< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
Maudits soient les pasteurs qui perdent et dispersent les brebis de leur pâturage!
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur sur les pasteurs de mon peuple: Vous avez dispersé et repoussé mes brebis, et vous ne les avez pas visitées. Et moi je vous punirai de vos méchantes œuvres.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
Moi-même je recueillerai les restes de mon peuple sur toute terre où je les ai bannis, et je les rétablirai en leurs pâturages, et ils croîtront et ils se multiplieront.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
Et je susciterai pour eux des pasteurs qui les mèneront paître, et ils n'auront plus peur, et ils ne trembleront plus, dit le Seigneur.
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
Voilà que les jours arrivent, dit le Seigneur, où je susciterai pour David un soleil de justice, et un roi règnera, et il comprendra, et il rendra justice selon le jugement à toute la terre.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
De son temps, Juda sera sauvé, et Israël s'abritera dans ses demeures en toute assurance. Et le nom que lui donnera le Seigneur sera Josédec, parmi les prophètes.
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
A cause de cela, voilà que les jours approchent, dit le Seigneur, où ils ne diront plus: Vive le Seigneur, qui a tiré la maison d'Israël de la terre d'Égypte!
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
Mais: Vive le Seigneur, qui a rassemblé toute la race d'Israël, et l'a ramenée de la terre du nord et de toutes les contrées où il les avait bannis, et qui les a rétablis dans leur héritage!
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
Parmi les prophètes, je suis celui au cœur brisé; tous mes os ont été ébranlés; je suis devenu comme un homme meurtri ou comme un homme pris de vin, à la vue du Seigneur et de la magnificence de sa gloire.
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
Devant sa face, la terre est en deuil, et les pâturages du désert sont desséchés; et la course de ces hommes est devenue mauvaise, et leur force pareillement.
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
Le prêtre et le prophète se sont souillés; jusque dans mon temple j'ai vu leur corruption.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
A cause de cela, que leur voie soit glissante et sombre, et ils y trébucheront, et ils y tomberont; car j'amènerai sur eux des maux en l'année où je les visiterai.
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
Et les prophètes de Samarie, j'ai vu en eux des iniquités; ils ont prophétisé par Baal, et ils ont égaré mon peuple d'Israël.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
Et les prophètes de Jérusalem, j'ai vu en eux des choses horribles; adultères, cheminant dans le mensonge, prenant de toutes mains pour ne point détourner les méchants de leurs voies, ils ont tous été pour moi comme Sodome, et les habitants de Jérusalem comme Gomorrhe.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
A cause de cela, ainsi dit le Seigneur: Voilà que je vais les nourrir de douleurs, et je les abreuverai d'eau saumâtre, parce que des prophètes de Jérusalem est sortie la souillure de toute la terre.
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
Voici ce que dit le Seigneur tout-puissant: N'écoutez point les discours des prophètes, parce qu'ils ont des visions vaines; ils parlent selon leur cœur, et non selon la bouche de Dieu.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
Ils disent à ceux qui rejettent la parole du Seigneur: La paix sera avec vous; et à ceux qui courent après leurs désirs et après les égarements de leurs cœurs: Il ne vous arrivera rien de mal.
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
Car qui a assisté au conseil du Seigneur? qui a vu sa parole? qui l'a entendue de ses oreilles?
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
Voilà un tremblement de terre venu du Seigneur, et sa colère produit ce tremblement; elle viendra frapper les impies.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
Et la colère du Seigneur ne se détournera plus qu'elle n'ait accompli toutes les résolutions de son cœur; et à la fin des jours ils comprendront.
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
Je n'ai point envoyé ces prophètes, et ils ont couru d'eux-mêmes; je ne leur ai rien dit, et d'eux-mêmes ils ont prophétisé.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
Et s'ils avaient assisté à mon conseil, s'ils avaient entendu mes paroles, je les aurais corrigés, et corrigé mon peuple de ses mauvaises inclinations.
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
Je suis Dieu de près, dit le Seigneur; ne suis-je pas aussi Dieu de loin?
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
Qui se cachera dans le secret, sans que je le découvre? Est-ce que je ne remplis pas le ciel et la terre? dit le Seigneur.
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
J'ai entendu ce que disent les prophètes, ce qu'ils prophétisent en mon nom; ils mentent quand ils disent: J'ai eu un songe.
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
Jusques à quand en sera-t-il ainsi du cœur de ces prophètes, qui prophétisent le mensonge, en prophétisant les séductions de leur cœur?
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
Ils s'imaginent faire oublier ma loi par des songes que chacun se raconte, comme d'autres ont fait oublier mon nom à leurs pères à cause de Baal?
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
Que le prophète qui a eu un songe le raconte; que celui à qui est venue ma parole annonce selon la vérité. Qu'est-ce que la paille auprès du grain? Ainsi en est-il de mes paroles, dit le Seigneur.
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
Mes paroles ne sont-elles pas comme le feu, dit le Seigneur, ou comme la hache qui fend un rocher?
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
Voilà pourquoi je suis contre les prophètes, dit le Seigneur Dieu, qui dérobent mes paroles à leurs frères.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
Voilà pourquoi je suis contre les prophètes qui prophétisent de la langue et disent les rêves de leur sommeil.
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
Voilà pourquoi je suis contre les prophètes qui prophétisent d'après des songes trompeurs et les racontent, et qui ont égaré mon peuple par leurs mensonges et leurs erreurs; et je ne les avais pas envoyés, et je ne leur avais rien prescrit, et ils ne seront d'aucun secours à ce peuple.
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
Et si ce peuple, ou le prêtre, ou le prophète demandent quel est le fardeau du Seigneur, dis-leur: Vous êtes ce fardeau, et je vous briserai, dit le Seigneur.
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
Si le prophète ou quelqu'un des prêtres ou du peuple se sert de ce mot: Le fardeau du Seigneur, je punirai cet homme et sa maison.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
Voici ce que vous direz chacun à votre ami, chacun à votre frère: Qu'a dit le Seigneur? quelle est la parole du Seigneur?
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
Mais ne prononcez plus ce mot: Le fardeau du Seigneur; car c'est votre parole qui sera un fardeau pour lui.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
C'est pourquoi il faut dire: Le Seigneur Dieu nous a-t-il parlé?
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
Voici donc ce que dit le Seigneur notre Dieu: En punition de ce que vous avez prononcé ce mot: Fardeau du Seigneur, après que j'eus envoyé vers vous, et que je vous eus fait dire: Ne dites plus: Le fardeau du Seigneur;
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
A cause de cela, voilà que moi je vous prends et vous brise, vous et cette ville, que j'ai donnée à vous et à vos pères.
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
Et je vous marquerai d'un éternel opprobre, d'une honte éternelle qui ne sera jamais oubliée.

< Yeremia 23 >