< Yeremia 17 >
1 “Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
Грех Иудин написан есть писалом железным на ногти адамантове, начертан на скрижали сердца их и на розех олтарей их.
2 Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
Егда воспомянут сынове их олтари своя и дубравы своя при древе лиственне и на холмех высоких,
3 Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
о, нагорный (жителю)! Крепость твою и сокровища твоя в расхищение дам, и высокая твоя, грех ради твоих, яже во всех пределех твоих,
4 Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
и останешися един от наследия твоего, еже дах тебе: и служити тя сотворю врагом твоим в земли, еяже не веси: яко огнь разжегл еси в ярости Моей, даже во век горети будет. Сия глаголет Господь:
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
проклят человек, иже надеется на человека и утвердит плоть мышцы своея на нем, и от Господа отступит сердце его:
6 Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
и будет яко дивия мирика в пустыни и не узрит, егда приидут благая, и обитати будет в сухоте и в пустыни, в земли сланей и необитаемей.
7 “Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
И благословен человек, иже надеется на Господа, и будет Господь упование его:
8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
и будет яко древо насажденное при водах, и во влаге пустит корение свое: не убоится, егда приидет зной, и будет на нем стеблие зелено, и во время бездождия не устрашится и не престанет творити плода.
9 Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
Глубоко сердце (человеку) паче всех, и человек есть, и кто познает его?
10 “Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
Аз Господь испытуяй сердца и искушаяй утробы, еже воздати комуждо по пути его и по плодом изобретений его.
11 Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
Возгласи ряб, собра, ихже не роди, творяй богатство свое не с судом: в преполовении дний своих оставит е и на последок свой будет безумен.
12 Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
Престол славы возвышен от начала, место святыни нашея.
13 Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
Чаяние Израилево, Господи! Вси оставляющии Тя да постыдятся, отступающии (от Тебе) на земли да напишутся, яко оставиша источник живых вод, Господа.
14 Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
Изцели мя, Господи, и изцелею: спаси мя, и спасен буду, яко хвала моя Ты еси.
15 Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
Се, тии глаголют ко мне: где есть слово Господне? Да приидет.
16 Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
Аз же не утрудихся, Тебе (пастырю) последуяй, и дне человеча не пожелах: Ты веси исходящая от устен моих, пред лицем Твоим суть:
17 Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
не буди ми во отчуждение, упование мое Ты в день лют.
18 Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
Да постыдятся гонящии мя, аз же да не постыждуся: да устрашатся тии, аз же да не устрашуся: наведи на них день озлобления, сугубым сокрушением сотри их.
19 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
Сия глаголет Господь ко мне: иди и стани во вратех сынов людий твоих, имиже входят царие Иудины и исходят, и во всех вратех Иерусалимских и речеши к ним:
20 Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
слышите слово Господне, царие Иудины и вся Иудеа и весь Иерусалим, входящии во врата сия.
21 Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
Сия глаголет Господь: сохраните душы вашя и не носите бремен в день суббот, и не исходите враты Иерусалима,
22 Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
и не износите бремен из домов ваших в день субботный, и всякаго дела не творите: освятите день субботный, якоже заповедах отцем вашым:
23 Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
и не услышаша, ни приклониша уха своего, но ожесточиша выи своя паче отец своих, да не услышат мя и да не приимут наказания.
24 Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
И будет, аще послушаете Мене, глаголет Господь, еже не вносити бремен во врата града сего в день субботный, и святити день субботный, не творити в онь всякаго дела,
25 ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
и внидут во врата града сего царие и началницы, седящии на престоле Давидове и восходящии на колесницах и конех своих, тии и началницы их, мужие Иудины и обитателие Иерусалима: и обитати будут во граде сем во веки:
26 Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
и приидут от градов Иудиных и от окрестных Иерусалима, и от земли Вениамини и от польных, и от горних и от юга, носяще всесожжения и жертву, и фимиам и манау и ливан, носяще хвалу в дом Господень.
27 Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”
И будет, аще не послушаете Мене еже святити день субботный и не носити бремен, ниже входити вратами Иерусалима в день субботный, то зажгу огнь во вратех его, и пожрет домы Иерусалимли и не угаснет.