< Yeremia 14 >

1 Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
The word of the Lord, that was maad to Jeremye, of the wordis of dryenesse.
2 “Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
Jude weilide, and the yatis therof fellen doun, and ben maad derk in erthe, and the cry of Jerusalem stiede.
3 Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
Grettere men senten her lesse men to water; thei camen to drawe watir, and thei foundun no water, thei brouyten ayen her vessels voide; thei weren schent and turmentid,
4 Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
and thei hiliden her heedis for distriyng of the lond, for reyn cam not in the lond. Erthe tilieris weren schent, thei hiliden her heedis.
5 Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
For whi and an hynde caluyde in the feeld, and lefte her calues, for noon eerbe was;
6 Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
and wield assis stoden in rochis, and drowen wynde as dragouns; her iyen failiden, for noon eerbe was.
7 Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
If oure wickidnessis answeren to vs, Lord, do thou for thi name, for oure turnyngis awei ben manye; we han synned ayens thee.
8 Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
Thou abidyng of Israel, the sauyour therof in the tyme of tribulacioun,
9 Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
whi schalt thou be as a comelyng in the lond, and as a weigoere bowynge to dwelle? whi schalt thou be as a man of vnstable dwellyng, as a strong man that mai not saue? Forsothe, Lord, thou art in vs, and thin hooli name is clepid to help on vs; forsake thou not vs.
10 Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
The Lord seith these thingis to this puple, that louede to stire hise feet, and restide not, and pleside not the Lord; now he schal haue mynde on the wickidnesses of hem, and he schal visite the synnes of hem.
11 Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
And the Lord seide to me, Nyle thou preie for this puple in to good.
12 Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
Whanne thei schulen faste, Y schal not here the preieris of hem; and if thei offren brent sacrifices and slayn sacrifices, Y schal not resseyue tho, for Y schal waste hem bi swerd and hungur and pestilence.
13 Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
And Y seide, A! A! A! Lord God, profetis seien to hem, Ye schulen not se swerd, and hungur schal not be in you, but he schal yyue to you veri pees in this place.
14 Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
And the Lord seide to me, The profetis profesien falsli in my name; Y sente not hem, and Y comaundide not to hem, nether Y spak to hem; thei profesien to you a fals reuelacioun, and a gileful dyuynyng, and the disseyuyng of her herte.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
Therfor the Lord seith these thingis of the profetis that profesien in my name, whiche Y sente not, and seien, Swerd and hungur schal not be in this lond; Tho profetis schulen be wastid bi swerd and hungur.
16 Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
And the puplis, to whiche thei profesieden, schulen be cast forth in the weies of Jerusalem, for hungur and swerd, and noon schal be, that schal birie hem; they and the wyues of hem, the sones and the douytris of hem `schulen be cast forth; and Y schal schede out on hem her yuel.
17 “Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
And thou schalt seie to hem this word, Myn iyen lede doun a teer bi niyt and dai, and be not stille, for the virgyn, the douyter of my puple, is defoulid bi greet defoulying, with the worste wounde greetli.
18 Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
If Y go out to feeldis, lo! men ben slayn bi swerd; and if Y entre in to the citee, lo! men ben maad leene for hungur; also a profete and a prest yeden in to the lond which thei knewen not.
19 Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
Whether thou castynge awei hast cast awei Juda, ether thi soule hath wlatid Sion? whi therfor hast thou smyte vs, so that noon heelthe is? We abididen pees, and no good is; and we abididen time of heeling, and lo! disturbling is.
20 Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
Lord, we han know oure vnfeithfulnessis, and the wickidnessis of oure fadris, for we han synned to thee.
21 Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
Yyue thou not vs in to schenschip, for thi name, nether do thou dispite to vs; haue thou mynde on the seete of thi glorie, make thou not voide thi boond of pees with vs.
22 Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.
Whether in grauun ymagis of hethene men ben thei that reynen, ethir heuenes moun yyue reynes? whether thou art not oure Lord God, whom we abididen? For thou madist alle these thingis.

< Yeremia 14 >