< Yeremia 19 >
1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
Ainsi dit l’Éternel: Va, et achète un vase de potier, et [prends] des anciens du peuple et des anciens des sacrificateurs,
2 na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
et sors vers la vallée du fils de Hinnom, qui est à l’entrée de la porte de la poterie, et crie là les paroles que je te dirai,
3 nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
et dis: Écoutez la parole de l’Éternel, vous, rois de Juda, et vous, habitants de Jérusalem: Ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Voici, je fais venir sur ce lieu-ci un mal tel, que quiconque l’entendra, les oreilles lui tinteront;
4 Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
parce qu’ils m’ont abandonné, et qu’ils m’ont aliéné ce lieu, et qu’ils y ont brûlé de l’encens à d’autres dieux que n’ont connus ni eux, ni leurs pères, ni les rois de Juda, et qu’ils ont rempli ce lieu du sang des innocents,
5 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
et ont bâti les hauts lieux de Baal, pour brûler au feu leurs fils en holocauste à Baal; ce que je n’ai point commandé, et dont je n’ai point parlé, et qui ne m’est point monté au cœur.
6 Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
C’est pourquoi, voici, des jours viennent, dit l’Éternel, où ce lieu-ci ne sera plus appelé Topheth, ni la vallée du fils de Hinnom, mais la vallée de la tuerie.
7 “‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
Et je rendrai vain le conseil de Juda et de Jérusalem dans ce lieu-ci, et je les ferai tomber par l’épée devant leurs ennemis et par la main de ceux qui cherchent leur vie, et je donnerai leurs cadavres en pâture aux oiseaux des cieux et aux bêtes de la terre.
8 Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
Et je ferai de cette ville un sujet d’étonnement et de sifflement: quiconque passera à côté d’elle s’étonnera et sifflera sur toutes ses plaies.
9 Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
Et je leur ferai manger la chair de leurs fils et la chair de leurs filles; et ils mangeront chacun la chair de son prochain, dans le siège et dans la détresse dont les enserreront leurs ennemis et ceux qui cherchent leur vie.
10 “Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
Et tu briseras le vase devant les yeux des hommes qui sont allés avec toi,
11 uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
et tu leur diras: Ainsi dit l’Éternel des armées: Je briserai ainsi ce peuple et cette ville, comme on brise un vase de potier qui ne peut être raccommodé; et on enterrera à Topheth, jusqu’à ce qu’il n’y ait plus de place pour enterrer.
12 Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
Je ferai ainsi à ce lieu, dit l’Éternel, et à ses habitants, pour rendre cette ville semblable à Topheth;
13 Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
et les maisons de Jérusalem et les maisons des rois de Juda seront, comme le lieu de Topheth, impures, – toutes les maisons sur les toits desquelles ils ont brûlé de l’encens à toute l’armée des cieux, et ont répandu des libations à d’autres dieux.
14 Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
Et Jérémie vint de Topheth, où l’Éternel l’avait envoyé pour prophétiser; et il se tint dans le parvis de la maison de l’Éternel, et dit à tout le peuple:
15 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”
Ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Voici, je fais venir sur cette ville, et sur toutes ses villes, tout le mal que j’ai prononcé contre elle, parce qu’ils ont roidi leur cou pour ne point écouter mes paroles.