œuvre de leurs mains. »
15 Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
Car Yahvé, le Dieu d'Israël, me dit: « Prends de ma main cette coupe du vin de la colère, et fais-la boire à toutes les nations vers lesquelles je t'envoie.
16 Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
Ils boiront, ils tituberont et seront fous, à cause de l'épée que j'enverrai au milieu d'eux. »
17 Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
Puis j'ai pris la coupe dans la main de Yahvé, et j'ai fait boire toutes les nations vers lesquelles Yahvé m'avait envoyé:
18 Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
Jérusalem et les villes de Juda, avec ses rois et ses chefs, pour en faire une désolation, un objet d'étonnement, de sifflement et de malédiction, comme il en existe aujourd'hui;
19 pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
Pharaon, roi d'Égypte, avec ses serviteurs, ses chefs, et tout son peuple;
20 pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
tout le peuple mélangé, tous les rois du pays d'Uz, tous les rois des Philistins, Askalon, Gaza, Ékron, et le reste d'Asdod;
21 Edomu, Moabu na Amoni;
Édom, Moab, et les enfants d'Ammon;
22 wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
tous les rois de Tyr, tous les rois de Sidon, et les rois de l'île qui est au delà de la mer;
23 Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
Dedan, Tema, Buz, et tous ceux qui ont les coins de leur barbe coupés;
24 wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
tous les rois d'Arabie, tous les rois du peuple mélangé qui habite dans le désert;
25 wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
tous les rois de Zimri, tous les rois d'Élam, tous les rois des Mèdes,
26 na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
tous les rois du nord, les uns avec les autres, de loin et de près, et tous les royaumes du monde, qui sont à la surface de la terre. Le roi de Sheshach boira après eux.
27 “Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
Tu leur diras: « L'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Buvez et soyez ivres, vomissez, tombez et ne vous relevez plus, à cause de l'épée que j'enverrai au milieu de vous ».
28 Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
S'ils refusent de prendre la coupe dans ta main pour boire, tu leur diras: « L'Éternel des armées dit: « Vous boirez ».
29 Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
Car voici que je commence à faire du mal à la ville qui s'appelle de mon nom. Vous ne resterez pas impunis, car j'appellerai l'épée sur tous les habitants de la terre, dit Yahvé des armées ».
30 “Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
« Prophétise donc contre eux toutes ces paroles, et dis-leur, "'Yahvé rugira du haut des cieux, et faire entendre sa voix depuis sa demeure sainte. Il rugira puissamment contre son pli. Il poussera un cri, comme ceux qui foulent le raisin, contre tous les habitants de la terre.
31 Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
Un bruit se fera entendre jusqu'à l'extrémité de la terre; car Yahvé a une controverse avec les nations. Il entrera en jugement avec toute chair. Quant aux méchants, il les livrera à l'épée, dit Yahvé. »
32 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
Yahvé des Armées dit, « Voici que le mal se répandra de nation en nation, et une grande tempête s'élèvera des extrémités de la terre. »
33 Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
En ce jour-là, les morts de Yahvé seront d'un bout à l'autre de la terre. On ne les pleurera pas. Ils ne seront ni recueillis ni enterrés. Ils seront du fumier à la surface de la terre.
34 Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
Gémissez, bergers, et criez. Va te vautrer dans la poussière, toi le chef du troupeau; car les jours de vos massacres et de vos dispersions sont arrivés, et vous tomberez comme une fine poterie.
35 Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
Les bergers n'auront aucun moyen de fuir. Le chef du troupeau n'aura pas d'échappatoire.
36 Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
Une voix du cri des bergers, et les lamentations du chef du troupeau, car Yahvé détruit leurs pâturages.
37 Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
Les plis paisibles sont réduits au silence à cause de l'ardente colère de Yahvé.
38 Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.
Il a quitté sa cachette, comme le lion; car leur pays est devenu un objet d'étonnement à cause de la férocité de l'oppression, et à cause de sa colère féroce.

< Yeremia 25 >