< Yeremia 14 >
1 Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
La parole de l'Éternel, qui fut adressée à Jérémie, à l'occasion de la sécheresse:
2 “Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
Juda est dans le deuil; et dans ses portes on languit tristement couché à terre, et le cri de Jérusalem monte vers le ciel.
3 Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
Et les grands d'entre eux envoient les petits chercher de l'eau; ils vont aux citernes, et ne trouvent point d'eau; ils reviennent leurs vases vides; ils sont honteux et confus, et couvrent leur tête.
4 Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
A cause du sol qui est consterné, parce qu'il n'y a point eu de pluie au pays, les laboureurs confus et honteux se couvrent la tête.
5 Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
Même la biche, dans la campagne, fait son faon et l'abandonne, parce qu'il n'y a point d'herbe.
6 Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
Les ânes sauvages se tiennent sur les lieux élevés, humant le vent comme les chacals; leurs yeux sont éteints, parce qu'il n'y a point de verdure.
7 Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
Si nos iniquités témoignent contre nous, agis à cause de ton nom, ô Éternel! Car nos infidélités sont nombreuses; c'est contre toi que nous avons péché.
8 Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
Toi qui es l'attente d'Israël et son libérateur au temps de la détresse, pourquoi serais-tu dans le pays comme un étranger, et comme un voyageur qui se détourne pour passer la nuit!
9 Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
Pourquoi serais-tu comme un homme stupéfait, et comme un héros qui ne peut sauver? Mais tu es au milieu de nous, ô Éternel! et ton nom est invoqué sur nous: ne nous abandonne pas!
10 Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
Ainsi a dit l'Éternel au sujet de ce peuple: C'est ainsi qu'ils aiment à aller çà et là. Ils ne retiennent point leurs pieds, et l'Éternel ne prend point plaisir en eux. Il se souvient maintenant de leur iniquité, et il punit leurs péchés.
11 Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
Puis l'Éternel me dit: N'intercède pas en faveur de ce peuple.
12 Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
S'ils jeûnent, je n'écouterai point leur cri, et s'ils offrent des holocaustes et des oblations, je ne les agréerai point; car je vais les consumer par l'épée, par la famine et par la peste.
13 Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
Et je dis: Ah! Seigneur Éternel! voici, les prophètes leur disent: Vous ne verrez point d'épée, et vous n'aurez point de famine; mais je vous donnerai dans ce lieu-ci une paix assurée!
14 Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
Et l'Éternel me dit: C'est le mensonge, que ces prophètes prophétisent en mon nom. Je ne les ai point envoyés, je ne leur ai point donné de charge, et je ne leur ai point parlé. Ce sont des visions de mensonge, de vaines prédictions, des tromperies de leur cœur, qu'ils vous prophétisent.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Éternel, touchant ces prophètes qui prophétisent en mon nom sans que je les aie envoyés, et qui disent: “Il n'y aura ni épée, ni famine dans ce pays”, ces prophètes eux-mêmes périront par l'épée et par la famine.
16 Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
Et ce peuple auquel ils prophétisent, sera jeté par la famine et l'épée dans les rues de Jérusalem, sans que personne les ensevelisse, tant eux que leurs femmes, leurs fils et leurs filles, et je répandrai sur eux leur méchanceté.
17 “Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
Et dis-leur cette parole: Que mes yeux se fondent en larmes nuit et jour, et qu'ils ne cessent point! Car la vierge, fille de mon peuple, a été frappée d'un grand coup, d'une plaie fort douloureuse.
18 Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
Si je sors aux champs, voici des gens percés de l'épée, et si j'entre dans la ville, voici des gens qui meurent de faim. Le prophète même et le sacrificateur courent par le pays, sans savoir où ils vont.
19 Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
Aurais-tu entièrement rejeté Juda? Ton âme aurait-elle Sion en horreur? Pourquoi nous frappes-tu sans qu'il y ait pour nous de guérison? On attend la paix, mais il n'y a rien de bon; un temps de guérison, et voici la terreur!
20 Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
Éternel! nous reconnaissons notre méchanceté, l'iniquité de nos pères; car nous avons péché contre toi!
21 Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
A cause de ton nom ne rejette pas, ne déshonore pas ton trône de gloire; souviens-toi; ne romps pas ton alliance avec nous!
22 Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.
Parmi les vaines idoles des nations y en a-t-il qui fassent pleuvoir? Ou sont-ce les cieux qui donnent la pluie menue? N'est-ce pas toi, Éternel, notre Dieu? Et nous espérerons en toi; car c'est toi qui fais toutes ces choses.