< Yeremia 20 >

1 Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya,
And Pashhur, the son of Immer, the priest who had been appointed leader in the house of the Lord, heard Jeremiah prophesying these words.
2 akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana.
And Pashhur struck the prophet Jeremiah, and he sent him to the stocks, which were at the upper gate of Benjamin at the house of the Lord.
3 Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.
And when it had become light on the next day, Pashhur led Jeremiah from the stocks. And Jeremiah said to him: “The Lord has not called your name: ‘Pashhur,’ but instead: ‘Fear all around.’”
4 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga.
For thus says the Lord: “Behold, I will give you over to fear, you and all your friends, and they will fall by the sword of their enemies, and your eyes will see it. And I will give all of Judah into the hand of the king of Babylon. And he will lead them away to Babylon, and he will strike them with the sword.
5 Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli.
And I will give away the entire substance of this city, and all its labor, and every precious thing. And I will give all the treasures of the kings of Judah into the hands of their enemies. And they will plunder them, and take them away, and lead them into Babylon.
6 Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’”
But you, Pashhur, and all the inhabitants of your house, will go into captivity. And you will go to Babylon. And there you shall die. And there you shall be buried, you and all your friends, to whom you have prophesied a lie.”
7 Ee Bwana, umenidanganya, nami nikadanganyika; wewe una nguvu kuniliko, nawe umenishinda. Ninadharauliwa mchana kutwa, kila mmoja ananidhihaki.
“You have led me away, O Lord, and I have been led away. You have been stronger than I, and you have prevailed. I have become a derision all day long; everyone mocks me.
8 Kila ninenapo, ninapiga kelele nikitangaza ukatili na uharibifu. Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano na mashutumu mchana kutwa.
For I speak now as I have long spoken: crying out against iniquity and proclaiming devastation. And the word of the Lord has been made into a reproach against me and a derision, all day long.
9 Lakini kama nikisema, “Sitamtaja wala kusema tena kwa jina lake,” neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto, moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu. Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu; kweli, siwezi kujizuia.
Then I said: I will not call him to mind, nor will I speak any longer in his name. And my heart became like a raging fire, enclosed within my bones. And I became weary of continuing to bear it.
10 Ninasikia minongʼono mingi, “Hofu iko pande zote! Mshtakini! Twendeni tumshtaki!” Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze, wakisema, “Labda atadanganyika; kisha tutamshinda na kulipiza kisasi juu yake.”
For I heard the insults of many, and terror all around: ‘Persecute him!’ and, ‘Let us persecute him!’ from all the men who had been at peace with me and who had kept watch by my side. ‘If only there were some way that he might be deceived, and we might prevail against him and obtain vengeance from him!’
11 Lakini Bwana yu pamoja nami kama shujaa mwenye nguvu; hivyo washtaki wangu watajikwaa na kamwe hawatashinda. Watashindwa, nao wataaibika kabisa; kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.
But the Lord is with me, like a strong warrior. For this reason, those who persecute me will fall, and they will be ineffective. They will be greatly confounded. For they have not understood the everlasting disgrace that will never be wiped away.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe umjaribuye mwenye haki na kupima moyo na nia, hebu nione ukilipiza kisasi juu yao, kwa maana kwako nimeliweka shauri langu.
And you, O Lord of hosts, the Tester of the just, who sees the temperament and the heart: I beg you to let me see your vengeance upon them. For I have revealed my case to you.
13 Mwimbieni Bwana! Mpeni Bwana sifa! Yeye huokoa uhai wa mhitaji kutoka mikononi mwa waovu.
Sing to the Lord! Praise the Lord! For he has freed the soul of the poor from the hand of the wicked.
14 Ilaaniwe siku niliyozaliwa! Nayo isibarikiwe ile siku mama yangu aliyonizaa!
Cursed is the day on which I was born! The day on which my mother gave birth to me: let it not be blessed!
15 Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, yule aliyemfanya afurahi sana, akisema, “Mtoto amezaliwa kwako, tena mtoto wa kiume!”
Cursed is the man who announced it to my father, saying, ‘A male child has been born to you,’ causing him to rejoice with gladness.
16 Mtu huyo na awe kama miji ile ambayo Bwana Mungu aliiangamiza bila huruma. Yeye na asikie maombolezo asubuhi na kilio cha vita adhuhuri.
Let that man be like the cities that the Lord has overthrown without regret. Let him hear an outcry in the morning, and wailing at the time of midday!
17 Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni, hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, nalo tumbo lake la uzazi lingebaki kuwa kubwa daima.
So let him be, who did not put me to death from the womb, so that my mother would have been my sepulcher, and her womb would have been my eternal resting place!
18 Kwa nini basi nilitoka tumboni ili kuona taabu na huzuni, na kuzimaliza siku zangu katika aibu?
Why did I depart from the womb, so that I would see hardship and sorrow, and so that my days would be consumed by trouble?”

< Yeremia 20 >