< Yeremia 16 >
1 Kisha neno la Bwana likanijia:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
Not you must take for yourself a wife and not they will belong to you sons and daughters in the place this.
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
For thus - he says Yahweh on the sons and on the daughters born in the place this and on mothers their who bore them and on fathers their who fathered them in the land this.
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
Deaths of diseases they will die not they will be mourned and not they will be buried dung on [the] surface of the ground they will become and by the sword and by famine they will come to an end and it will become corpse[s] their food for [the] bird[s] of the heavens and for [the] animal[s] of the earth.
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
For thus - he says Yahweh may not you enter a house of mourning and may not you go to lament and may not you show sympathy to them for I have withdrawn peace my from with the people this [the] utterance of Yahweh the covenant loyalty and compassion.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
And they will die great [people] and insignificant [people] in the land this not they will be buried and not people will mourn for them and not anyone will cut himself and not anyone will make himself bald for them.
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
And not people will break for them on mourning to comfort him on a dead [person] and not people will give to drink them a cup of consolations on father his and on mother his.
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
And a house of a feast not you must go to sit with them to eat and to drink.
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
For thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel here I [am] about to cause to cease from the place this to eyes your and in days your [the] sound of joy and [the] sound of gladness [the] sound of a bridegroom and [the] sound of a bride.
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
And it will be that you will tell to the people this all the words these and they will say to you concerning what? has he spoken Yahweh on us all the calamity great this and what? [is] iniquity our and what? [is] sin our which we have sinned to Yahweh God our.
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
And you will say to them on that they forsook ancestors your me [the] utterance of Yahweh and they walked after gods other and they served them and they bowed down to them and me they forsook and law my not they kept.
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
And you you have done evil to act more than ancestors your and here you [are] walking everyone after [the] stubbornness of own heart his wicked to not to listen to me.
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
And I will throw out you from on the land this to the land which not you have known you and ancestors your and you will serve there gods other by day and night that not I will give to you favor.
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Therefore here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and not it will be said again [by] [the] life of Yahweh who he brought up [the] people of Israel from [the] land of Egypt.
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
That except [by] [the] life of Yahweh who he brought up [the] people of Israel from a land of [the] north and from all the lands where he had banished them there towards and I will bring back them to land their which I gave to ancestors their.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
Here I [am] about to send (for fishermen *Q(K)*) many [the] utterance of Yahweh and they will fish out them and after thus I will send for many hunters and they will hunt them from on every mountain and from on every hill and from [the] clefts of the rocks.
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
For eyes my [are] on all ways their not they have been hidden from to before me and not it has been concealed iniquity their from before eyes my.
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
And I will repay first [the] double of iniquity their and sin their because have profaned they land my with [the] corpse[s] of detestable things their and abominations their they have filled inheritance my.
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
O Yahweh strength my and stronghold my and place of escape my in a day of trouble to you nations they will come from [the] ends of [the] earth so they may say surely falsehood they possessed ancestors our futility and not [there was] in them a [thing that] profits.
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
¿ Will he make for himself anyone gods and they not [are] God.
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
Therefore here I [am] about to make know them at the time this I will make know them hand my and might my and they will know that name my [is] Yahweh.