< Yeremia 20 >
1 Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya,
But when Pashchur the son of Immer the priest, who was chief superintendent in the house of the Lord, heard Jeremiah prophesying these words:
2 akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana.
Then smote Pashchur Jeremiah the prophet, and put him in the stocks that were in the upper gate of Benjamin, which was in the house of the Lord.
3 Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.
And it came to pass on the morrow, that Pashchur brought forth Jeremiah out of the stocks. And Jeremiah said unto him, Not Pashchur [Fulness of Freedom] hath the Lord called thy name, but Magor-missabib [[Terror all around]].
4 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga.
For thus hath said the Lord, Behold, I will make thee a terror to thyself, and to all thy friends; and they shall fall by the sword of their enemies, and thy eyes shall see it; and all Judah will I give into the hand of the king of Babylon, and he shall lead them into exile to Babylon, and shall smite them with the sword.
5 Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli.
And I will give up all the wealth of this city, and all its acquisitions, and all its precious things; and all the treasures of the kings of Judah will I give into the hand of their enemies, who shall plunder them, and take them and carry them away to Babylon.
6 Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’”
And thou, Pashchur, and all the inhabitants of thy house, shall go into captivity; and to Babylon shalt thou come, and there thou shalt die, and there shalt thou be buried, thou, and all thy friends, to whom thou hast prophesied with falsehood.
7 Ee Bwana, umenidanganya, nami nikadanganyika; wewe una nguvu kuniliko, nawe umenishinda. Ninadharauliwa mchana kutwa, kila mmoja ananidhihaki.
Thou didst persuade me, O Lord, and I was persuaded; thou laidst thy [hand] strongly on me, and didst prevail: I am laughed at all the time, every one mocketh me.
8 Kila ninenapo, ninapiga kelele nikitangaza ukatili na uharibifu. Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano na mashutumu mchana kutwa.
For as often as I speak must I cry out, violence and wasting must I proclaim; because the word of the Lord is become unto me a disgrace, and a derision, all the time.
9 Lakini kama nikisema, “Sitamtaja wala kusema tena kwa jina lake,” neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto, moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu. Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu; kweli, siwezi kujizuia.
And I thought, I will not make mention of him, and I will not speak any more in his name. But it became in my heart as a burning fire enclosed within my bones, and I was weary with enduring, and I could not overcome it.
10 Ninasikia minongʼono mingi, “Hofu iko pande zote! Mshtakini! Twendeni tumshtaki!” Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze, wakisema, “Labda atadanganyika; kisha tutamshinda na kulipiza kisasi juu yake.”
For I heard the defaming of many, angry assemblies on every side, “Tell, and we will tell of him.” All the men who ought to seek my welfare, watch for my fall; saying, “Peradventure he may he enticed, and we shall prevail against him, and we will then take our revenge on him.”
11 Lakini Bwana yu pamoja nami kama shujaa mwenye nguvu; hivyo washtaki wangu watajikwaa na kamwe hawatashinda. Watashindwa, nao wataaibika kabisa; kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.
But the Lord is with me as a mighty powerful one; therefore my persecutors will stumble, and they will not prevail: they will be greatly ashamed, for they will not prosper; [it is] an everlasting confusion which will never be forgotten.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe umjaribuye mwenye haki na kupima moyo na nia, hebu nione ukilipiza kisasi juu yao, kwa maana kwako nimeliweka shauri langu.
But, O Lord of hosts, that probest the righteous, seest the reins and the heart, let me see thy vengeance on them; for unto thee have I laid open my cause.
13 Mwimbieni Bwana! Mpeni Bwana sifa! Yeye huokoa uhai wa mhitaji kutoka mikononi mwa waovu.
Sing unto the Lord, praise ye the Lord; for he hath delivered the soul of the needy from the hand of evil-doers.
14 Ilaaniwe siku niliyozaliwa! Nayo isibarikiwe ile siku mama yangu aliyonizaa!
Cursed be the day whereon I was born: the day on which my mother bore me shall not be blessed.
15 Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, yule aliyemfanya afurahi sana, akisema, “Mtoto amezaliwa kwako, tena mtoto wa kiume!”
Cursed be the man who brought tidings to my father, saying, A man-child is born unto thee. How very glad did he make him!
16 Mtu huyo na awe kama miji ile ambayo Bwana Mungu aliiangamiza bila huruma. Yeye na asikie maombolezo asubuhi na kilio cha vita adhuhuri.
And may that same man become like the cities which the Lord overthrew, and bethought himself not; and may he hear a cry of anguish in the morning, and a tumultuous noise at noontide;
17 Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni, hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, nalo tumbo lake la uzazi lingebaki kuwa kubwa daima.
Because I was not slain [as I escaped] from the womb; or that my mother might have become unto me my grave, and her womb have been affected with a perpetual pregnancy.
18 Kwa nini basi nilitoka tumboni ili kuona taabu na huzuni, na kuzimaliza siku zangu katika aibu?
Wherefore was this that I came forth out of the womb to see trouble and sorrow, that my days should pass away in shame?