< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
Wo to the scheepherdis, that scateren and to-drawen the floc of my lesewe, seith the Lord.
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
Therfor the Lord God of Israel seith these thingis to the scheepherdis, that feeden my puple, Ye han scaterid my floc, and han cast hem out, and han not visitid hem; lo! Y schal visite on you the malice of youre studies, seith the Lord.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
And Y schal gadere togidere the remenauntis of my floc fro alle londis, to whiche Y schal caste hem out thidur; and Y schal turne hem to her feeldis, and thei schulen encreesse, and schulen be multiplied.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
And Y schal reise schepherdis on hem, and thei schulen feede hem; thei schulen no more drede, and schulen not be aferd; and noon schal be souyt of the noumbre seith the Lord.
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
Lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal reise a iust buriownyng to Dauid; and he schal regne a kyng, and he schal be wijs, and he schal make doom and riytfulnesse in erthe.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
In tho daies Juda schal be sauid, and Israel schal dwelle tristili; and this is the name which thei schulen clepe hym, The Lord oure riytful.
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
For this thing lo! daies comen, seith the Lord, and thei schulen no more seie, The Lord lyueth, that ledde the sones of Israel out of the lond of Egipt;
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
but, The Lord lyueth, that ledde out, and brouyte the seed of the hous of Israel fro the lond of the north, and fro alle londis to whiche Y hadde cast hem out thidur; and thei schulen dwelle in her lond.
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
To the prophetis; Myn herte is contrit in the myddis of me, alle my boonys trembliden togidere; Y am maad as a man drunkun, and as a man weet of wyn, of the face of the Lord, and of the face of the hooli wordis of hym;
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
for the lond is fillid with auowteris. For the erthe mourenede of the face of cursyng; the feeldis of desert ben maad drie, the cours of hem is maad yuel, and her strengthe is vnlijk.
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
For whi the profete and the prest ben defoulid; and in myn hous, seith the Lord, Y foond the yuel of hem.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
Therfor the weie of hem schal be as slidur in derknessis, for thei schulen be hurtlid, and schulen falle doun therynne; for Y schal bringe on hem yuels, the yeer of visitacioun of hem, seith the Lord.
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
And in the profetis of Samarie Y siy fonnednesse, and thei profesieden in Baal, and disseyueden my puple Israel.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
And in the profetis of Jerusalem Y siy licnesse, auoutrie, and the weie of leesyng; and thei confortiden the hondis of the worste men, that ech man schulde not conuerte fro his malice; alle thei ben maad as Sodom to me, and alle the dwellers therof `ben maad as Gommorre.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
Therfor the Lord of oostis seith these thingis to the prophetis, Lo! Y schal feed hem with wermod, and Y schal yyue drynke to hem with galle; for whi defoulyng is goen out of the profetis of Jerusalem on al the lond.
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
The Lord of oostis seith these thingis, Nyle ye here the wordis of profetis, that profesien to you, and disseyuen you; thei speken the visioun of her herte, not of the mouth of the Lord.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
Thei seien to hem that blasfemen me, The Lord spak, Pees schal be to you; and thei seiden to ech man that goith in the schrewidnesse of his herte, Yuel schal not come on you.
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
For whi who is present in the councel of the Lord, and siy, and herde his word? who bihelde, and herde the word of hym?
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
Lo! the whirlewynd of the Lordis indignacioun schal go out, and tempest brekynge schal come on the heed of wickid men.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
The strong veniaunce of the Lord schal not turne ayen, til that he do, and til that he fille the thouyt of his herte. In the laste daies ye schulen vndurstonde the councel of hym.
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
Y sente not the profetis, and thei runnen; Y spak not to hem, and thei profesieden.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
If thei hadden stonde in my councel, and hadde maad knowun my wordis to my puple, forsothe Y hadde turned hem awei fro her yuel weie, and fro her worste thouytis.
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
Gessist thou, whether Y am God of niy, seith the Lord, and not God afer?
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
A man schal not be priuy in hid places, and Y schal not se hym, seith the Lord. Whether Y fille not heuene and erthe? seith the Lord.
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
Y herde what thingis the profetis seiden, profesiynge a leesyng in my name, and seiynge, Y dremede dremes.
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
Hou longe is this thing in the herte of profetis, profesiynge a leesyng, and profesiynge the disseite of her herte?
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
Whiche wolen make, that my puple foryete my name for the dremes of hem, which ech man tellith to his neiybore, as the fadris of hem foryaten my name for Baal.
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
A profete that hath a dreme, telle a dreem; and he that hath my word, speke verili my word. What is with chaffis to the wheete? seith the Lord.
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
Whether my wordis ben not as fier brennynge, seith the Lord, and as an hamer al to-brekynge a stoon?
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
Therfor lo! Y am redi to the profetis, seith the Lord, that stelen my wordis, ech man fro his neiybore.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
Lo! Y to the profetis, seith the Lord, that taken her tungis, and seien, The Lord seith.
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
Lo! Y to the profetis, dremynge a leesyng, seith the Lord; which telden tho, and disseyueden my puple in her leesyng, and in her myraclis, whanne Y hadde not sente hem, nether hadde comaundide to hem; whiche profitiden no thing to this puple, seith the Lord.
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
Therfor if this puple, ether profete, ether prest, axith thee, and seith, What is the birthun of the Lord? thou schalt seie to hem, Ye ben the birthun, for Y schal caste you awei, seith the Lord;
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
and a profete, and a prest, and the puple, that seith, The birthun of the Lord, Y schal visite on that man, and on his hous.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
Ye schulen seie these thingis, ech man to his neiybore, and to his brother, What answeride the Lord? and what spak the Lord?
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
For the birthun of the Lord schal no more be remembrid, and the word of ech man schal be birthun to hym; and ye han peruertid the wordis of lyuynge God, of the Lord of oostis, youre God.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
Thou schalt seie these thingis to the profete, What answeride the Lord to thee? and what spak the Lord?
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
Forsothe if ye seien, The birthin of the Lord, for this thing the Lord seith these thingis, For ye seiden this word, The birthun of the Lord, and Y sente to you, and Y seide, Nyle ye seie, The birthun of the Lord; therfor lo!
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
Y schal take you awei, and schal bere, and Y schal forsake you, and the citee which Y yaf to you, and to youre fadris, fro my face.
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
And Y schal yyue you in to euerlastynge schenschipe, and in to euerlastynge sclaundir, that schal neuere be doon awei bi foryetyng.

< Yeremia 23 >