< Yeremia 14 >

1 Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
Parole de Yahweh qui fut adressée à Jérémie à l'occasion de la sécheresse.
2 “Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
Juda est dans le deuil; ses portes languissent; elles gisent désolées sur la terre, et le cri de Jérusalem s'élève.
3 Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
Les grands envoient les petits chercher de l'eau; ceux-ci vont aux citernes, ils ne trouvent pas d'eau, ils reviennent avec leurs vases vides; ils sont confus et honteux, ils se couvrent la tête.
4 Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
A cause du sol crevassé, parce qu'il n'y a pas eu de pluie sur la terre, les laboureurs sont confondus, ils se couvrent la tête.
5 Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
Même la biche dans la campagne met bas et abandonne ses petits, parce qu'il n'y a pas d'herbe.
6 Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
Les onagres se tiennent sur les hauteurs, aspirant l'air comme des chacals; leurs yeux s'éteignent, parce qu'il n'y a pas de verdure.
7 Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
Si nos iniquités témoignent contre nous, Yahweh, agis pour l'honneur de ton nom; car nos infidélités sont nombreuses; nous avons péché contre toi.
8 Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
O toi, l'espérance d'Israël, son libérateur au temps de la détresse, pourquoi serais-tu comme un étranger dans le pays, comme un voyageur qui y dresse sa tente pour la nuit?
9 Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
Pourquoi serais-tu comme un homme éperdu, comme un héros impuissant à délivrer? Pourtant tu habites au milieu de nous, Yahweh; ton nom est invoqué sur nous, ne nous abandonne pas! —
10 Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
Ainsi parle Yahweh au sujet de ce peuple: Oui, ils aiment à courir çà et là, et ils ne savent pas retenir leurs pieds. Yahweh ne trouve plus de plaisir en eux; Il va maintenant se souvenir de leurs iniquités et châtier leurs péchés.
11 Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
Et Yahweh me dit: " N'intercède pas en faveur de ce peuple.
12 Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
Quand ils jeûneront, je n'écouterai pas leurs supplications; quand ils m'offriront des holocaustes et des offrandes, je ne les agréerai pas; car par l'épée, la famine et la peste je veux les détruire. "
13 Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
Et je répondis: " Ah! Seigneur, Yahweh, voici que les prophètes leur disent: Vous ne verrez point d'épée, et vous n'aurez point de famine; mais je vous donnerai une paix assurée dans ce lieu-ci. "
14 Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
Et Yahweh me dit: " C'est le mensonge que les prophètes prophétisent en mon nom: je ne les ai pas envoyés, je ne leur ai point donné d'ordre, et je ne leur ai point parlé; visions mensongères, vaines divinations, imposture de leur propre cœur, voilà ce qu'ils vous prophétisent. "
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
C'est pourquoi ainsi parle Yahweh: Au sujet des prophètes qui prophétisent en mon nom sans que je les aie envoyés, et qui disent: " D'épée et de famine il n'y aura pas dans ce pays!... " Ils périront par l'épée et par la famine, ces prophètes-là!
16 Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
Et les gens auxquels ils prophétisent seront jetés dans les rues de Jérusalem, victimes de la famine et de l'épée, et il n'y aura personne pour les ensevelir, eux, leurs femmes, leurs fils et leurs filles et je verserai sur eux leur méchanceté.
17 “Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
Et tu leur diras cette parole: Mes yeux se fondront en larmes la nuit et le jour, sans arrêt; car la vierge, fille de mon peuple, va être frappée d'un grand désastre, d'une plaie très douloureuse.
18 Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
Si je vais dans les champs, voici des hommes que le glaive a percés; si j'entre dans la ville, voilà les douleurs de la faim. Le prophète lui-même et le prêtre sont errants, vers un pays qu'ils ne connaissaient pas.
19 Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
As-tu donc entièrement rejeté Juda? Ton âme a-t-elle pris Sion en dégoût? Pourquoi nous frappes-tu sans qu'il y ait pour nous de guérison? Nous attendions la paix, et il ne vient rien de bon; le temps de la guérison, et voici l'épouvante.
20 Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
Nous reconnaissons, ô Yahweh, notre méchanceté, l'iniquité de nos pères, car nous avons péché contre toi.
21 Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
A cause de ton nom, ne dédaigne pas, ne profane pas le trône de ta gloire; souviens-toi, ne romps pas ton alliance avec nous.
22 Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.
Parmi les vaines idoles des nations, en est-il qui fasse pleuvoir? Est-ce le ciel qui donnera les ondées? N'est-ce pas toi, Yahweh, notre Dieu? Nous espérons en toi, car c'est toi qui fais toutes ces choses.

< Yeremia 14 >