< Yeremia 20 >

1 Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya,
RAB'bin Tapınağı'nın baş görevlisi İmmer oğlu Kâhin Paşhur, Yeremya'nın böyle peygamberlik ettiğini duyunca,
2 akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana.
onun dövülüp RAB'bin Tapınağı'nın Yukarı Benyamin Kapısı'ndaki tomruğa vurulmasını buyurdu.
3 Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.
Ertesi gün Paşhur kendisini tomruktan salıverince, Yeremya ona, “RAB sana Paşhur değil, Magor-Missaviv adını verdi” dedi,
4 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga.
“RAB diyor ki, ‘Seni de dostlarını da yıldıracağım. Dostlarının düşman kılıcıyla düştüğünü gözlerinle göreceksin. Bütün Yahuda'yı Babil Kralı'nın eline teslim edeceğim; onları Babil'e sürecek ya da kılıçtan geçirecek.
5 Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli.
Bu kentin bütün zenginliğini –ürününü, değerli eşyalarını, Yahuda krallarının hazinelerini– düşmanlarının eline vereceğim. Hepsini yağmalayıp Babil'e götürecekler.
6 Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’”
Sana gelince, ey Paşhur, sen de evinde yaşayanların hepsi de Babil'e sürüleceksiniz. Sen de kendilerine yalan peygamberlik ettiğin bütün dostların da orada ölüp gömüleceksiniz.’”
7 Ee Bwana, umenidanganya, nami nikadanganyika; wewe una nguvu kuniliko, nawe umenishinda. Ninadharauliwa mchana kutwa, kila mmoja ananidhihaki.
Beni kandırdın, ya RAB, Ben de kandım. Bana üstün geldin, beni yendin. Bütün gün alay konusu oluyorum, Herkes benimle eğleniyor.
8 Kila ninenapo, ninapiga kelele nikitangaza ukatili na uharibifu. Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano na mashutumu mchana kutwa.
Çünkü konuştukça feryat ediyor, Şiddet diye, yıkım diye haykırıyorum. RAB'bin sözü yüzünden bütün gün yeriliyor, Gülünç duruma düşüyorum.
9 Lakini kama nikisema, “Sitamtaja wala kusema tena kwa jina lake,” neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto, moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu. Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu; kweli, siwezi kujizuia.
“Bir daha onu anmayacak, O'nun adına konuşmayacağım” desem, Sözü kemiklerimin içine hapsedilmiş, Yüreğimde yanan bir ateş sanki. Onu içimde tutmaktan yoruldum, Yapamıyorum artık.
10 Ninasikia minongʼono mingi, “Hofu iko pande zote! Mshtakini! Twendeni tumshtaki!” Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze, wakisema, “Labda atadanganyika; kisha tutamshinda na kulipiza kisasi juu yake.”
Birçoğunun, “Her yer dehşet içinde! Suçlayın! Suçlayalım onu!” diye fısıldaştığını duydum. Bütün güvendiğim insanlar düşmemi gözlüyor, “Belki kanar, onu yeneriz, Sonra da öcümüzü alırız” diyorlar.
11 Lakini Bwana yu pamoja nami kama shujaa mwenye nguvu; hivyo washtaki wangu watajikwaa na kamwe hawatashinda. Watashindwa, nao wataaibika kabisa; kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.
Ama RAB güçlü bir savaşçı gibi benimledir. Bu yüzden bana eziyet edenler tökezleyecek, Üstün gelemeyecek, Başarısızlığa uğrayıp büyük utanca düşecekler; Onursuzlukları sonsuza dek unutulmayacak.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe umjaribuye mwenye haki na kupima moyo na nia, hebu nione ukilipiza kisasi juu yao, kwa maana kwako nimeliweka shauri langu.
Ey doğru kişiyi sınayan, Yüreği ve düşünceyi gören Her Şeye Egemen RAB! Davamı senin eline bırakıyorum. Onlardan alacağın öcü göreyim!
13 Mwimbieni Bwana! Mpeni Bwana sifa! Yeye huokoa uhai wa mhitaji kutoka mikononi mwa waovu.
Ezgiler okuyun RAB'be! Övün RAB'bi! Çünkü yoksulun canını kötülerin elinden O kurtardı.
14 Ilaaniwe siku niliyozaliwa! Nayo isibarikiwe ile siku mama yangu aliyonizaa!
Lanet olsun doğduğum güne! Kutlu olmasın annemin beni doğurduğu gün!
15 Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, yule aliyemfanya afurahi sana, akisema, “Mtoto amezaliwa kwako, tena mtoto wa kiume!”
“Bir oğlun oldu!” diyerek babama haber getiren, Onu sevince boğan adama lanet olsun!
16 Mtu huyo na awe kama miji ile ambayo Bwana Mungu aliiangamiza bila huruma. Yeye na asikie maombolezo asubuhi na kilio cha vita adhuhuri.
RAB'bin acımadan yerle bir ettiği Kentler gibi olsun o adam! Sabah feryatlar, Öğlen savaş naraları duysun!
17 Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni, hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, nalo tumbo lake la uzazi lingebaki kuwa kubwa daima.
Çünkü beni annemin rahminde öldürmedi; Annem mezarım olur, Rahmi hep gebe kalırdı.
18 Kwa nini basi nilitoka tumboni ili kuona taabu na huzuni, na kuzimaliza siku zangu katika aibu?
Neden ana rahminden çıktım? Dert, üzüntü görmek, Ömrümü utanç içinde geçirmek için mi?

< Yeremia 20 >