< Yeremia 18 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word which came to Jeremiah from Jehovah, saying:
2 “Shuka uende mpaka nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu.”
Arise, and go down to the potter's house, and there will I cause thee to hear my words.
3 Kwa hiyo nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake.
So I went down to the potter's house, and behold, he was at work at the wheel.
4 Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake, hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kama vile ilivyoonekana vyema kwake yeye.
And the vessel which he was making of clay was marred in the hand of the potter; so he began anew and made it another vessel, as seemed good to the potter to make it.
5 Kisha neno la Bwana likanijia kusema:
Then came the word of Jehovah to me, saying:
6 “Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?” asema Bwana. “Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.
Cannot I do after the manner of this potter With respect to you. O house of Israel, saith Jehovah? Behold, as the clay is in the hand of the potter, So are ye in my hand, O house of Israel!
7 Ikiwa wakati wowote nikitangaza kuwa taifa au ufalme utangʼolewa, utaangushwa na kuangamizwa,
Whenever I speak concerning a nation or a kingdom, That I will pluck it up, cast it down, or destroy it,
8 ikiwa lile taifa nililolionya litatubia uovu wake, ndipo nitakapokuwa na huruma, wala sitawapiga kwa maafa niliyokuwa nimewakusudia.
If that nation shall turn from its wickedness On account of which I threatened it, Then will I repent of the evil which I purposed to do to it.
9 Ikiwa wakati mwingine nitatangaza kuwa taifa ama utawala ujengwe na kuwekwa wakfu,
And whenever I speak concerning a nation or a kingdom, That I will build it, or plant it,
10 ikiwa utafanya maovu mbele zangu na hukunitii, ndipo nitakapoghairi makusudio yangu mema niliyokuwa nimeyakusudia.
And it shall do that which is evil in my sight, And not hearken to my voice, Then will I repent of the good with which I promised to bless them.
11 “Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama! Ninaandaa maafa kwa ajili yenu, nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’
And now speak to the men of Judah, And to the inhabitants of Jerusalem, saying, Thus saith Jehovah: Behold, I am framing evil against you, And meditating a design against you; Return ye now every one from his evil way, And amend your ways and your doings.
12 Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’”
But they say, “There is no remedy, For we will walk after our own devices, And we will practise every one the perverseness of his evil heart.”
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Ulizia miongoni mwa mataifa: Ni nani alishasikia jambo kama hili? Jambo la kutisha sana limefanywa na Bikira Israeli.
Therefore thus saith Jehovah: Inquire ye now among the nations, Who hath heard such things as these? The virgin of Israel hath done a deed of horror.
14 Je, barafu ya Lebanoni iliwahi kutoweka kwenye miteremko yake ya mawe wakati wowote? Je, maji yake baridi yatokayo katika vyanzo vilivyo mbali yaliwahi kukoma kutiririka wakati wowote?
Shall the snow from the rocks of Lebanon forsake my fields? Or shall the cold flowing waters, that come from afar, be dried up?
15 Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanafukizia uvumba sanamu zisizofaa kitu, zilizowafanya wajikwae katika njia zao na katika mapito ya zamani. Zimewafanya wapite kwenye vichochoro na kwenye barabara ambazo hazikujengwa.
Yet my people have forgotten me, And burned incense to vanity; They stumble in their paths, the old ways, And walk in ways that have not been thrown up,
16 Nchi yao itaharibiwa, itakuwa kitu cha kudharauliwa daima; wote wapitao karibu nayo watashangaa na kutikisa vichwa vyao.
To make their land a desolation, A perpetual hissing; Every one that passeth through it shall be amazed, And shake his head.
17 Kama upepo utokao mashariki, nitawatawanya mbele ya adui zao; nitawapa kisogo wala sio uso, katika siku ya maafa yao.”
I will scatter them before the enemy, as with the east wind; I will show them the back, and not the face, In the day of their calamity.
18 Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
But they say, “Come, let us devise measures against Jeremiah; For the law shall not perish from the priest, Nor counsel from the wise, Nor the word from the prophet; Come, let us smite him with the tongue, And not give heed to any of his words.”
19 Nisikilize, Ee Bwana, sikia wanayosema washtaki wangu!
Give heed to me, O Jehovah, And hear the voice of my adversaries!
20 Je, mema yalipwe kwa mabaya? Lakini wao wamenichimbia shimo. Kumbuka kwamba nilisimama mbele yako na kunena mema kwa ajili yao, ili wewe ugeuze hasira yako kali mbali nao.
Shall evil be returned for good? For they have digged a pit for me. Remember how I have stood before thee, To announce good to them, And to turn away thy wrath from them!
21 Kwa hiyo uwaache watoto wao waone njaa; uwaache wauawe kwa makali ya upanga. Wake zao wasiwe na watoto, na wawe wajane; waume wao wauawe, nao vijana wao waume wachinjwe kwa upanga vitani.
Therefore give thou up their sons to famine, And deliver them to the edge of the sword! Let their wives be childless and widows, Let their men be slain by pestilence, And their young men fall by the sword in battle!
22 Kilio na kisikike kutoka kwenye nyumba zao ghafula uwaletapo adui dhidi yao, kwa kuwa wamechimba shimo ili kunikamata na wameitegea miguu yangu mitego.
Let a cry be heard from their houses, When thou shalt bring a troop upon them suddenly! For they have digged a pit to take me, And hidden snares for my feet.
23 Lakini unajua, Ee Bwana, hila zao zote za kuniua. Usiyasamehe makosa yao wala usifute dhambi zao mbele za macho yako. Wao na waangamizwe mbele zako; uwashughulikie wakati wa hasira yako.
Thou, O Jehovah, knowest all their plots against my life! Cover not their iniquity, And blot not out their sin from thy sight! But let them be overthrown before thee; Deal with them in the time of thy wrath!

< Yeremia 18 >