< Yeremia 2 >
1 Neno la Bwana lilinijia kusema,
The Lord's message came to me, saying,
2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu.
Go and announce to the people of Jerusalem that this is what the Lord says: I remember when you were young how devoted to me you were. I remember how you loved me when you were my bride. I remember how you followed me in the desert, in a land where nothing is grown.
3 Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana, kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia, nayo maafa yaliwakumba,’” asema Bwana.
Israel was holy to the Lord, the firstfruits of his harvest. Anyone who ate this harvest was guilty of sin, and they experienced the disastrous results, declares the Lord.
4 Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.
Listen to the Lord's message, descendants of Jacob, all you Israelites.
5 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu, hata wakatangatanga mbali nami hivyo? Walifuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai.
This is what the Lord says: What did your forefathers think was wrong with me that they went so far away from me? They went off to worship useless idols, and as a result became useless themselves!
6 Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana, aliyetupandisha kutoka Misri na kutuongoza kupitia nyika kame, kupitia nchi ya majangwa na mabonde, nchi ya ukame na giza, nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake wala hakuna mtu aishiye humo?’
They didn't ask themselves, “Where is the Lord who led us from Egypt, who led us through the wasteland, through a land of deserts and ravines, a land of drought and darkness, a land that no one travels through and where no one lives?”
7 Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu ili mpate kula matunda yake na utajiri wa mazao yake. Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu, na kuufanya urithi wangu chukizo.
I led you into a productive land to eat all the good things that grow there. But you came and made my land unclean, making it offensive to me.
8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana?’ Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi; viongozi waliasi dhidi yangu. Manabii walitabiri kwa jina la Baali, wakifuata sanamu zisizofaa.
Your priests did not ask, “Where is the Lord?” Your teachers of the law no longer believed in me, and your leaders rebelled against me. Your prophets prophesied by calling on Baal and followed worthless idols.
9 “Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,” asema Bwana. “Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.
So I'm going to confront you again, declares the Lord, and I will bring charges against your children's children.
10 Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu nawe uangalie, tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini, uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.
Travel over to the islands of Cyprus and take a look; go to the land of Kedar and examine carefully to see if anything like this has ever happened before.
11 Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote? (Hata ingawa hao si miungu kamwe.) Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao kwa sanamu zisizofaa kitu.
Has a nation ever changed its gods? —even though they're not gods at all! Yet my people have traded their glorious God for worthless idols.
12 Shangaeni katika hili, ee mbingu, nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,” asema Bwana.
You heavens, you should be appalled, shocked and horrified! declares the Lord.
13 “Watu wangu wametenda dhambi mbili: Wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji yaliyo hai, nao wamejichimbia visima vyao wenyewe, visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.
For my people have done two evil things. They have abandoned me, the source of living water, and they have dug their own cisterns—broken cisterns that can't hold water.
14 Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa? Kwa nini basi amekuwa mateka?
Are Israelites slaves? Were they born into slavery? So why have they become victims?
15 Simba wamenguruma; wamemngurumia. Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.
The young lions roared at you; they growled loudly. They have devastated your country; your towns lie in ruins. No one lives there.
16 Pia watu wa Memfisi na Tahpanhesi wamevunja taji ya kichwa chako.
The men of Memphis and Tahpanhes have shaved your heads.
17 Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe kwa kumwacha Bwana, Mungu wako alipowaongoza njiani?
Didn't you bring this on yourself by abandoning the Lord your God when he was leading you in the right way?
18 Sasa kwa nini uende Misri kunywa maji ya Shihori? Nawe kwa nini kwenda Ashuru kunywa maji ya Mto Frati?
Now what will you benefit as you travel back to Egypt to drink the waters of Shihor River? What will you gain on your way to Assyria to drink the waters of the Euphrates River?
19 Uovu wako utakuadhibu; kurudi nyuma kwako kutakukemea. Basi kumbuka, utambue jinsi lilivyo ovu na chungu kwako unapomwacha Bwana Mungu wako na kutokuwa na hofu yangu,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Your own wickedness will discipline you; your own disobedience will teach you a lesson. Think about it and you'll recognize what a bitter evil it is for you to abandon the Lord your God and not to respect me, declares the Lord God Almighty.
20 “Zamani nilivunja nira yako na kukatilia mbali vifungo vyako; ukasema, ‘Sitakutumikia!’ Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda matawi yake ulijilaza kama kahaba.
You broke off your yoke and ripped off your chains long ago. “I won't worship you!” you declared. On the contrary, you lay down like a prostitute on every high hill and under every green tree.
21 Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana, mkamilifu na wa mbegu nzuri. Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami, ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?
I was the one who planted you like the finest vine, grown from the very best seed. How could you degenerate into a useless wild vine?
22 Hata ujisafishe kwa magadi na kutumia sabuni nyingi, bado doa la hatia yako liko mbele zangu,” asema Bwana Mwenyezi.
Even bleach and plenty of soap can't get rid of your guilty stains. I still see them, declares the Lord God.
23 “Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi, sijawafuata Mabaali’? Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni; fikiri uliyoyafanya. Wewe ni ngamia jike mwenye mbio ukikimbia hapa na pale,
How dare you say, “I'm not unclean! I haven't gone to worship the Baals!” Look at what you've been doing down in the valley. Admit what you've done! You're a young female camel, racing around everywhere.
24 punda-mwitu aliyezoea jangwa, anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa: katika wakati wake wa kuhitaji mbegu ni nani awezaye kumzuia? Madume yoyote yanayomfuatilia hayana haja ya kujichosha; wakati wa kupandwa kwake watampata tu.
You're a female donkey living in the desert, sniffing the wind for a mate because she's in heat. No one can control her at mating time. All those who're looking for her won't have trouble finding her when she's in heat.
25 Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu, na koo lako liwe limekauka. Lakini ulisema, ‘Haina maana! Ninaipenda miungu ya kigeni, nami lazima niifuatie.’
You don't have to run around barefoot or have your throat go dry. But you reply, “No, it's impossible! I'm in love with foreign gods—I must go to them.”
26 “Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa, hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa: wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao.
In the same way that a thief feels guilty when they're caught, so the people of Israel have been shamed. All of them—their kings, their officials, their priests, and their prophets.
27 Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’ nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’ Wamenipa visogo vyao wala hawakunigeuzia nyuso zao; lakini wakiwa katika taabu, wanasema, ‘Njoo utuokoe!’
They say to an idol made of wood, “You are my father,” and one made of stone, “You gave birth to me.” They turn their backs on me, and hide their faces from me. But when they're in trouble they come begging to me, saying, “Please come and save us!”
28 Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea? Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa wakati mko katika taabu! Kwa maana mna miungu mingi kama mlivyo na miji, ee Yuda.
So where are these “gods” of yours that you made for yourselves? Let them come and help you when you're in trouble! Let them save you if they can, because you Israelites have as many gods as you have towns.
29 “Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu? Ninyi nyote mmeniasi,” asema Bwana.
Why are you complaining to me? It's all of you who have all rebelled against me! declares the Lord.
30 “Nimeadhibu watu wako bure tu, hawakujirekebisha. Upanga wako umewala manabii wako kama simba mwenye njaa.
It was pointless of me to punish your children because they refused to accept any discipline. You used your own swords to kill your prophets, destroying them like a ferocious lion.
31 “Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana: “Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi ya giza kuu? Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura, hatutarudi kwako tena’?
You people of today, think about what the Lord is saying: Israel, have I treated you like an empty desert, or a land of thick darkness? Why are my people saying, “We can go where we like! We don't have to come and worship you any more”?
32 Je, mwanamwali husahau vito vyake, au bibi arusi mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau mimi, tena kwa siku zisizo na hesabu.
Does a girl forget her jewelry or a bride her wedding dress? Yet my people have forgotten me for too many years to count.
33 Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi! Hata wale wanawake wabaya kuliko wote wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.
How cleverly you look for your lovers! Even prostitutes could learn something from you!
34 Katika nguo zako watu huona damu ya uhai ya maskini wasio na hatia, ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba. Lakini katika haya yote
On top of that, your clothes are stained with the blood of the poor and the innocent. It's not like you killed them breaking into your homes. Despite all this,
35 unasema, ‘Sina hatia; Mungu hajanikasirikia.’ Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema, ‘Mimi sijatenda dhambi.’
you go on saying, “I'm innocent! Surely he can't still be upset with me!” Watch out! I'm going to punish you because you go on saying, “I haven't sinned.”
36 Kwa nini unatangatanga sana, kubadili njia zako? Utakatishwa tamaa na Misri kama ulivyokatishwa na Ashuru.
You're just so fickle—you keep on changing your mind! You will end up just as disappointed by your alliance with Egypt as you were with Assyria.
37 Pia utaondoka mahali hapo ukiwa umeweka mikono kichwani, kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia; hutasaidiwa nao.
In fact you will go into exile with your hands on your head as prisoners, because the Lord will have nothing to do with those you trust; they will be no help to you.