< Yeremia 2 >
1 Neno la Bwana lilinijia kusema,
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu.
Va, et crie aux oreilles de Jérusalem, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Je me suis souvenu de toi, ayant compassion de ta jeunesse, et de l’amour de tes fiançailles, lorsque tu me suivis dans le désert, dans une terre qui n’est pas cultivée.
3 Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana, kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia, nayo maafa yaliwakumba,’” asema Bwana.
Israël a été consacré au Seigneur; il est les prémices de ses fruits; tous ceux qui le dévorent se rendent coupables; les maux viendront sur eux, dit le Seigneur.
4 Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.
Ecoutez la parole du Seigneur, maison de Jacob, et vous toutes, les familles d’Israël.
5 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu, hata wakatangatanga mbali nami hivyo? Walifuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai.
Voici ce que dit le Seigneur: Quelle iniquité ont trouvée vos pères en moi, pour s’être éloignés de moi, avoir couru après la vanité, et être devenus vains eux-mêmes?
6 Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana, aliyetupandisha kutoka Misri na kutuongoza kupitia nyika kame, kupitia nchi ya majangwa na mabonde, nchi ya ukame na giza, nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake wala hakuna mtu aishiye humo?’
Et ils n’ont pas dit: Où est le Seigneur qui nous a fait monter de la terre d’Egypte; qui nous a conduits à travers le désert, par une terre inhabitable et inaccessible, par une terre aride et image de la mort, par une terre dans laquelle homme n’a passé, et homme n’a habité?
7 Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu ili mpate kula matunda yake na utajiri wa mazao yake. Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu, na kuufanya urithi wangu chukizo.
Et je vous ai fait entrer dans une terre de carmel, afin que vous en mangiez les fruits et que vous jouissiez de ses biens; et étant entrés, vous avez souillé ma terre, et de mon héritage vous avez fait une abomination.
8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana?’ Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi; viongozi waliasi dhidi yangu. Manabii walitabiri kwa jina la Baali, wakifuata sanamu zisizofaa.
Les prêtres n’ont pas dit: Où est le Seigneur? les dépositaires de la loi ne m’ont pas connu, les pasteurs ont prévariqué contre moi, et les prophètes ont prophétisé au nom de Baal, et ont suivi les idoles.
9 “Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,” asema Bwana. “Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.
À cause de cela, j’entrerai encore en jugement avec vous, dit le Seigneur, et avec vos fils je discuterai.
10 Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu nawe uangalie, tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini, uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.
Passez aux îles de Céthim, et voyez; et envoyez à Cédar, et considérez avec le plus grand soin, et voyez s’il y a été fait quelque chose de semblable;
11 Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote? (Hata ingawa hao si miungu kamwe.) Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao kwa sanamu zisizofaa kitu.
Si une nation a changé ses dieux, et certainement ce ne sont pas des dieux; et cependant mon peuple a changé sa gloire en une idole.
12 Shangaeni katika hili, ee mbingu, nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,” asema Bwana.
Cieux, soyez frappés de stupeur sur cela; et vous, portes du ciel, soyez dans la plus grande désolation, dit le Seigneur.
13 “Watu wangu wametenda dhambi mbili: Wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji yaliyo hai, nao wamejichimbia visima vyao wenyewe, visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.
Car mon peuple a fait deux maux: ils m’ont abandonné, moi, source d’eau vive, et ils se sont creusé des citernes, des citernes entr’ouvertes qui ne peuvent retenir les eaux.
14 Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa? Kwa nini basi amekuwa mateka?
Est-ce qu’Israël est un esclave ou fils d’un esclave? pourquoi donc est-il devenu en proie?
15 Simba wamenguruma; wamemngurumia. Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.
Les lions ont rugi sur lui, ils ont fait entendre leur voix, ils ont réduit sa terre en une solitude; ses cités ont été brûlées, et il n’y a personne qui y habite.
16 Pia watu wa Memfisi na Tahpanhesi wamevunja taji ya kichwa chako.
Les fils de Memphis et de Taphnès t’ont déshonorée jusqu’au sommet de la tête.
17 Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe kwa kumwacha Bwana, Mungu wako alipowaongoza njiani?
Est-ce que tout cela ne t’est pas arrivé, parce que tu as abandonné le Seigneur ton Dieu, dans le temps même où il te gardait dans la droite voie?
18 Sasa kwa nini uende Misri kunywa maji ya Shihori? Nawe kwa nini kwenda Ashuru kunywa maji ya Mto Frati?
Et maintenant que veux-tu faire dans la voie de l’Egypte? boire de l’eau bourbeuse? et que t’importe la voie des Assyriens? est-ce pour boire de l’eau d’un fleuve?
19 Uovu wako utakuadhibu; kurudi nyuma kwako kutakukemea. Basi kumbuka, utambue jinsi lilivyo ovu na chungu kwako unapomwacha Bwana Mungu wako na kutokuwa na hofu yangu,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Ta malice t’accusera, et ton éloignement de moi te gourmandera. Sache et vois combien il est mal et amer d’avoir abandonné le Seigneur ton Dieu, et de n’avoir plus ma crainte auprès de toi, dit le Seigneur Dieu des armées.
20 “Zamani nilivunja nira yako na kukatilia mbali vifungo vyako; ukasema, ‘Sitakutumikia!’ Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda matawi yake ulijilaza kama kahaba.
Dès les temps anciens tu as brisé mon joug, tu as rompu mes liens et tu as dit: Je ne servirai pas. Sur toute colline élevée, sous tout arbre touffu, tu te prostituais comme une femme de mauvaise vie.
21 Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana, mkamilifu na wa mbegu nzuri. Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami, ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?
Pour moi, je t’avais plantée comme une vigne choisie, comme un plant franc: comment donc es-tu devenue pour moi un plant bâtard, ô vigne étrangère?
22 Hata ujisafishe kwa magadi na kutumia sabuni nyingi, bado doa la hatia yako liko mbele zangu,” asema Bwana Mwenyezi.
Quand tu te laverai s avec du nitre, quand tu multiplierais pour toi le borith, tu es souillée par ton iniquité devant moi, dit le Seigneur Dieu.
23 “Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi, sijawafuata Mabaali’? Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni; fikiri uliyoyafanya. Wewe ni ngamia jike mwenye mbio ukikimbia hapa na pale,
Comment dis-tu: Je ne suis pas souillée, je n’ai pas couru après les Baalim? Regarde tes voies dans la vallée; sache ce que tu as tait; tu es comme un coureur léger étendant ses voies.
24 punda-mwitu aliyezoea jangwa, anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa: katika wakati wake wa kuhitaji mbegu ni nani awezaye kumzuia? Madume yoyote yanayomfuatilia hayana haja ya kujichosha; wakati wa kupandwa kwake watampata tu.
Anesse sauvage accoutumée à vivre dans la solitude, dans le désir de son âme, elle a attiré à elle le vent de son amour; nul ne la détournera: tous ceux qui la cherchent ne se fatigueront pas: ils la trouveront dans ses souillures.
25 Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu, na koo lako liwe limekauka. Lakini ulisema, ‘Haina maana! Ninaipenda miungu ya kigeni, nami lazima niifuatie.’
Préserve ton pied de la nudité, et ton gosier de la soif. Et tu as dit: J’ai perdu tout espoir, je n’en ferai rien; car j’ai aimé avec passion des étrangers, et c’est à leur suite que je marcherai.
26 “Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa, hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa: wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao.
Comme est confondu un voleur, quand il est surpris, ainsi ont été confondus ceux de la maison d’Israël, eux-mêmes, et leurs rois, leurs princes, et leurs prêtres, et leurs prophètes,
27 Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’ nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’ Wamenipa visogo vyao wala hawakunigeuzia nyuso zao; lakini wakiwa katika taabu, wanasema, ‘Njoo utuokoe!’
Disant au bois: Mon père, c’est toi; et à la pierre: C’est toi qui m’as engendré; ils ont tourné vers moi le dos et non la face, et au temps de leur affliction ils diront: Seigneur, levez-vous, et délivrez-nous.
28 Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea? Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa wakati mko katika taabu! Kwa maana mna miungu mingi kama mlivyo na miji, ee Yuda.
Où sont tes dieux que tu t’es faits? qu’ils se lèvent, qu’ils te délivrent au temps de ton affliction; car selon le nombre de tes cités, était le nombre de tes dieux, ô Juda.
29 “Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu? Ninyi nyote mmeniasi,” asema Bwana.
Pourquoi voulez-vous entrer avec moi en jugement? tous, vous m’avez abandonné, dit le Seigneur.
30 “Nimeadhibu watu wako bure tu, hawakujirekebisha. Upanga wako umewala manabii wako kama simba mwenye njaa.
En vain j’ai frappé vos enfants, ils n’ont pas reçu la correction; votre glaive a dévoré vos prophètes; comme un lion destructeur est
31 “Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana: “Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi ya giza kuu? Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura, hatutarudi kwako tena’?
Votre génération. Voyez la parole du Seigneur: Est-ce que je suis devenu pour Israël une solitude ou une terre tardive? Pourquoi donc mon peuple a-t-il dit: Nous nous sommes retirés, nous ne viendrons plus à vous?
32 Je, mwanamwali husahau vito vyake, au bibi arusi mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau mimi, tena kwa siku zisizo na hesabu.
Est-ce qu’une vierge oubliera sa parure; ou une épouse la bandelette qu’elle porte sur la poitrine? mais mon peuple m’a oublié pendant des jours innombrables.
33 Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi! Hata wale wanawake wabaya kuliko wote wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.
Pourquoi t’efforces-tu de montrer comme bonne ta voie, pour rechercher mon amour, lorsque d’ailleurs tu as enseigné tes méchancetés comme étant tes voies,
34 Katika nguo zako watu huona damu ya uhai ya maskini wasio na hatia, ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba. Lakini katika haya yote
Et que dans les pans de ta robe a été trouvé le sang des âmes des pauvres et des innocents? Ce n’est pas dans les fosses que je les ai trouvés; mais dans tous les lieux que j’ai rappelés plus haut.
35 unasema, ‘Sina hatia; Mungu hajanikasirikia.’ Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema, ‘Mimi sijatenda dhambi.’
Et tu as dit: Moi je suis sans péché, et innocente; que votre fureur se détourne donc de moi. Voici que j’entrerai en jugement avec toi, puisque tu as dit: Je n’ai pas péché.
36 Kwa nini unatangatanga sana, kubadili njia zako? Utakatishwa tamaa na Misri kama ulivyokatishwa na Ashuru.
Combien tu es devenue vile en renouvelant tes voies! Ainsi tu seras confondue par l’Egypte, comme tu as été confondue par Assur.
37 Pia utaondoka mahali hapo ukiwa umeweka mikono kichwani, kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia; hutasaidiwa nao.
Car d’elle aussi tu sortiras, et tes mains seront sur ta tête, parce que le Seigneur a brisé cet objet de ton assurance, et tu n’y trouveras rien d’avantageux.