< Yeremia 19 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
The Lord seith these thingis, Go thou, and take an erthene potel of a pottere, of the eldre men of the puple, and of the eldre men of preestis.
2 na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
And go thou out to the valei of the sones of Ennon, which is bisidis the entring of the erthene yate; and there thou schalt preche the wordis whiche Y schal speke to thee;
3 nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
and thou schalt seie, Kyngis of Juda, and the dwelleris of Jerusalem, here ye the word of the Lord. The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Lo! Y schal bringe in turment on this place, so that ech man that herith it, hise eeris tyngle.
4 Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
For thei han forsake me, and maad alien this place, and offriden sacrifices to alien goddis ther ynne, whiche thei, and the fadris of hem, and the kingis of Juda, knewen not; and thei filliden this place with the blood of innocentis,
5 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
and bildiden hiy thingis to Baalym, to brenne her sones in fier, in to brent sacrifice to Baalym; whiche thingis Y comaundide not, nether spak, nether tho stieden in to myn herte.
6 Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
Therfor the Lord seith, Lo! daies comen, and this place schal no more be clepid Tophet, and the valei of the sone of Ennon, but the valei of sleyng.
7 “‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
And Y schal distrie the councel of Juda and of Jerusalem in this place, and Y schal distrie hem bi swerd, in the siyt of her enemyes, and in the hond of men sekynge the lyues of hem; and Y schal yyue her deed bodies mete to the briddis of the eir, and to beestis of erthe.
8 Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
And Y schal sette this citee in to wondring, and in to hissing; ech that passith bi it, schal wondre, and hisse on al the veniaunce therof.
9 Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
And Y schal feede hem with the fleischis of her sones, and with the fleischis of her douytris; and ech man schal ete the fleischis of his frend in the bisegyng and angwisch, in which the enemyes of hem, and thei that seken the lyues of hem, schulen close hem togidere.
10 “Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
And thou schalt al to-breke the potel bifore the iyen of the men, that schulen go with thee.
11 uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
And thou schalt seie to hem, The Lord of oostis seith these thingis, So Y schal al to-breke this puple, and this citee, as the vessel of a pottere is al to-brokun, which mai no more be restorid; and thei schulen be biried in Tophet, for noon other place is to birie.
12 Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
So Y schal do to this place, seith the Lord, and to dwelleris therof, that Y sette this citee as Tophet.
13 Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
And the housis of Jerusalem, and the housis of the kingis of Juda, schulen be as the place of Tophet; alle the vncleene housis, in whose roouys thei sacrifieden to al the chyualrie of heuene, and offriden moist sacrifices to alien goddis.
14 Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
Forsothe Jeremye cam fro Tophet, whidur the Lord hadde sente hym for to profesie; and he stood in the porche of the hous of the Lord,
15 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”
and seide to al the puple, The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Lo! Y schal bringe in on this citee, and on alle the citees therof, alle the yuelis whiche Y spak ayens it; for thei maden hard her nol, that thei herden not my wordis.

< Yeremia 19 >