< Yeremia 24 >

1 Baada ya Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana.
The Lord schewide to me, and lo! twei panyeris ful of figys weren set bifor the temple of the Lord, aftir that Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, translatide Jeconye, the sone of Joachym, the kyng of Juda, and the princes of hym, and a sutil crafti man, and a goldsmith fro Jerusalem, and brouyte hem in to Babiloyne.
2 Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.
And o panyere hadde ful good figis, as figis of the firste tyme ben wont to be; and o panyere hadde ful yuel figis, that miyten not be etun, for tho weren yuel figis.
3 Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?” Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”
And the Lord seide to me, Jeremye, what thing seest thou? And Y seide, Figis, goode figis, ful goode, and yuele figis, ful yuele, that moun not be etun, for tho ben yuele figis.
4 Kisha neno la Bwana likanijia:
And the word of the Lord was maad to me,
5 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.
and seide, The Lord God of Israel seith these thingis, As these figis ben goode, so Y schal knowe the transmygracioun of Juda, which I sente out fro this place in to the lond of Caldeis, in to good.
6 Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa,
And Y schal sette myn iyen on hem to plese, and Y schal brynge hem ayen in to this lond; and Y schal bilde hem, and Y schal not distrie hem; and Y schal plaunte hem, and Y schal not drawe vp bi the roote.
7 nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
And Y schal yyue to hem an herte, that thei knowe me, for Y am the Lord; and thei schulen be in to a puple to me, and Y schal be in to God to hem, for thei schulen turne ayen to me in al her herte.
8 “‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri.
And as the worste figis ben, that moun not be etun, for tho ben yuele figis, the Lord seith these thingis, So Y schal yyue Sedechie, the kyng of Juda, and the princes of hym, and other men of Jerusalem, that dwelliden in this citee, and that dwellen in the lond of Egipt.
9 Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia.
And Y schal yyue hem into trauelyng and turment in alle rewmes of erthe, in to schenschipe, and in to parable, and in to a prouerbe, and in to cursyng, in alle places to whiche Y castide hem out.
10 Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’”
And Y schal sende in hem a swerd, and hungur, and pestilence, til thei be wastid fro the lond which Y yaf to hem, and to the fadris of hem.

< Yeremia 24 >