< Yeremia 16 >
1 Kisha neno la Bwana likanijia:
Puis la parole de l'Éternel me fut adressée en ces mots:
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
Tu ne prendras point de femme, et tu n'auras point dans ce lieu de fils ni de filles.
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
Car ainsi a dit l'Éternel, sur les fils et les filles qui naîtront en ce lieu, et sur leurs mères qui les auront enfantés, et sur leurs pères qui les auront engendrés dans ce pays:
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
Ils mourront de mort misérable; ils ne seront ni pleurés, ni ensevelis; mais ils seront comme du fumier sur la terre; ils seront consumés par l'épée et par la famine, et leurs cadavres serviront de pâture aux oiseaux des cieux et aux bêtes de la terre.
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
Car ainsi a dit l'Éternel: N'entre pas dans la maison de deuil, et ne va pas te lamenter ni t'affliger avec eux; car j'ai retiré de ce peuple ma paix, dit l'Éternel, ma grâce et mes compassions.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
Grands et petits mourront en ce pays; ils ne seront pas ensevelis: on ne les pleurera pas, on ne se fera point d'incisions, et l'on ne se rasera pas pour eux.
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
On ne rompra pas le pain dans le deuil, pour consoler quelqu'un au sujet d'un mort; on n'offrira pas la coupe de consolation, pour leur père ou pour leur mère.
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
N'entre pas non plus dans la maison de festin, pour t'asseoir avec eux, pour manger ou pour boire.
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
Car ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël: Voici, je ferai cesser en ce lieu, devant vos yeux et en vos jours, la voix de joie et la voix d'allégresse, la voix de l'époux et la voix de l'épouse.
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
Et quand tu auras annoncé à ce peuple toutes ces choses, et qu'ils te diront: “Pourquoi l'Éternel a-t-il prononcé tout ce grand mal contre nous? Quelle est donc notre iniquité, quel est le péché que nous avons commis contre l'Éternel notre Dieu?”
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
Tu leur diras: C'est parce que vos pères m'ont abandonné, dit l'Éternel, et sont allés après d'autres dieux et les ont servis, et se sont prosternés devant eux; parce qu'ils m'ont abandonné et n'ont pas gardé ma loi;
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
Et que vous faites encore pis que vos pères. Car voici, chacun de vous marche suivant la dureté de son cœur méchant, pour ne point m'écouter.
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
Aussi je vous transporterai de ce pays dans un pays que vous n'avez point connu, ni vous ni vos pères, et là vous servirez les autres dieux, jour et nuit, car je ne vous accorderai point de grâce.
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
C'est pourquoi voici, les jours viennent, dit l'Éternel, où l'on ne dira plus: L'Éternel est vivant, lui qui a fait monter du pays d'Égypte les enfants d'Israël;
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
Mais on dira: L'Éternel est vivant, lui qui a fait monter les enfants d'Israël du pays du Nord, et de tous les pays où il les avait chassés; car je les ramènerai dans leur pays, que j'avais donné à leurs pères.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
Voici, j'envoie de nombreux pêcheurs, dit l'Éternel, et ils les pêcheront; et après cela, j'enverrai de nombreux chasseurs, et ils les chasseront de toutes les montagnes, et de toutes les collines, et des fentes des rochers.
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
Car mes yeux sont sur toutes leurs voies; elles ne me sont point cachées, et leur iniquité n'est point couverte devant mes yeux.
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
Et je leur rendrai d'abord le double de leur iniquité et de leur péché, parce qu'ils ont souillé ma terre par les cadavres de leurs infamies, et qu'ils ont rempli mon héritage de leurs abominations.
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
Éternel! ma force, mon rempart, et mon refuge au jour de la détresse! les nations viendront à toi des bouts de la terre, et elles diront: Nos pères n'ont hérité que le mensonge, que des choses vaines, où il n'y a point de profit.
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
L'homme se fera-t-il lui-même des dieux, qui ne sont pas des dieux?
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
C'est pourquoi, voici, je leur ferai connaître cette fois, je leur ferai connaître ma force et ma puissance, et ils sauront que mon nom est l'Éternel.