< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
Woe unto the shepherds that destroy and scatter the flocks of my pasture! saith the Lord.
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
Therefore thus hath said the Lord the God of Israel concerning the shepherds that feed my people, Ye have scattered my flocks, and driven them away, and have not taken care of them: now, behold, I will visit upon you the evil of your doings, saith the Lord.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
And I will indeed gather the remnant of my flock together out of all the countries whither I have driven them; and I will bring them back again to their folds: and they shall be fruitful and multiply.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
And I will raise up over them shepherds who shall feed them: and they shall fear no more, nor be dismayed, and none of them shall be missing, saith the Lord.
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
Behold, days are coming, saith the Lord, when I will raise up unto David a righteous sprout, and he shall reign as king, and prosper, and he shall execute justice and righteousness on the earth.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
In his days shall Judah be helped, and Israel shall dwell in safety: and this is his name whereby he shall be called, The Lord is our righteousness.
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Therefore, behold, days are coming, saith the Lord, when they shall no more say, As the Lord liveth, who hath brought up the children of Israel out of the land of Egypt;
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
But, As the Lord liveth, who hath brought up and who hath led forth the seed of the house of Israel out of the north country, and out of all countries whither I had driven them: and they shall dwell in their own land.
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
To the prophets—Broken is my heart within me; all my bones shake; I am like a drunken man, and like a person whom wine hath overcome, because of the Lord, and because of his holy words.
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
For of adulterers is the land full; for because of false swearing mourneth the land, dried up are the pastures in the wilderness; because their course was for evil, and their strength was for injustice.
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
For both prophet and priest are hypocrites: yea, in my own house have I found their wickedness, saith the Lord.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
Therefore shall their way be unto them as slippery ways in the darkness; they shall be pushed forward, and fall thereon; for I will bring upon them evil, the year of their punishment, saith the Lord.
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
And on the prophets of Samaria have I seen absurdity: they prophesied by Ba'al, and misled my people Israel.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
But on the prophets of Jerusalem have I seen a horrible thing; they commit adultery, and walk in falsehood; and they strengthen the hands of evil-doers, so that not one of these doth return from his wickedness: they are become unto me all of them as Sodom, and its inhabitants as Gomorrah.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
Therefore thus hath said the Lord of hosts concerning the prophets, Behold, I will feed them with wormwood, and make them drink poison-water; for from the prophets of Jerusalem is hypocrisy gone forth over all the land.
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
Thus hath said the Lord of hosts, Hearken not unto the words of the prophets that prophesy unto you, they bring you unto vanity: a vision of their own heart do they ever speak, not out of the mouth of the Lord.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
They say indeed unto those that incense me, The Lord hath spoken, Peace shall ye have; and unto every one that walketh in the stubbornness of his own heart, they said, There shall come no evil upon you.
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
For who hath stood in the secret counsel of the Lord, that he could perceive and hear his word? who hath listened to his word and heard it?
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
Behold, the storm-wind of the Lord is gone forth in fury, yea, a whirling storm: upon the head of the wicked shall it fall grievously.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
The anger of the Lord will not return, until he have executed, and until he have fulfilled the purposes of his heart: in the end of days shall ye understand this fully.
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
I had not sent these prophets, yet they ran: I had not spoken to them, yet they prophesied.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
But if they had stood in my secret counsel, they should have announced my words to my people, and have caused them to turn back from their evil way, and from the wrongfulness of their doings.
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
Am I a God for those near at hand, saith the Lord, and not a God for those who are afar off?
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
If a man should hide himself in secret places should I not then see him? saith the Lord. Do I not fill the heavens and the earth? saith the Lord.
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
I have heard what the prophets have said, that prophesy falsely in my name, saying, I have dreamt, I have dreamt.
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
How long shall it be in the heart of the prophets that prophesy falsehood? yea, the prophets of the deceit of their own heart, —
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
[How long] do they think to cause my people to forget my name by their dreams which they relate every man to his neighbor, as their fathers forgot my name for the sake of Ba'al?
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
The prophet that hath had a dream, let him relate his dream; and he that hath received my word, let him speak my word of truth. What hath the straw to do with the corn? saith the Lord.
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
Is not thus my word, like the fire? saith the Lord, and like a hammer that shivereth the rock?
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
Therefore, behold, I am against the prophets, saith the Lord, that steal my words every one from his neighbor.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
Behold, I am against the prophets, saith the Lord, that use their own word, and say, [The Lord] saith.
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
Behold, I am against those that prophesy with false dreams, saith the Lord, and do relate them, and mislead my people by their falsehoods, and by their vain boasting: while I have not sent them, nor commanded them; and they cannot bring the least profit to this people, saith the Lord.
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
And if this people, or the prophet, or a priest, should ask thee, saying, What is the message of the Lord? then shalt thou say unto them, Because of this “What is the message?” will I even cast you off, saith the Lord.
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
And as for the prophet, and the priest, and the people, that will say, “A message of the Lord,” I will even inflict punishment on that man and on his house.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
Thus shall ye say every one to his neighbor, and every one to his brother, What hath the Lord answered? and, What hath the Lord spoken?
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
But “A message of the Lord” shall ye not mention any more; for the message cometh indeed to the man of his [prophetic] word; but ye pervert the words of the living God, of the Lord of hosts our God.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
Thus shalt thou say to the prophet, What hath the Lord answered thee? and, What hath the Lord spoken?
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
But if ye will say, “A message of the Lord,” then thus saith the Lord, Because ye say this word, “A message of the Lord,” and I have sent unto you, saying, Ye shall not say, “A message of the Lord:”
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
Therefore, behold, I am here, and I will tear you completely away, and I will cast you off, and the city that I have given to you and to your fathers, out of my presence;
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
And I will lay upon you an everlasting disgrace, and a perpetual shame, which shall not be forgotten.

< Yeremia 23 >