< Yeremia 24 >

1 Baada ya Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana.
L'Éternel me fit voir que deux corbeilles de figues étaient placées devant le temple de l'Éternel, après que Nebucadnetsar, roi de Babylone, eut emmené captifs de Jérusalem Jeconia, fils de Jojakim, roi de Juda, et les princes de Juda, avec les artisans et les forgerons, et les eut emmenés à Babylone.
2 Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.
L'un des paniers contenait de très bonnes figues, comme les figues de première maturité, et l'autre panier contenait de très mauvaises figues, qui ne pouvaient pas être mangées tant elles étaient mauvaises.
3 Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?” Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”
Alors Yahvé me demanda: « Que vois-tu, Jérémie? » J'ai dit: « Des figues. Les bonnes figues sont très bonnes, et les mauvaises sont très mauvaises, si mauvaises qu'on ne peut pas les manger. »
4 Kisha neno la Bwana likanijia:
La parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
5 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.
L'Éternel, le Dieu d'Israël, dit: « Comme ces bonnes figues, je considère comme bons les captifs de Juda que j'ai envoyés de ce lieu au pays des Chaldéens.
6 Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa,
Car je les regarderai comme un bien, et je les ramènerai dans ce pays. Je les bâtirai, et je ne les abattrai pas. Je les planterai, et je ne les arracherai pas.
7 nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
Je leur donnerai le cœur de me connaître, de savoir que je suis Yahvé. Ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu, car ils reviendront à moi de tout leur cœur.
8 “‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri.
"'Comme les figues mauvaises qui ne se mangent pas, tant elles sont mauvaises, dit Yahvé, je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses princes, et le reste de Jérusalem qui demeure dans ce pays, et ceux qui habitent au pays d'Égypte.
9 Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia.
Je les livrerai même pour qu'ils soient ballottés parmi tous les royaumes de la terre, pour qu'ils soient un opprobre et un proverbe, une raillerie et une malédiction, dans tous les lieux où je les chasserai.
10 Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’”
J'enverrai parmi eux l'épée, la famine et la peste, jusqu'à ce qu'ils soient exterminés du pays que j'ai donné à eux et à leurs pères.'"

< Yeremia 24 >