< Yeremia 21 >

1 Neno lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana wakati Mfalme Sedekia alipowatuma Pashuri mwana wa Malkiya, na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwake, kusema:
Parole qui fut adressée à Jérémie par le Seigneur, quand le roi Sédécias envoya vers lui Phassur, fils de Melchias, et Sophonias, le prêtre, fils de Maasias, disant:
2 “Tuulizie sasa kwa Bwana, kwa sababu Nebukadneza mfalme wa Babeli anatushambulia. Labda Bwana atatenda maajabu kwa ajili yetu kama nyakati zilizopita, ili Nebukadneza atuondokee.”
Consulte pour nous le Seigneur, parce que Nabuchodonosor, roi de Babylone, combat contre nous; pour savoir si le Seigneur agira avec nous selon toutes ses merveilles, et si l’ennemi s’éloignera de nous.
3 Lakini Yeremia akawajibu, “Mwambieni Sedekia,
Et Jérémie leur dit: Ainsi vous direz à Sédécias:
4 ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kuwageuzia silaha za vita zilizo mikononi mwenu, ambazo mnatumia kupigana na mfalme wa Babeli na Wakaldayo ambao wako nje ya ukuta wakiwazunguka kwa jeshi. Nami nitawakusanya ndani ya mji huu.
Voici ce que dit le Seigneur, Dieu d’Israël: Voilà que moi, j’enlèverai les instruments de guerre qui sont en vos mains, et avec lesquels vous combattez contre le roi de Babylone et contre les Chaldéens, qui vous assiègent autour des murs, et je les rassemblerai au milieu de cette cité.
5 Mimi mwenyewe nitapigana dhidi yenu kwa mkono wangu ulionyooshwa na mkono wa nguvu, kwa hasira na ghadhabu kali na ukali mwingi.
Et je combattrai moi-même contre vous avec une main étendue, et avec un bras fort, et avec fureur, et avec indignation, et avec une grande colère.
6 Nitawaangamiza waishio katika mji huu, watu na wanyama, nao watauawa kwa tauni ya kutisha.
Et je frapperai les habitants de cette cité: les hommes et les bêtes mourront d’une grande peste.
7 Baada ya hayo, nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na watu wa mji huu ambao walinusurika tauni, upanga na njaa, mkononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, na kwa adui zao wale wanaotafuta uhai wao. Atawaua kwa upanga; hatakuwa na rehema juu yao au huruma wala kuwasikitikia,’ asema Bwana.
Et après cela, dit le Seigneur, je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses serviteurs et son peuple, et ceux qui auront été épargnés dans cette cité par la peste, et par le glaive, et par la famine, à la main de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et à la main de leurs ennemis, et à la main de ceux qui cherchent leur âme; et il les frappera du tranchant du glaive, et on ne le fléchira pas, et il n’épargnera pas, et il n’aura pas de pitié.
8 “Zaidi ya hayo, waambie watu hawa, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama, naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.
Et à ce peuple tu diras: Voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je mets devant vous la voie de la vie et la voie de la mort.
9 Yeyote atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni. Lakini yeyote atakayetoka na kujisalimisha kwa Wakaldayo ambao wameuzunguka mji huu kwa jeshi, atanusurika, naye ataishi.
Celui qui habitera dans cette ville mourra par le glaive, et par la famine, et par la peste; mais celui qui sortira et qui fuira chez les Chaldéens qui vous assiègent, vivra, et son âme sera pour lui comme une dépouille qu’il aura sauvée.
10 Nimekusudia kuufanyia mji huu jambo baya, wala si jema. Utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto, asema Bwana.’
Car j’ai posé ma face vers cette cité pour son mal, et non pour son bien, dit le Seigneur; elle sera livrée à la main du roi de Babylone, et il la brûlera entièrement par le feu.
11 “Zaidi ya hayo, ambia nyumba ya mfalme ya Yuda, ‘Sikia neno la Bwana,
Et tu diras à la maison du roi de Juda: Ecoutez la parole du Seigneur;
12 Ewe nyumba ya Daudi, hili ndilo Bwana asemalo: “‘Hukumuni kwa haki kila asubuhi, mwokoeni mikononi mwa mdhalimu yeye aliyetekwa nyara, la sivyo ghadhabu yangu italipuka na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mlioufanya: itawaka na hakuna wa kuizima.
Maison de David, voici ce que dit le Seigneur: Rendez dès le matin la justice, et arrachez celui qui est opprimé par la violence de la main de l’oppresseur, de peur que ne sorte comme un feu mon indignation, et qu’elle ne s’enflamme, et qu’il n’y ait personne qui l’éteigne, à cause de la malice de vos œuvres.
13 Niko kinyume nawe, ee Yerusalemu, wewe uishiye juu ya bonde hili kwenye uwanda wa juu wa miamba, asema Bwana, wewe usemaye, “Ni nani awezaye kuja kinyume chetu? Nani ataingia mahali pa kimbilio letu?”
Voilà que moi je viens à toi, habitante de la vallée solide et de la plaine, dit le Seigneur; à vous qui dites: Qui nous frappera? et qui entrera dans nos maisons?
14 Nitawaadhibu kama istahilivyo matendo yenu, asema Bwana. Nitawasha moto katika misitu yenu ambao utateketeza kila kitu kinachowazunguka.’”
Et je vous visiterai, dit le Seigneur, selon le fruit de vos œuvres; et j’allumerai un feu dans sa forêt, et il dévorera toutes choses autour d’elle.

< Yeremia 21 >