< Yeremia 18 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word which came to Jeremiah from the LORD, saying,
2 “Shuka uende mpaka nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu.”
Arise, and go down to the potter's house, and there I will cause thee to hear my words.
3 Kwa hiyo nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake.
Then I went down to the potter's house, and behold, he wrought a work on the wheels.
4 Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake, hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kama vile ilivyoonekana vyema kwake yeye.
And the vessel that he made of clay was marred in the hand of the potter: so he made it again another vessel, as it seemed good to the potter to make [it].
5 Kisha neno la Bwana likanijia kusema:
Then the word of the LORD came to me, saying,
6 “Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?” asema Bwana. “Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.
O house of Israel, cannot I do with you as this potter? saith the LORD. Behold, as the clay [is] in the potter's hand, so [are] ye in my hand, O house of Israel.
7 Ikiwa wakati wowote nikitangaza kuwa taifa au ufalme utangʼolewa, utaangushwa na kuangamizwa,
[At what] instant I shall speak concerning a nation, and concerning a kingdom, to pluck up, and to pull down, and to destroy [it];
8 ikiwa lile taifa nililolionya litatubia uovu wake, ndipo nitakapokuwa na huruma, wala sitawapiga kwa maafa niliyokuwa nimewakusudia.
If that nation against which I have pronounced, shall turn from their evil, I will repent of the evil that I thought to do to them.
9 Ikiwa wakati mwingine nitatangaza kuwa taifa ama utawala ujengwe na kuwekwa wakfu,
And [at what] instant I shall speak concerning a nation, and concerning a kingdom, to build and to plant [it];
10 ikiwa utafanya maovu mbele zangu na hukunitii, ndipo nitakapoghairi makusudio yangu mema niliyokuwa nimeyakusudia.
If it shall do evil in my sight, that it obey not my voice, then I will repent of the good, with which I said I would benefit them.
11 “Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama! Ninaandaa maafa kwa ajili yenu, nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’
Now therefore come, speak to the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem, saying, Thus saith the LORD; Behold, I frame evil against you, and devise a device against you: return ye now every one from his evil way, and make your ways and your doings good.
12 Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’”
And they said, There is no hope: but we will walk after our own devices, and we will every one do the imagination of his evil heart.
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Ulizia miongoni mwa mataifa: Ni nani alishasikia jambo kama hili? Jambo la kutisha sana limefanywa na Bikira Israeli.
Therefore thus saith the LORD; Ask ye now among the heathen, who hath heard such things: the virgin of Israel hath done a very horrible thing.
14 Je, barafu ya Lebanoni iliwahi kutoweka kwenye miteremko yake ya mawe wakati wowote? Je, maji yake baridi yatokayo katika vyanzo vilivyo mbali yaliwahi kukoma kutiririka wakati wowote?
Will [a man] leave the snow of Lebanon [which cometh] from the rock of the field? [or] shall the cold flowing waters that come from another place be forsaken?
15 Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanafukizia uvumba sanamu zisizofaa kitu, zilizowafanya wajikwae katika njia zao na katika mapito ya zamani. Zimewafanya wapite kwenye vichochoro na kwenye barabara ambazo hazikujengwa.
Because my people hath forgotten me, they have burned incense to vanity, and they have caused them to stumble in their ways [from] the ancient paths, to walk in paths, [in] a way not cast up;
16 Nchi yao itaharibiwa, itakuwa kitu cha kudharauliwa daima; wote wapitao karibu nayo watashangaa na kutikisa vichwa vyao.
To make their land desolate, [and] a perpetual hissing; every one that passeth by it shall be astonished, and wag his head.
17 Kama upepo utokao mashariki, nitawatawanya mbele ya adui zao; nitawapa kisogo wala sio uso, katika siku ya maafa yao.”
I will scatter them as with an east wind before the enemy; I will show them the back, and not the face, in the day of their calamity.
18 Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
Then said they, Come, and let us devise devices against Jeremiah; for the law shall not perish from the priest, nor counsel from the wise, nor the word from the prophet. Come, and let us smite him with the tongue, and let us not give heed to any of his words.
19 Nisikilize, Ee Bwana, sikia wanayosema washtaki wangu!
Give heed to me, O LORD, and hearken to the voice of them that contend with me.
20 Je, mema yalipwe kwa mabaya? Lakini wao wamenichimbia shimo. Kumbuka kwamba nilisimama mbele yako na kunena mema kwa ajili yao, ili wewe ugeuze hasira yako kali mbali nao.
Shall evil be recompensed for good? for they have digged a pit for my soul. Remember that I stood before thee to speak good for them, [and] to turn away thy wrath from them.
21 Kwa hiyo uwaache watoto wao waone njaa; uwaache wauawe kwa makali ya upanga. Wake zao wasiwe na watoto, na wawe wajane; waume wao wauawe, nao vijana wao waume wachinjwe kwa upanga vitani.
Therefore deliver their children to the famine, and pour out their [blood] by the force of the sword; and let their wives be bereaved of their children, and [be] widows; and let their men be put to death; [let] their young men [be] slain by the sword in battle.
22 Kilio na kisikike kutoka kwenye nyumba zao ghafula uwaletapo adui dhidi yao, kwa kuwa wamechimba shimo ili kunikamata na wameitegea miguu yangu mitego.
Let a cry be heard from their houses, when thou shalt bring a troop suddenly upon them: for they have digged a pit to take me, and hid snares for my feet.
23 Lakini unajua, Ee Bwana, hila zao zote za kuniua. Usiyasamehe makosa yao wala usifute dhambi zao mbele za macho yako. Wao na waangamizwe mbele zako; uwashughulikie wakati wa hasira yako.
Yet, LORD, thou knowest all their counsel against me to slay [me]: forgive not their iniquity, neither blot out their sin from thy sight, but let them be overthrown before thee; deal [thus] with them in the time of thy anger.

< Yeremia 18 >