< Yeremia 16 >

1 Kisha neno la Bwana likanijia:
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
Tu ne prendras point de femme, et tu n’auras point de fils et de filles en ce lieu.
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
Parce que voici ce que dit le Seigneur sur les fils et les filles qui sont enfantés en ce lieu, et sur les mères qui les ont enfantés, et sur leurs pères de la souche desquels ils sont nés en cette terre:
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
De différentes morts de maladies ils mourront; ils ne seront pas pleures et ils ne seront pas ensevelis; comme un fumier, ils seront sur la face de la terre; par le glaive et par la famine ils seront consumés, et leur cadavre sera en pâture aux volatiles du ciel et aux bêtes de la terre.
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
Car voici ce que dit le Seigneur: N’entre point dans une maison de festin; et ne va pas pour pleurer, et ne les console point; parce que j’ai retiré ma paix à ce peuple, dit le Seigneur, ma miséricorde et mes bontés.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
Et ils mourront, grands et petits, sur cette terre, et ils ne seront pas ensevelis, ni pleures, et on ne se fera pas d’incision, et on ne se rasera pas la tête pour eux.
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
Et on ne rompra pas parmi eux de pain pour consoler celui qui pleure un mort, et on ne leur donnera pas le calice à boire pour le consoler de la perte de son père et de sa mère.
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
Et tu n’entreras pas dans une maison d’un festin, afin de l’asseoir et de manger et de boire;
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
Parce que voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Voilà que moi j’ôterai de ce lieu, à vos yeux et en vos jours, la voix de la joie et la voix de l’allégresse, la voix de l’époux et la voix de l’épouse.
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
Et lorsque tu annonceras à ce peuple toutes ces paroles, et qu’ils le diront: Pourquoi le Seigneur a-t-il prononcé sur nous tous ces grands maux? quelle est notre iniquité? et quel péché avons-nous commis contre le Seigneur notre Dieu?
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
Tu leur diras: C’est parce que vos pères m’ont abandonné, dit le Seigneur, qu’ils ont couru après des dieux étrangers, qu’ils les ont servis, qu’ils les ont adorés; et qu’ils m’ont abandonné, et qu’ils n’ont point gardé ma loi.
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
Mais vous-même, vous avez fait pis que vos pères; car voilà que chacun marche à la suite de la dépravation de son cœur mauvais, afin de ne pas m’écouter.
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
Et je vous jetterai de cette terre dans une terre que vous ignorez comme vos pères; et vous servirez là des dieux étrangers, le jour et la nuit, qui ne vous donneront pas de repos.
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
À cause de cela, voilà que des jours viennent, dit le Seigneur, et l’on ne dira plus: Le Seigneur vit! qui a retiré les fils d’Israël de la terre d’Egypte,
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
Mais: Vive le Seigneur qui a tiré les fils d’Israël de la terre de l’aquilon, et de toutes les terres où je les ai jetés; et je les ramènerai dans leur terre que j’ai donnée à leurs pères.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
Voilà que moi j’enverrai des pêcheurs nombreux, dit le Seigneur, et ils pécheront; et après cela je leur enverrai beaucoup de chasseurs, qui leur feront la chasse sur toute montagne, sur toute colline et dans toutes les cavernes des rochers;
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
Parce que mes yeux sont sur toutes les voies; elles ne sont pas cachées à ma face, et leur iniquité n’est pas voilée à mes yeux.
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
Et je leur rendrai d’abord au double leurs iniquités et leurs péchés, parce qu’ils ont souillé ma terre de morts pour leurs idoles, et que de leurs abominations ils ont rempli mon héritage.
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
Seigneur, mon courage, ma force et mon refuge au jour de la tribulation, vers vous viendront des nations des extrémités de la terre, et elles diront: Il est vrai que nos pères ont possédé le mensonge et la vanité, qui ne leur a pas été utile.
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
Est-ce qu’un homme se fera des dieux, lesquels même ne sont pas des dieux?
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
C’est pourquoi voici que moi je leur montrerai cette fois, je leur montrerai ma main et ma force, et ils sauront que mon nom est le Seigneur.

< Yeremia 16 >