< Yeremia 17 >

1 “Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
«ای قوم یهودا، گناهان شما با قلم آهنین و با نوک الماس بر دلهای سنگی‌تان نوشته شده و بر گوشه‌های مذبحهایتان کنده‌کاری شده است.
2 Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
جوانانتان یک دم از گناه غافل نمی‌مانند، زیر هر درخت سبز و روی هر کوه بلند بت می‌پرستند؛ پس به سبب گناهانتان، تمام گنجها و بتخانه‌هایتان را به تاراج خواهم داد،
3 Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
4 Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
و مجبور خواهید شد این سرزمین را که به میراث به شما داده بودم ترک کنید و دشمنانتان را در سرزمینهای دور دست بندگی نمایید، چون آتش خشم مرا شعله‌ور ساخته‌اید، آتشی که هرگز خاموش نخواهد شد!
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
«لعنت بر کسی که به انسان تکیه می‌کند و چشم امیدش به اوست و بر خداوند توکل نمی‌نماید.
6 Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
او مثل بوته‌ای است که در بیابان خشک و سوزان و در شوره‌زارها می‌روید، جایی که هیچ گیاه دیگری وجود ندارد؛ او هرگز خیر و برکت نخواهد دید!
7 “Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
«خوشا به حال کسی که بر خداوند توکل دارد و تمام امید و اعتمادش بر اوست!
8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
او مانند درختی خواهد بود که در کنار رودخانه است و ریشه‌هایش از هر طرف به آب می‌رسد درختی که نه از گرما می‌ترسد و نه از خشکسالی! برگش شاداب می‌ماند و از میوه آوردن باز نمی‌ایستد!
9 Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
«هیچ چیز مانند دل انسان فریبکار و شرور نیست؛ کیست که از آنچه در آن می‌گذرد آگاه باشد؟
10 “Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
تنها من که خداوند هستم می‌دانم در دل انسان چه می‌گذرد! تنها من از درون دل انسان آگاهم و انگیزه‌های او را می‌دانم و هر کس را مطابق اعمالش جزا می‌دهم.»
11 Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
شخصی که ثروتش را از راه نادرست به دست می‌آورد، همانند پرنده‌ای است که لانهٔ خود را از جوجه‌های دیگران پر می‌سازد. همان‌گونه که این جوجه‌ها خیلی زود او را واگذاشته می‌روند، او نیز به‌زودی ثروتش را از دست خواهد داد و سرانجام چوب حماقتش را خواهد خورد.
12 Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
اما ما در برابر تاج جاودانی، رفیع و پرجلال تو ستایش می‌کنیم.
13 Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
ای خداوند، ای امید اسرائیل، تمام کسانی که از تو برگردند، رسوا و شرمسار می‌شوند؛ آنها مانند نوشته‌های روی خاک محو خواهند شد، چون خداوند را که چشمۀ آب حیات است، ترک کرده‌اند.
14 Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
خداوندا، تنها تو می‌توانی مرا شفا بخشی، تنها تو می‌توانی مرا نجات دهی و من تنها تو را ستایش می‌کنم!
15 Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
مردم با تمسخر به من می‌گویند: «پس هشدارهای خداوند که مدام دربارهٔ آنها سخن می‌گفتی چه شد؟ اگر آنها واقعاً از سوی خدا هستند، پس چرا انجام نمی‌شوند؟»
16 Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
خداوندا، من هیچگاه از تو نخواسته‌ام که بر آنها بلا نازل کنی و هرگز خواستار هلاکت ایشان نبوده‌ام؛ تو خوب می‌دانی که من تنها هشدارهای تو را به ایشان اعلام کرده‌ام.
17 Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
خداوندا، مرا به وحشت نیانداز! تنها امید من در روز مصیبت، تو هستی!
18 Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
تمام کسانی را که مرا آزار می‌دهند، به رسوایی و هراس گرفتار بساز، ولی مرا از هر بلایی محفوظ بدار. آری، بر ایشان دو چندان بلا بفرست و نابودشان کن!
19 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
آنگاه خداوند فرمود که بروم و در کنار دروازهٔ قوم که پادشاهان یهودا از آن عبور می‌کنند و در کنار سایر دروازه‌های اورشلیم بایستم،
20 Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
و در آنجا خطاب به همۀ مردم بگویم که خداوند چنین می‌فرماید: «ای پادشاهان و مردم یهودا، ای ساکنان اورشلیم و همۀ کسانی که از این دروازه‌ها عبور می‌کنید،
21 Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
به این هشدار توجه کنید تا زنده بمانید: نباید در روز شَبّات کار کنید بلکه این روز را به عبادت و استراحت اختصاص دهید. به اجدادتان هم همین دستور را دادم،
22 Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
23 Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
ولی آنها گوش ندادند و اطاعت نکردند بلکه با سرسختی به دستور من بی‌توجهی نمودند و اصلاح نشدند.
24 Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
«حال، اگر شما از من اطاعت نمایید و روز شَبّات را مقدّس بدارید و در این روز کار نکنید،
25 ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
آنگاه پادشاهانی که بر تخت داوود می‌نشینند، سوار بر ارابه‌ها و اسبان، همراه با صاحبمنصبان و مردمان یهودا و ساکنان اورشلیم از دروازه‌های این شهر داخل خواهند شد، و این شهر تا به ابد مسکون خواهد ماند.
26 Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
از اطراف اورشلیم و از شهرهای یهودا و سرزمین بنیامین و از دشتها و کوهستانها و جنوب یهودا مردم همه خواهند آمد و قربانیهای گوناگون به خانۀ خداوند تقدیم خواهند نمود.
27 Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”
«اما اگر از من اطاعت نکنید و روز شَبّات را به عبادت و استراحت اختصاص ندهید، و اگر در این روز همچون روزهای دیگر، از دروازه‌های اورشلیم کالا به شهر وارد کنید، آنگاه این دروازه‌ها را به آتش خواهم کشید، آتشی که به کاخهایتان سرایت کند و آنها را از بین ببرد و هیچ‌کس نتواند شعله‌های آن را خاموش کند.»

< Yeremia 17 >