< Yeremia 2 >
1 Neno la Bwana lilinijia kusema,
A palavra de Javé veio até mim, dizendo:
2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu.
“Vá e proclame aos ouvidos de Jerusalém, dizendo: 'Javé diz, “Lembro para você a gentileza de sua juventude, seu amor como uma noiva, como você foi atrás de mim no deserto, em uma terra que não foi semeada.
3 Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana, kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia, nayo maafa yaliwakumba,’” asema Bwana.
Israel era santidade para Yahweh, os primeiros frutos de seu aumento. Todos os que o devorarem serão considerados culpados. O mal virá sobre eles”, diz Yahweh”.
4 Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.
Ouça a palavra de Javé, ó casa de Jacó, e de todas as famílias da casa de Israel!
5 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu, hata wakatangatanga mbali nami hivyo? Walifuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai.
diz Yahweh, “Que iniquidade seus pais encontraram em mim”, que eles foram longe de mim, e caminharam depois de uma vaidade sem valor, e se tornaram inúteis?
6 Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana, aliyetupandisha kutoka Misri na kutuongoza kupitia nyika kame, kupitia nchi ya majangwa na mabonde, nchi ya ukame na giza, nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake wala hakuna mtu aishiye humo?’
Eles não disseram: 'Onde está Javé que nos tirou da terra do Egito', que nos conduziu através do deserto, através de uma terra de desertos e de fossos, através de uma terra de seca e da sombra da morte, através de uma terra por onde ninguém passava, e onde nenhum homem vivia'?
7 Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu ili mpate kula matunda yake na utajiri wa mazao yake. Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu, na kuufanya urithi wangu chukizo.
Eu o trouxe para uma terra abundante para comer seus frutos e sua bondade; mas quando você entrou, você contaminou minha terra, e fez de minha herança uma abominação.
8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana?’ Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi; viongozi waliasi dhidi yangu. Manabii walitabiri kwa jina la Baali, wakifuata sanamu zisizofaa.
Os padres não disseram: “Onde está Yahweh?”. e aqueles que lidam com a lei não me conheciam. Os governantes também transgrediram contra mim, e os profetas profetizados por Ba'al e seguiu coisas que não lucram.
9 “Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,” asema Bwana. “Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.
“Portanto, ainda vou contender com você”, diz Yahweh, “e eu lutarei com os filhos de seus filhos”.
10 Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu nawe uangalie, tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini, uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.
Para passar para as ilhas de Kittim, e veja. Envie para Kedar, e considere com diligência, e ver se isso já existiu.
11 Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote? (Hata ingawa hao si miungu kamwe.) Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao kwa sanamu zisizofaa kitu.
Tem uma nação que mudou seus deuses, que realmente não são deuses? Mas meu povo mudou sua glória por aquilo que não beneficia.
12 Shangaeni katika hili, ee mbingu, nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,” asema Bwana.
“Fiquem surpreendidos, vocês, céus, com isto e ter um medo horrível. Seja muito desolado”, diz Yahweh.
13 “Watu wangu wametenda dhambi mbili: Wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji yaliyo hai, nao wamejichimbia visima vyao wenyewe, visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.
“Pois meu povo cometeu dois males: eles me abandonaram, a fonte das águas vivas, e cortam cisternas para si mesmos: cisternas quebradas que não conseguem segurar água.
14 Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa? Kwa nini basi amekuwa mateka?
Israel é um escravo? Ele nasceu na escravidão? Por que ele se tornou um cativo?
15 Simba wamenguruma; wamemngurumia. Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.
Os jovens leões rugiram para ele e levantaram suas vozes. Eles fizeram de sua terra um desperdício. Suas cidades estão incendiadas, sem habitantes.
16 Pia watu wa Memfisi na Tahpanhesi wamevunja taji ya kichwa chako.
As crianças também de Memphis e Tahpanhes quebraram a coroa de sua cabeça.
17 Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe kwa kumwacha Bwana, Mungu wako alipowaongoza njiani?
“Você não trouxe isto a si mesmo, em que você abandonou Yahweh seu Deus, quando ele o conduziu pelo caminho?
18 Sasa kwa nini uende Misri kunywa maji ya Shihori? Nawe kwa nini kwenda Ashuru kunywa maji ya Mto Frati?
Agora, o que você ganha indo ao Egito, para beber as águas do Shihor? Ou por que você deve ir a caminho da Assíria, para beber as águas do rio?
19 Uovu wako utakuadhibu; kurudi nyuma kwako kutakukemea. Basi kumbuka, utambue jinsi lilivyo ovu na chungu kwako unapomwacha Bwana Mungu wako na kutokuwa na hofu yangu,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
“Sua própria maldade irá corrigi-lo, e seu recuo irá repreendê-lo. Saiba e veja, portanto, que é uma coisa má e amarga, que você abandonou Yahweh seu Deus, e que meu medo não esteja em você”, diz o Senhor, Javé dos Exércitos.
20 “Zamani nilivunja nira yako na kukatilia mbali vifungo vyako; ukasema, ‘Sitakutumikia!’ Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda matawi yake ulijilaza kama kahaba.
“Há muito tempo eu quebrei o seu jugo, e romper seus laços. Você disse: “Eu não vou servir; em cada colina alta e sob cada árvore verde que você mesmo se curvou, fazendo-se de prostituta.
21 Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana, mkamilifu na wa mbegu nzuri. Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami, ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?
Yet Eu tinha plantado uma nobre videira para você, uma semente pura e fiel. Como então você se tornou para mim os ramos degenerados de uma videira estrangeira?
22 Hata ujisafishe kwa magadi na kutumia sabuni nyingi, bado doa la hatia yako liko mbele zangu,” asema Bwana Mwenyezi.
Pois embora você se lave com lixívia, e usar muito sabão, no entanto, sua iniquidade está marcada diante de mim”, diz o Senhor Yahweh.
23 “Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi, sijawafuata Mabaali’? Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni; fikiri uliyoyafanya. Wewe ni ngamia jike mwenye mbio ukikimbia hapa na pale,
“Como você pode dizer: 'Eu não estou contaminado'. Eu não fui atrás dos Baals'? Veja seu caminho no vale. Saiba o que você tem feito. Você é um rápido dromedário percorrendo seus caminhos,
24 punda-mwitu aliyezoea jangwa, anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa: katika wakati wake wa kuhitaji mbegu ni nani awezaye kumzuia? Madume yoyote yanayomfuatilia hayana haja ya kujichosha; wakati wa kupandwa kwake watampata tu.
um burro selvagem acostumado com a natureza, que fareja o vento em sua ânsia. Quando ela está no cio, quem pode recusá-la? Todos aqueles que a procuram não se cansarão. Em seu mês, eles a encontrarão.
25 Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu, na koo lako liwe limekauka. Lakini ulisema, ‘Haina maana! Ninaipenda miungu ya kigeni, nami lazima niifuatie.’
“Não fique com os pés descalços, e sua garganta da sede. Mas você disse: “É em vão”. Não, pois eu amei estranhos, e eu irei atrás deles”.
26 “Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa, hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa: wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao.
Como o ladrão se envergonha quando é encontrado, por isso a casa de Israel está envergonhada... eles, seus reis, seus príncipes, seus sacerdotes e seus profetas,
27 Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’ nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’ Wamenipa visogo vyao wala hawakunigeuzia nyuso zao; lakini wakiwa katika taabu, wanasema, ‘Njoo utuokoe!’
que dizem à madeira: 'Você é meu pai'. e uma pedra, 'Você me deu à luz'. pois eles viraram as costas para mim, e não a cara deles, mas no momento de seus problemas eles dirão: “Levantem-se e nos salvem!
28 Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea? Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa wakati mko katika taabu! Kwa maana mna miungu mingi kama mlivyo na miji, ee Yuda.
“Mas onde estão seus deuses que vocês fizeram para si mesmos? Deixe-os surgir, se eles puderem salvá-lo no tempo de seu problema, pois você tem tantos deuses quanto cidades, ó Judá.
29 “Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu? Ninyi nyote mmeniasi,” asema Bwana.
“Por que você vai contender comigo? Todos vocês transgrediram contra mim”, diz Yahweh.
30 “Nimeadhibu watu wako bure tu, hawakujirekebisha. Upanga wako umewala manabii wako kama simba mwenye njaa.
“Eu bati em seus filhos em vão. Eles não receberam nenhuma correção. Sua própria espada devorou seus profetas, como um leão destruidor.
31 “Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana: “Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi ya giza kuu? Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura, hatutarudi kwako tena’?
Geração, considere a palavra de Yahweh. Eu tenho sido um sertão selvagem para Israel? Ou uma terra de escuridão espessa? Por que meu povo diz: “Nós nos soltamos”. Não iremos mais até você”?
32 Je, mwanamwali husahau vito vyake, au bibi arusi mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau mimi, tena kwa siku zisizo na hesabu.
“Uma virgem pode esquecer seus enfeites, ou uma noiva com seus trajes? No entanto, meu povo me esqueceu por dias sem número.
33 Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi! Hata wale wanawake wabaya kuliko wote wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.
Como você prepara bem seu caminho para buscar o amor! Portanto, você até ensinou seus caminhos às mulheres perversas.
34 Katika nguo zako watu huona damu ya uhai ya maskini wasio na hatia, ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba. Lakini katika haya yote
Também o sangue das almas dos pobres inocentes é encontrado em suas saias. Você não os encontrou arrombando a porta, mas é por causa de todas essas coisas.
35 unasema, ‘Sina hatia; Mungu hajanikasirikia.’ Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema, ‘Mimi sijatenda dhambi.’
“No entanto, o senhor disse: 'Estou inocente'. Certamente sua raiva se desviou de mim”. “Eis que eu o julgarei”, porque você diz: “Eu não pequei”.
36 Kwa nini unatangatanga sana, kubadili njia zako? Utakatishwa tamaa na Misri kama ulivyokatishwa na Ashuru.
Por que você se esforça tanto para mudar seus caminhos? Você também terá vergonha do Egito, como você tinha vergonha da Assíria.
37 Pia utaondoka mahali hapo ukiwa umeweka mikono kichwani, kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia; hutasaidiwa nao.
Você também deixará esse lugar com as mãos na cabeça; pois Yahweh rejeitou aqueles em quem você confia, e você não prosperará com eles.