< Yeremia 22 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Shuka kwenye jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, utangaze ujumbe huu huko:
Pakaiyin hitin aseiye, “Nangma Judah lengpa in-ah chesuh inlang, hiche thuhi gaseipeh tan,’’
2 ‘Sikia neno la Bwana, ee mfalme wa Yuda, wewe uketiye kwenye kiti cha enzi cha Daudi: wewe, maafisa wako na watu wako mnaopitia malango haya.
Juda lengpa, David laltouna toupa, ngaiyin, chule namite leh nasohten jong ngaicheh’uhen.
3 Hili ndilo Bwana asemalo: Tenda haki na adili. Mwokoe mkononi mwa mdhalimu yeye aliyetekwa nyara. Usimtendee mabaya wala ukatili mgeni, yatima au mjane, wala usimwage damu isiyo na hatia mahali hapa.
Pakaiyin hitin aseiye, Thu adih in tanpih uvin chule thil adih in bol uvin. Athil kichompih ho chu panhu’uvin lang, amaho chu akibol ganthei nauva kon in huhdoh uvin. Chule nagitlounau chu dalhauvin. Gamchom mileh kholjin miho bolse hih un, chule chagate leh meithai ho chu pumhat in boldauvin. Chule themmona bei mite chunga thisan sodauvin.
4 Kwa kuwa ukiwa mwangalifu kushika maagizo haya, ndipo wafalme watakaokalia kiti cha enzi cha Daudi watakapoingia kupitia malango ya jumba hili la kifalme, wakiwa wamepanda magari na farasi, huku wakifuatana na maafisa wao na watu wao.
Nanghon kathu nangaiyuleh, hiche mun’a hi, David laltouna-a, David son le pah ho toujing ding ahi. Chutia chu, lengho leh alhachac ho chule asohte, kangtalai leh sakol a tou uva, leng inpi kelkot a chu, lutle potle abol diu ahi.
5 Lakini kama hutayatii maagizo haya, asema Bwana, ninaapa kwa nafsi yangu kwamba jumba hili litakuwa gofu.’”
Amavang, nanghon kathusei hi donlouva nakoi vang ule, keima tah kamin’a kakitepna kasem ahi; Hiche mun hi ahomkeo leh keohel’a kalha ding ahi, tin Pakaiyin aseiye.
6 Kwa kuwa hili ndilo Bwana asemalo kuhusu jumba la kifalme la mfalme wa Yuda: “Ingawa uko kama Gileadi kwangu, kama kilele cha Lebanoni, hakika nitakufanya uwe kama jangwa, kama miji ambayo haijakaliwa na watu.
Pakaiyin, Judah leng inpi thua hitin aseiye, “Keiding in nangma hi, Gilead lhang leh Lebanon gam hoitah banga chule mihem chennalou gam kasosah ding nahi.
7 Nitawatuma waharabu dhidi yako, kila mtu akiwa na silaha zake, nao watazikata boriti zako nzuri za mierezi na kuzitupa motoni.
Keiman nangma sumang ding mi kakou ding, amahon ama cheh manchah ahin kichoi uva, nasuh gamdiu ahi. Amahon, Cedar thing hoilai ho aphuh uva, meiya ahalvam diu ahi.
8 “Watu kutoka mataifa mengi watapitia karibu na mji huu na kuulizana, ‘Kwa nini Bwana amefanya jambo la namna hii juu ya mji huu mkubwa?’
Gam chom chom’a kon hung kholjin namtin vaipin, hiche khopi hinjotpa jousen, ‘Ibol’a Pakaiyin hiche khopi lentah hi ahiti suhmang jeng hitam? tia amaho leh amaho kihoudiu ahi.
9 Nalo jibu litakuwa: ‘Kwa sababu wameliacha agano la Bwana, Mungu wao, na wameabudu na kuitumikia miungu mingine.’”
Chutengle, “Amahon Pakai a Pathen’u toh akitepnau asuhkeh jeh uva, kisumang ahiuve,’ ti ahetdoh diu ahi.
10 Usimlilie yeye aliyekufa, wala usimwombolezee; badala yake, afadhali umlilie kwa uchungu yule aliyepelekwa uhamishoni, kwa sababu kamwe hatairudia wala kuiona tena nchi yake alikozaliwa.
Lengpa din kadauvin, lunghempi dauvin, ama chu athi ahitai. Amavang, sohchanga kikaimangpa chu kapiuvin lang, apul douvun. Ajeh chu, aman agamsung ahung mukit louhel ding ahitai.
11 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Shalumu mwana wa Yosia, aliyeingia mahali pa baba yake kuwa mfalme wa Yuda, lakini ameondoka mahali hapa: “Yeye kamwe hatarudi tena.
Hiche thuhi, apa Josiah khel’a lengchang Jehoahaz chungthu asei ahi. ama chu gal-hinga kikaimang ahin, agam a hung kilekit louding ahi.
12 Atafia huko mahali walipompeleka kuwa mateka; hataiona tena nchi hii.”
Ama chu migam’a thiden ding, agamsung anungmu louhel ding ahi.
13 “Ole wake yeye ajengaye jumba lake la kifalme kwa njia ya dhuluma, vyumba vyake vya juu kwa udhalimu, akiwatumikisha watu wa nchi yake pasipo malipo, bila kuwalipa kwa utumishi wao.
Pakaiyin hitin aseiye, ‘Ohe ada ahi, lamdih lou tah’a in kisahpa! Thudih louva inpi kehlen’a, aheng akom tohman pelouva goipa, chule pumhat a kulpi kisempa!
14 Asema, ‘Nitajijengea jumba kuu la kifalme, na vyumba vya juu vyenye nafasi kubwa.’ Hivyo anaweka ndani yake madirisha makubwa, huweka kuta za mbao za mierezi, na kuipamba kwa rangi nyekundu.
Hichepa hin, ‘Keiman inlentah khat kisah inge, indan tampi sem ing katin chule bangkot tampi Cedar thing in sem inge. Hichu rong sen in hoitah in loi ing kate,’’ ati.
15 “Je, inakufanya kuwa mfalme huko kuongeza idadi ya mierezi? Je, baba yako hakuwa na chakula na kinywaji? Alifanya yaliyo sawa na haki, hivyo yeye akafanikiwa katika yote.
amavang, Cedar thinga leng inpi nomtah leh loupitah kisahdoh jeh’a, leng vaipoa kipang ahipoi. Napa Josiah chu neh le don aning lhing set in; ama chu thudihtah ahin, ijakai adih in abol’e. Hijeh chun, Pathen phattheiboh achange.
16 Aliwatetea maskini na wahitaji, hivyo yeye akafanikiwa katika yote. Je, hiyo si ndiyo maana ya kunijua mimi?” asema Bwana.
Aman vaicha gentheite apanpin, dihtah in vai ahom e. chule ama din imajouse aphatouvin akhangtouve. Hiche hi hilouham, keima toh kivopjing, kitichu,’’ tin Pakaiyin aseiye.
17 “Lakini macho yako na moyo wako vimeelekezwa tu katika mapato ya udhalimu, kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa uonevu na ukatili.”
Nang invang, namit teni leh nalungthim hi, nangma changseh ding le alamlouva phatchomna muna ding bouvin naming in; monabei nathat in, vaicha gentheite nabol gentheijin, chule hepina umlouvin vai nahom e.
18 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda: “Hawatamwombolezea wakisema: ‘Ole, ndugu yangu! Ole, umbu langu!’ Hawatamwombolezea wakisema: ‘Ole, bwana wangu! Ole, fahari yake!’
Hijeh chun, Josaih chapa Jehoiakim chung thuhi, Pakaiyin hitin aseiye. “Amapa hi, mihon athini le along a-oplou diu, vo sopipa vo golpa tiajong koima kaplou ding ahi. Amite jeng injong, vo Lengpa, kapu tia akapi umlou ding ahiuve.
19 Atazikwa maziko ya punda: ataburutwa na kutupwa nje ya malango ya Yerusalemu.”
Athi long chu, sangan thisa kivui banga, Jerusalem khopia kon’a kikaidoh’a, kelkot polam’a gakivui ding ahi.
20 “Panda Lebanoni ukapige kelele, sauti yako na isikike huko Bashani, piga kelele toka Abarimu, kwa kuwa wote waliojiunga nawe wameangamizwa.
Lebanon’a naloi ho din kapin, chule amaho ding chu Bashan mun’a othong leuvin gasamin. Ab’arim mun’a amaho chu gaholtan, chule amaho din kapin, amaho chu abon'un akisugamtauve.
21 Nilikuonya wakati ulipojisikia kwamba uko salama, lakini ulisema, ‘Mimi sitasikiliza!’ Hii imekuwa kawaida yako tangu ujana wako; hujanitii mimi.
Nangma nakhantoupet in kana hil in, Ahinlah, nangman ngaiseh in naneipoi. Hitia hi, naneolaiya pat a kathusei ngailouva hung umpeh chu nahi.
22 Upepo utawaondoa wachungaji wako wote, na wale ulioungana nao wataenda uhamishoni. Kisha utaaibika na kufedheheka kwa sababu ya uovu wako wote.
Tua hi, khopi huiyin napankhompi jouse asumang ding chule naloi nagol ho abon’a sohchanga kikaimang ding ahiuve. Chutahle nagitlouna ho jal’a, nangma najah chading chule nakisuh lungdong ding ahi.
23 Wewe uishiye Lebanoni, wewe uliyetulia kwenye majengo ya mierezi, tazama jinsi utakavyoomboleza maumivu makali yatakapokupata, maumivu kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa!
Lebanon gam Cedar thinga kisa leng inpi hoitah sung’a busah chu anom e. Hijongle, numei naosonat tobanga nathoh gimmna ding hesoh gentheina nachunga hung lhung ding ahi.
24 “Hakika kama niishivyo,” asema Bwana, “hata kama wewe, Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ungekuwa pete yangu ya muhuri katika mkono wangu wa kuume, bado ningekungʼoa hapo.
Pakaiyin aseiye, ‘Keima kahing jinge. Juda lengpa Jehoiakim chapa Jehoiachin, keiman nagma kadalhah ding nahi. Keidinga nangma hi kajitlam’a kibut khutjem nahivangin, kasutlhah ding nahi.
25 Nitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako, wale unaowaogopa, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na kwa Wakaldayo.
Nanghi, thadinga nahol namelmate khut’a, chule nakichat mama jeng Nebuchadnezzar leh asepaite khut’a kapehdoh nahitai.
26 Nitakutupa mbali wewe na mama aliyekuzaa mwende katika nchi nyingine, ambayo hakuna hata mmoja wenu aliyezaliwa huko, nanyi mtafia huko.
Nang le nanu jong hiche gamsung’a kon’a kanodoh ding, chule nangma hiche gamsunga nathi lou ding, migam danga nathiden ding ahi.
27 Kamwe hamtarudi katika nchi mliyotamani kuirudia.”
Chule nagam’a nahung kilekit tah louding ahi.
28 Je, huyu mtu Yekonia ni chungu kilichodharauliwa, chungu kilichovunjika, chombo kisichotakiwa na mtu yeyote? Kwa nini yeye na watoto wake watupwe nje kwa nguvu, na kutupwa kwenye nchi wasioijua?
Ibol’a Jehoiachin kitipa hi, belkehsa panna neilou banga um hitam? Ibol’a ama leh achate jouse mi gamdanga soh’a kinomang u hitam?
29 Ee nchi, nchi, nchi, sikia neno la Bwana!
Vo leiset, vo gam leiset, Pakai thusei hi ngaiyun!
30 Hili ndilo Bwana asemalo: “Mwandike huyu mtu kama asiye na mtoto, mtu ambaye hatafanikiwa maisha yake yote, kwa maana hakuna mtoto wake atakayefanikiwa, wala kukaa kwenye kiti cha enzi cha Daudi wala kuendelea kutawala katika Yuda.”
Pakaiyin hitin aseiye, Jehoiachin kitipa hi, son leh pah neilou, ahinkho sunga ima boldohlou mipa ahi, tin sunlut un. Ajeh chu achate atute khatcha beh jong, David laltouna touva, Judah gamsung a vaihom ding umlou ding ahi.

< Yeremia 22 >