< Yeremia 14 >

1 Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
This is the word of Yahweh that came to Jeremiah regarding the drought,
2 “Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
“Let Judah mourn; let her gates fall apart. They are wailing for the land; their cries for Jerusalem are going up.
3 Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
Their mighty ones send out their servants for water. When they go to the trenches, they cannot find water. They all return unsuccessful; they cover their heads ashamed and dishonored.
4 Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
Because of this the ground is cracked, for there is no rain in the land. The plowmen are ashamed and cover their heads.
5 Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
For even the doe leaves her young in the fields and abandons them, for there is no grass.
6 Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
The wild donkeys stand on the bare plains and they pant in the wind like jackals. Their eyes fail to work, for there is no vegetation.”
7 Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
Even though our iniquities testify against us, Yahweh, act for the sake of your name. For our faithless actions increase; we have sinned against you.
8 Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
You are the Hope of Israel, the one who saves him in the time of distress, why will you be like a stranger in the land, like a foreign wanderer who stretches out and spends just one night?
9 Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
Why are you like someone who is astounded, or like a warrior who has no power to rescue? You are in our midst, Yahweh, and your name is called over us. Do not leave us!
10 Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
Yahweh says this to this people: “Since they love to wander, they have not held back their feet from doing so.” Yahweh is not pleased with them. Now he calls to mind their iniquity and has punished their sins.
11 Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
Yahweh said to me, “Do not pray for good on behalf of this people.
12 Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
For if they fast, I will not listen to their wailing, and if they offer up burnt offerings and food offerings, I will not take pleasure in them. For I will put an end to them by sword, famine, and plague.”
13 Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
Then I said, “Oh, Lord Yahweh! Behold! The prophets are saying to the people, 'You will not see the sword; there will be no famine for you, for I will give you true security in this place.'”
14 Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
Yahweh said to me, “The prophets prophesy deceit in my name. I did not send them out, nor did I give them any command or speak to them. But deceitful visions and useless, deceitful divination coming from their own minds are what they are prophesying to you.”
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
Therefore Yahweh says this, “About the prophets prophesying in my name but whom I did not send out—those who say there will be no sword or famine in this land: These prophets will perish by sword and famine.
16 Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
Then the people to whom they prophesied will be thrown out in the streets of Jerusalem because of famine and sword, for there will be no one to bury them—them, their wives, their sons, or their daughters—for I will pour out their wickedness on them.
17 “Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
Say this word to them: 'Let my eyes flow with tears, night and day. Do not let them stop, for there will be a great collapse of the virgin daughter of my people— a great and incurable wound.
18 Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
If I go out to the field, there are the ones who were killed by the sword! If I come to the city, there are the diseases that are caused by famine. Both the prophet and the priest wander about the land, and they do not know.'”
19 Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
Have you completely rejected Judah? Do you hate Zion? Why will you afflict us when there is no healing for us? We hoped for peace, but there was nothing good— and for a time of healing, but see, there is only terror.
20 Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
We admit, Yahweh, our offenses, the iniquity of our ancestors, for we have sinned against you.
21 Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
Do not reject us! For the sake of your name, do not make your glorious throne a disgrace. Remember and do not break your covenant with us.
22 Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.
Do any of the worthless idols of the nations bring rain? Or can the skies themselves send down showers? Are you not the one, Yahweh our God? We wait for you, for you are the one who does all these things.

< Yeremia 14 >