< Yeremia 16 >

1 Kisha neno la Bwana likanijia:
Then the word of Yahweh came to me, saying,
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
“Do not take a wife for yourself, and do not have sons or daughters for yourself in this place.
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
For Yahweh says this to the sons and daughters who are born in this place, to the mothers who bear them, and to the fathers who caused them to be born in this land,
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
'They will die diseased deaths. They will not be mourned or buried. They will be like dung on the ground. For they will come to an end by sword and famine, and their corpses will be food for the birds of the skies and the beasts of the earth.'
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
For the word of Yahweh came to me, saying, 'Do not enter a house where there is mourning. Do not go to mourn or to show sympathy for them, for I have taken away my peace from this people—this is Yahweh's declaration—and my steadfast love and mercy.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
Both the great and the small will die in this land. They will not be buried, and no one will mourn for them or cut themselves or shave their heads for them.
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
No one must share any food in mourning to comfort them because of the deaths, and none must give a comforting cup to his father or his mother in order to comfort them.
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
You must not go to a banquet house to sit with them in order to eat or drink.'
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
For Yahweh of hosts, God of Israel, says this, 'See, before your eyes, in your days and in this place, I am about to put an end to the sound of joy and the sound of gladness, the sound of the groom and the sound of the bride.'
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
Then it will happen that you will report all these words to this people, and they will say to you, 'Why has Yahweh decreed all this great disaster against us? What is our iniquity and sin that we sinned against Yahweh our God?'
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
So say to them, 'Because your ancestors abandoned me—this is Yahweh's declaration—and they went after other gods and worshiped and bowed down to them. They abandoned me and have not kept my law.
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
But you yourselves have brought about more wickedness than your ancestors, for see, each person is walking by the stubbornness of his wicked heart; there is no one who listens to me.
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
So I will throw you from this land to a land that you have not known, neither you nor your ancestors, and you will worship other gods there by day and night, for I will not give any favor to you.'
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Therefore, behold, the days are coming—this is Yahweh's declaration—when it will no longer be said, 'As Yahweh lives, the one who brought up the people of Israel from the land of Egypt.'
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
but, 'As Yahweh lives, the one who brought up the people of Israel from the land of the north and from the lands where he had scattered them.' For I will bring them back to the land that I gave to their ancestors.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
Behold! I will send for many fishermen—this is Yahweh's declaration—so they will fish the people out. After this I will send for many hunters so they will hunt for them among all the mountains and hills, and in rock crevices.
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
For my eye is on all their ways; they cannot be hidden from before me. Their iniquity cannot be concealed from before my eyes.
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
I will first pay back double for their iniquity and sin for their polluting of my land with their disgusting idol figures, and for their filling my inheritance with their disgusting idols.”
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
Yahweh, you are my stronghold and my refuge, my place of safety in the day of distress. The nations will go to you from the ends of the earth and say, “Surely our ancestors inherited deceit. They are empty; there is no profit in them.
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
Do people make gods for themselves? But they are not gods.”
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
Therefore see! I will cause them to know in this time, I will cause them to know my hand and my power, so they will know that Yahweh is my name.

< Yeremia 16 >