< Yeremia 15 >

1 Kisha Bwana akaniambia: “Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele zangu, moyo wangu usingewaelekea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende!
И рече Господь ко мне: аще станут Моисей и Самуил пред лицем Моим, несть душа Моя к людем сим: изрини тех (от лица Моего), и да изыдут.
2 Nao kama wakikuuliza, ‘Twende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe; waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga; waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa: waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’”
И будет, аще рекут к тебе: камо изыдем? И речеши к ним: сия глаголет Господь: иже ко смерти, ко смерти: и иже к мечу, к мечу: и иже ко гладу, ко гладу: и иже ко пленению, ко пленению.
3 Bwana asema, “Nitatuma aina nne za waharabu dhidi yao: nazo ni upanga ili kuua na mbwa ili wakokote mbali, ndege wa angani na wanyama wa nchi ili kula na kuangamiza.
И отмщу имъчетырьми образы, рече Господь: мечь на заклание, и пси на растерзание, и птицы небесе и зверие земли на пожрения и расхищение.
4 Nitawafanya wawe machukizo kwa falme zote za dunia kwa sababu ya kile alichofanya Manase mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda huko Yerusalemu.
И предам их во утеснение всем царствам земным, ради Манассии сына Езекиина царя Иудина за вся, яже сотвори во Иерусалиме.
5 “Ni nani atakayekuhurumia, ee Yerusalemu? Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako? Ni nani atakayesimama ili kuuliza kuhusu hali yako?
Кто умилосердится к тебе, Иерусалиме? И кто поскорбит о тебе, или кто пойдет молити о мире тебе?
6 Umenikataa mimi,” asema Bwana. “Unazidi kukengeuka. Hivyo nitanyoosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza, siwezi kuendelea kukuonea huruma.
Ты оставил Мя еси, рече Господь, вспять пошел еси: и простру руку Мою на тя и убию тя, и ктому не пощажу их
7 Nitawapepeta kwa uma wa kupepetea kwenye malango ya miji katika nchi. Nitaleta msiba na maangamizi juu ya watu wangu, kwa maana hawajabadili njia zao.
и расточу их расточением во вратех людий Моих: обезчадеша, погубиша людий Моих злобами своими, и не обратишася.
8 Nitawafanya wajane wao kuwa wengi kuliko mchanga wa bahari. Wakati wa adhuhuri nitamleta mharabu dhidi ya mama wa vijana wao waume; kwa ghafula nitaleta juu yao maumivu makuu na hofu kuu.
Умножишася вдовицы их паче песка морскаго: наведох на матерь юношы, бедность о полудни, навергох на ню внезапу страх и трепет.
9 Mama mwenye watoto saba atazimia na kupumua pumzi yake ya mwisho. Jua lake litatua kungali bado mchana, atatahayarika na kufedheheka. Wale wote waliobaki nitawaua kwa upanga mbele ya adui zao,” asema Bwana.
Праздна бысть родившая седмь, оскуде душа ея, зайде ей солнце еще среде полудне, постыждена бысть и укорена: прочыя их в мечь дам пред враги их, рече Господь.
10 Ole wangu, mama yangu, kwamba ulinizaa, mtu ambaye ulimwengu wote unashindana na kugombana naye! Sikukopa wala sikukopesha, lakini kila mmoja ananilaani.
Горе мне, мати (моя), вскую мя родила еси мужа прителнаго и судимаго по всей земли? Не заях, ниже заят у мене кто: сила моя оскуде от кленущих мя, (рече Господь).
11 Bwana akasema, “Hakika nitakuokoa kwa kusudi jema, hakika nitawafanya adui zako wakuombe msaada nyakati za maafa na nyakati za dhiki.
Буди, Владыко, исправляющым им: аще не притекох ко Тебе во время озлобления их и во время скорби их, во благая на врага.
12 “Je, mtu aweza kuvunja chuma, chuma kitokacho kaskazini, au shaba?
Еда познается железо? И одеяние медяно крепость твоя.
13 Utajiri wako na hazina zako nitavitoa kuwa nyara, bila gharama, kwa sababu ya dhambi zako zote katika nchi yako yote.
И сокровища твоя в расхищение дам, измену за вся грехи твоя, и во всех пределех твоих:
14 Nitakufanya uwe mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa katika hasira yangu moto umewashwa utakaowaka juu yako daima.”
и порабощу тя окрест врагом твоим, в земли, еяже не веси: яко огнь возжжеся от ярости Моея, на вас горети будет.
15 Wewe unafahamu, Ee Bwana, unikumbuke na unitunze mimi. Lipiza kisasi juu ya watesi wangu. Kwa uvumilivu wako usiniondolee mbali; kumbuka jinsi ninavyoshutumiwa.
Ты веси, Господи, воспомяни мя и посети мя и защити мя от гонящих мя, не в долготерпение Твое восприими мя: веждь, яко приях Тебе ради поношение от отвергающих словеса Твоя:
16 Maneno yako yalipokuja, niliyala; yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
скончай их, и будет слово Твое мне в радость и во веселие сердца моего, яко призвано есть имя Твое на мне, Господи Боже Сил.
17 Kamwe sikuketi katika kundi la wafanyao sherehe, wala kamwe sikujifurahisha pamoja nao; niliketi peke yangu kwa sababu mkono wako ulikuwa juu yangu, na wewe ulikuwa umenijaza hasira.
Не седох в сонме их играющих, но бояхся от лица руки Твоея: на едине седях, яко горести исполнихся.
18 Kwa nini maumivu yangu hayakomi, na jeraha langu ni la kuhuzunisha, wala haliponyeki? Je, utakuwa kwangu kama kijito cha udanganyifu, kama chemchemi iliyokauka?
Вскую оскорбляющии мя возмогают на мя? Язва моя тверда, откуду изцелюся? Бысть мне яко вода лживая, не имущая верности.
19 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Kama ukitubu, nitakurejeza ili uweze kunitumikia; kama ukinena maneno yenye maana, wala si ya upuzi, utakuwa mnenaji wangu. Watu hawa ndio watakaokugeukia, wala si wewe utakayewageukia wao.
Сего ради сия глаголет Господь: аще обратишися, возставлю тя, и пред лицем Моим станеши: и аще изведеши честное от недостойнаго, яко уста Моя будеши: и обратятся тии к тебе, и ты не обратишися к ним.
20 Nitakufanya wewe uwe ukuta kwa watu hawa, ngome ya ukuta wa shaba; watapigana nawe lakini hawatakushinda, kwa maana mimi niko pamoja nawe kukuponya na kukuokoa,” asema Bwana.
И дам тя людем сим аки стену крепку, медяну: и поратуют на тя и не возмогут на тя, яко Аз с тобою есмь, да спасу тя и избавлю тя, рече Господь:
21 “Nitakuokoa kutoka mikono ya waovu, na kukukomboa kutoka makucha ya watu wakatili.”
избавлю тя от рук злейших и искуплю тя от рук губителей.

< Yeremia 15 >