< Yeremia 2 >

1 Neno la Bwana lilinijia kusema,
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu.
to go: went and to call: call out in/on/with ear: hearing Jerusalem to/for to say thus to say LORD to remember to/for you kindness youth your love betrothal your to go: follow you after me in/on/with wilderness in/on/with land: country/planet not to sow
3 Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana, kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia, nayo maafa yaliwakumba,’” asema Bwana.
holiness Israel to/for LORD first: beginning (produce his *Q(K)*) all to eat him be guilty distress: harm to come (in): come to(wards) them utterance LORD
4 Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.
to hear: hear word LORD house: household Jacob and all family house: household Israel
5 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu, hata wakatangatanga mbali nami hivyo? Walifuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai.
thus to say LORD what? to find father your in/on/with me injustice for to remove from upon me and to go: follow after [the] vanity and to become vain
6 Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana, aliyetupandisha kutoka Misri na kutuongoza kupitia nyika kame, kupitia nchi ya majangwa na mabonde, nchi ya ukame na giza, nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake wala hakuna mtu aishiye humo?’
and not to say where? LORD [the] to ascend: rise [obj] us from land: country/planet Egypt [the] to go: take [obj] us in/on/with wilderness in/on/with land: country/planet plain and pit in/on/with land: country/planet dryness and shadow in/on/with land: country/planet not to pass in/on/with her man: anyone and not to dwell man there
7 Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu ili mpate kula matunda yake na utajiri wa mazao yake. Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu, na kuufanya urithi wangu chukizo.
and to come (in): bring [obj] you to(wards) land: country/planet [the] plantation to/for to eat fruit her and goodness her and to come (in): come and to defile [obj] land: country/planet my and inheritance my to set: make to/for abomination
8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana?’ Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi; viongozi waliasi dhidi yangu. Manabii walitabiri kwa jina la Baali, wakifuata sanamu zisizofaa.
[the] priest not to say where? LORD and to capture [the] instruction not to know me and [the] to pasture to transgress in/on/with me and [the] prophet to prophesy in/on/with Baal and after not to gain to go: follow
9 “Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,” asema Bwana. “Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.
to/for so still to contend with you utterance LORD and with son: child son: child your to contend
10 Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu nawe uangalie, tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini, uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.
for to pass coastland Cyprus and to see: see and Kedar to send: depart and to understand much and to see: see look! to be like/as this
11 Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote? (Hata ingawa hao si miungu kamwe.) Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao kwa sanamu zisizofaa kitu.
to exchange nation God and they(masc.) not God and people my to change glory his in/on/with not to gain
12 Shangaeni katika hili, ee mbingu, nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,” asema Bwana.
be desolate: appalled heaven upon this and to shudder to destroy much utterance LORD
13 “Watu wangu wametenda dhambi mbili: Wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji yaliyo hai, nao wamejichimbia visima vyao wenyewe, visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.
for two distress: evil to make people my [obj] me to leave: forsake fountain water alive to/for to hew to/for them cistern cistern to break which not to sustain [the] water
14 Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa? Kwa nini basi amekuwa mateka?
servant/slave Israel if: surely no born house: household he/she/it why? to be to/for plunder
15 Simba wamenguruma; wamemngurumia. Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.
upon him to roar lion to give: cry out voice: sound their and to set: make land: country/planet his to/for horror: destroyed city his (to kindle *Q(K)*) from without to dwell
16 Pia watu wa Memfisi na Tahpanhesi wamevunja taji ya kichwa chako.
also son: descendant/people Memphis (and Tahpanhes *Q(k)*) to pasture you crown
17 Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe kwa kumwacha Bwana, Mungu wako alipowaongoza njiani?
not this to make: do to/for you to leave: forsake you [obj] LORD God your in/on/with time to go: take you in/on/with way: journey
18 Sasa kwa nini uende Misri kunywa maji ya Shihori? Nawe kwa nini kwenda Ashuru kunywa maji ya Mto Frati?
and now what? to/for you to/for way: journey Egypt to/for to drink water Nile and what? to/for you to/for way: journey Assyria to/for to drink water River
19 Uovu wako utakuadhibu; kurudi nyuma kwako kutakukemea. Basi kumbuka, utambue jinsi lilivyo ovu na chungu kwako unapomwacha Bwana Mungu wako na kutokuwa na hofu yangu,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
to discipline you distress: evil your and faithlessness your to rebuke you and to know and to see: see for bad: evil and bitter to leave: forsake you [obj] LORD God your and not dread my to(wards) you utterance Lord YHWH/God Hosts
20 “Zamani nilivunja nira yako na kukatilia mbali vifungo vyako; ukasema, ‘Sitakutumikia!’ Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda matawi yake ulijilaza kama kahaba.
for from forever: antiquity to break yoke your to tear bond your and to say not (to pass: trespass *Q(K)*) for upon all hill high and underneath: under all tree luxuriant you(f. s.) to march to fornicate
21 Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana, mkamilifu na wa mbegu nzuri. Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami, ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?
and I to plant you vine all his seed truth: faithful and how? to overturn to/for me degenerate [the] vine foreign
22 Hata ujisafishe kwa magadi na kutumia sabuni nyingi, bado doa la hatia yako liko mbele zangu,” asema Bwana Mwenyezi.
for if to wash in/on/with lye and to multiply to/for you lye be stained iniquity: guilt your to/for face: before my utterance Lord YHWH/God
23 “Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi, sijawafuata Mabaali’? Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni; fikiri uliyoyafanya. Wewe ni ngamia jike mwenye mbio ukikimbia hapa na pale,
how? to say not to defile after [the] Baal not to go: follow to see: see way: journey your in/on/with valley to know what? to make: do young camel swift to twist way: journey her
24 punda-mwitu aliyezoea jangwa, anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa: katika wakati wake wa kuhitaji mbegu ni nani awezaye kumzuia? Madume yoyote yanayomfuatilia hayana haja ya kujichosha; wakati wa kupandwa kwake watampata tu.
wild donkey disciple wilderness in/on/with desire (soul: myself her *Q(K)*) to long for spirit: breath estrous her who? to return: turn back her all to seek her not to faint in/on/with month her to find her
25 Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu, na koo lako liwe limekauka. Lakini ulisema, ‘Haina maana! Ninaipenda miungu ya kigeni, nami lazima niifuatie.’
to withhold foot your from barefoot (and throat your *Q(K)*) from parched and to say to despair not for to love: lover be a stranger and after them to go: went
26 “Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa, hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa: wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao.
like/as shame thief for to find so be ashamed house: household Israel they(masc.) king their ruler their and priest their and prophet their
27 Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’ nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’ Wamenipa visogo vyao wala hawakunigeuzia nyuso zao; lakini wakiwa katika taabu, wanasema, ‘Njoo utuokoe!’
to say to/for tree father my you(m. s.) and to/for stone you(f. s.) (to beget us *Q(K)*) for to turn to(wards) me neck and not face and in/on/with time distress: harm their to say to arise: rise [emph?] and to save us
28 Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea? Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa wakati mko katika taabu! Kwa maana mna miungu mingi kama mlivyo na miji, ee Yuda.
and where? God your which to make to/for you to arise: rise if to save you in/on/with time distress: harm your for number city your to be God your Judah
29 “Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu? Ninyi nyote mmeniasi,” asema Bwana.
to/for what? to contend to(wards) me all your to transgress in/on/with me utterance LORD
30 “Nimeadhibu watu wako bure tu, hawakujirekebisha. Upanga wako umewala manabii wako kama simba mwenye njaa.
to/for vanity: vain to smite [obj] son: child your discipline not to take: take to eat sword your prophet your like/as lion to ruin
31 “Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana: “Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi ya giza kuu? Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura, hatutarudi kwako tena’?
[the] generation you(m. p.) to see: behold! word LORD wilderness to be to/for Israel if: surely no land: country/planet darkness why? to say people my to roam not to come (in): come still to(wards) you
32 Je, mwanamwali husahau vito vyake, au bibi arusi mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau mimi, tena kwa siku zisizo na hesabu.
to forget virgin ornament her daughter-in-law: bride sash her and people my to forget me day nothing number
33 Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi! Hata wale wanawake wabaya kuliko wote wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.
what? be good way: conduct your to/for to seek love to/for so also [obj] [the] bad: evil (to learn: teach *Q(K)*) [obj] way: conduct your
34 Katika nguo zako watu huona damu ya uhai ya maskini wasio na hatia, ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba. Lakini katika haya yote
also in/on/with wing your to find blood soul: life needy innocent not in/on/with breaking to find them for upon all these
35 unasema, ‘Sina hatia; Mungu hajanikasirikia.’ Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema, ‘Mimi sijatenda dhambi.’
and to say for to clear surely to return: turn back face: anger his from me look! I to judge with you upon to say you not to sin
36 Kwa nini unatangatanga sana, kubadili njia zako? Utakatishwa tamaa na Misri kama ulivyokatishwa na Ashuru.
what? be gone much to/for to change [obj] way: journey your also from Egypt be ashamed like/as as which be ashamed from Assyria
37 Pia utaondoka mahali hapo ukiwa umeweka mikono kichwani, kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia; hutasaidiwa nao.
also from with this to come out: come and hand your upon head your for to reject LORD in/on/with confidence your and not to prosper to/for them

< Yeremia 2 >