< Yeremia 19 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
Ainsi parle Yahvé: Va, achète un vase de terre de potier, prends quelques anciens du peuple et des anciens des prêtres,
2 na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
et va dans la vallée du fils de Hinnom, qui est à l'entrée de la porte Harsith, et proclame là les paroles que je te dirai.
3 nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
Dites: « Écoutez la parole de Yahvé, rois de Juda et habitants de Jérusalem: Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici que je vais faire venir sur ce lieu un malheur dont l'oreille de celui qui l'entendra frissonnera.
4 Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
Parce qu'ils m'ont abandonné, parce qu'ils ont souillé ce lieu, parce qu'ils y ont offert de l'encens à d'autres dieux qu'ils ne connaissaient pas, eux, leurs pères, et les rois de Juda, parce qu'ils ont rempli ce lieu du sang des innocents,
5 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
parce qu'ils ont bâti les hauts lieux de Baal, et qu'ils ont brûlé leurs enfants au feu en holocauste à Baal, ce que je n'ai ni ordonné, ni dit, ce qui ne m'est pas venu à l'esprit.
6 Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
C'est pourquoi voici, les jours viennent, dit Yahvé, où ce lieu ne sera plus appelé Topheth, ni vallée du fils de Hinnom, mais vallée du carnage.
7 “‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
"''Je réduirai à néant le conseil de Juda et de Jérusalem en ce lieu. Je les ferai tomber par l'épée devant leurs ennemis, et par la main de ceux qui en veulent à leur vie. Je donnerai leurs cadavres en pâture aux oiseaux du ciel et aux animaux de la terre.
8 Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
Je ferai de cette ville un objet d'étonnement et un sifflement. Tous ceux qui passeront près d'elle seront étonnés et siffleront à cause de tous ses fléaux.
9 Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
Je leur ferai manger la chair de leurs fils et la chair de leurs filles. Ils mangeront chacun la chair de leur ami dans le siège et dans la détresse avec lesquels leurs ennemis, et ceux qui en veulent à leur vie, les accableront. »''
10 “Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
« Puis tu briseras le récipient sous les yeux des hommes qui t'accompagnent,
11 uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
et tu leur diras: « Yahvé des armées dit: « Je briserai ce peuple et cette ville comme on brise le vase d'un potier, qui ne peut plus être reconstitué. Ils enterreront à Topheth jusqu'à ce qu'il n'y ait plus de place pour enterrer.
12 Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
C'est ce que je ferai à ce lieu, dit Yahvé, et à ses habitants, et je rendrai cette ville semblable à Topheth.
13 Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
Les maisons de Jérusalem et les maisons des rois de Juda, qui sont souillées, seront comme le lieu de Topheth, toutes les maisons sur les toits desquelles on a brûlé de l'encens à toute l'armée du ciel et versé des libations à d'autres dieux. »'"
14 Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
Jérémie revint de Topheth, où Yahvé l'avait envoyé prophétiser, et il se tint dans le parvis de la maison de Yahvé, et dit à tout le peuple:
15 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”
« Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici, je vais faire venir sur cette ville et sur toutes ses cités tous les malheurs que j'ai prononcés contre elle, parce qu'ils ont raidi leur cou pour ne pas entendre mes paroles. »

< Yeremia 19 >