< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
Yahweh declares, “Terrible things will happen to [the leaders] [MET] [of my people—those who are like] shepherds of [the people who are like] my sheep—because they have scattered my people and sent them away, and have not taken care of them.
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
So, this is what [I, ] Yahweh, the God whom the Israeli [people worship], say to those leaders: ‘Instead of taking care of my people and [leading them to places where they are safe, like a shepherd does for] his sheep, you have scattered them. So I will punish you for the evil things that you have done.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
But later I will gather those who are still alive, from the countries where I have forced them to go. I will bring them back to their own country, where they will have many children, and their number/population will increase.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
[Then] I will appoint [other] leaders for my people, leaders who will take care of them. And my people will never be afraid [DOU] of anything again, and none of them will be [like a] lost [sheep].’”
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
Yahweh [also] says, “Some day I will appoint for you a righteous man who will be a descendant of King David. He will be a king who rules wisely. He will do what is just and right throughout the land.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
At that time, all the Israeli people [DOU] will be saved [from their enemies], and they will be safe. And his name will be ‘Yahweh, the one who vindicates/defends us.’”
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Yahweh [also] says that at that time, people [who are solemnly promising to do something] will no longer say, “[I will do it as surely] as Yahweh lives, who rescued the Israeli people from Egypt.”
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
Instead, they will say, “[I will do it] as surely as Yahweh lives, who brought [us] Israeli people back to our own land, from the land to the northeast and from all the [other] countries to which he had exiled us.” And they will live in their own land [again].
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
I am very shocked because of the sacred message that Yahweh has spoken about [what will happen to] the [false] prophets; [it is as though] all my bones shake. I stagger like a man who is drunk after drinking a lot of wine.
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
The land is full of [people who commit] adultery; and [Yahweh] has cursed the land. Even the pastures in the desert are all dried up, because the people do what is evil, and [the false prophets] use their power to do things that are not just/fair.
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
Yahweh says, “[Yes, even] the priests and the prophets are ungodly; they do wicked things even in my temple.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
Therefore, [it will be as though] the paths that they walk on are slippery. [It will be as though] they are being chased in the darkness, and there they will fall down, because I will cause them to experience disasters at the time that I will punish them. [That will surely happen because I], Yahweh, have said it.”
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
[Previously] I saw that the prophets in Samaria were doing something that was wrong; they were prophesying, saying that Baal [gave them the messages that they were proclaiming], and they were deceiving my people.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
And [now] I have seen the prophets in Jerusalem doing terrible things. They commit adultery and habitually tell lies. They encourage evil people to continue to do evil things, with the result that the people do not stop sinning. Those prophets are as wicked as the people in Sodom and Gomorrah were.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
So, this is what the Commander of the armies of angels says about those [false] prophets: “I will give those prophets bitter things to eat and poison to drink, because it is because of them that this land is filled with [people who do] wicked things.”
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
This is what the Commander of the armies of angels says: “Do not pay any attention to what those [false] prophets say to you, because they are just deceiving you. They tell you about visions that they have thought/created [only] in their own minds, not about visions that I have given them.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
They habitually say to those who hate me, ‘[Yahweh says that] you will have peace.’ And they say to those who stubbornly do what they want to do, ‘Nothing bad will happen to you [because of your doing those things].’
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
But none of them has ever been in a council [meeting] in heaven in order to listen to a message from me. None of them has paid attention to anything that [I], Yahweh, have said.
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
So, listen to this: I will punish them; it will be [like] a great storm; it will come down [like] a whirlwind, swirling around the heads of those wicked people.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
I will not stop being angry until I completely accomplish all that I have planned. In the future, you will understand [all of] this clearly.”
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
[Yahweh also says, ] “I have not appointed those prophets, but they run [around telling people their messages]. I did not speak to them, but they [continue to] prophesy.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
If they had been in my council [meetings], they would have been able to speak messages from me, and they would have caused people to turn away from committing evil things.”
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
Yahweh [also] says, “Am I a God who is only nearby? No, I am a God who is far away, also.
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
So, no one can hide in some secret place with the result that I cannot see him. I am everywhere, in heaven and on the earth! [That is what I], Yahweh, say!
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
I have heard those prophets prophesy lies, saying that they are telling people messages from me. They say, ‘[Listen to me tell you] the dream that God gave me last night! I [really] had this dream!’
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
How long will they continue to do this? How long will those lying prophets continue to prophesy things that come only from their own minds?
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
They think that because of the dreams that they tell to each other, people will forget me, like their ancestors forgot about me when they started to worship Baal.
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
Allow those [false] prophets to tell people their dreams, but those who have messages that [really] come from me should proclaim those messages faithfully. I, Yahweh, say [that like] straw and grain are certainly very different, [my messages and the messages from those false prophets are certainly very different].
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
[It is as though] my messages [burn] like a fire; they [strike people’s inner beings like] someone strikes a rock with a hammer and smashes it into pieces.
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
Therefore, [I, ] Yahweh say, 'I oppose all those prophets who steal messages from each other and claim that those messages came from me.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
I oppose those prophets who speak their own messages but claim that those messages came from me.
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
I oppose those prophets who falsely say that I told them something in a vision, but they are [only] telling lies that cause my people to sin. I did not send those prophets. I did not even appoint them [to be prophets]. And they have no messages that will benefit my people at all.' [That is what I, ] Yahweh, declare.”
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
[Yahweh said to me], “If one of those prophets or priests or one of the [other] people asks you, ‘What problem has Yahweh told you about [now]?’, you must reply, ‘You are the problem! And Yahweh says that he will abandon you!’
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
And if any prophet or priest or anyone [else falsely] says, ‘[I have] a prophecy from Yahweh,’ I will punish that person and his family.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
What you should continually ask each other is, ‘[When you spoke to Yahweh, ] what did he reply? What is he saying [to us]?’
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
But stop saying ‘[I have] a prophecy/message from Yahweh,’ because those who say that are doing it only because they want people to accept their ideas, and by doing that they distort/change the messages that are from our God, the Commander of the armies of angels.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
This is what you should ask each prophet: ‘What did Yahweh reply [when you talked to him]? What is he saying [to us]?’
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
If he replies, ‘[What I told you] is a prophecy/message from Yahweh,’ you should say to him, ‘You have continued to say, “[I received] a prophecy/message from Yahweh” even though I told you to not claim that you have received prophecies/messages from Yahweh.’
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
So I [, Yahweh, ] will get rid of you [false prophets]. I will expel you from my presence. And I will get rid of this city that I gave to you and to your ancestors.
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
I will cause people to make fun of you forever. People will never forget that you were disgraced.”

< Yeremia 23 >