< Yeremia 14 >

1 Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
The word of Jehovah, which came to Jeremiah concerning a drought.
2 “Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
Judah mourneth, And the gates thereof languish; They are in deep mourning upon the ground. And the cry of Jerusalem goeth up.
3 Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
The nobles send their younger ones for water; They come to the wells, they find none; They return with their vessels empty; They are ashamed and confounded; They cover their heads.
4 Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
Because of the ground, which is in consternation, No rain falling upon the earth, The husbandmen are ashamed, They hide their heads.
5 Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
Even the hind in the field is delivered, And deserteth her young, Because there is no grass.
6 Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
The wild asses stand upon the hills, They snuff up the wind like jackals; Their eyes fail, Because there is no grass.
7 Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
Though our iniquities testify against us, Yet do thou, O Jehovah, act from a regard to thine own name. For our transgressions have been many; We have sinned against thee.
8 Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
O thou hope of Israel, His saviour in the time of trouble, Why wilt thou be as a stranger in the land, As a traveller who spreadeth his tent to pass the night?
9 Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
Why wilt thou be as a man that is amazed, As a hero that cannot save? Thou art in the midst of us, O Jehovah, And we are called by thy name; Do not forsake us!
10 Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
Thus saith Jehovah concerning this people: Thus they love to wander, They restrain not their feet; Therefore Jehovah doth not accept them; Now will he remember their iniquities, And punish their sins.
11 Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
Then said Jehovah to me: Pray not for this people for their good!
12 Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
Though they fast, I will not hear their cry; Though they offer burnt-offerings and flour-offerings, I will not accept them; But by the sword, and by famine, and by pestilence, I will make an end of them.
13 Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
Then said I, Alas! O Lord Jehovah! Behold, the prophets say to them, “Ye shall not see the sword, Nor shall famine come upon you; But Jehovah will give you lasting peace in this place.”
14 Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
Then said Jehovah to me: The prophets prophesy lies in my name; I have not sent them, nor commissioned them, nor spoken to them; A false vision, and divination, and vanity, And the fraud of their hearts, do they prophesy to you.
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
Therefore thus saith Jehovah concerning the prophets Who prophesy in my name, though I sent them not, But who themselves say, “The sword and famine shall not be in this land”: By the sword and by famine shall those prophets be consumed.
16 Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
And the people to whom they prophesy Shall be cast forth in the streets of Jerusalem By means of famine and the sword; And they shall have none to bury them, —They, their wives, and their sons, and their daughters; For I will pour their wickedness upon them.
17 “Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
Thus also shalt thou speak to them: My eyes shall run down with tears night and day; They shall not cease; For a deep wound hath she received, The virgin daughter of my people, A deadly blow.
18 Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
If I go forth into the fields, Then behold them that are slain by the sword! And if I enter the city, Then behold them that pine with famine! Both prophet and priest wander about the land, they know not whither.
19 Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
Hast thou utterly rejected Judah? Doth thy soul abhor Zion? Why hast thou smitten us, so that there is no healing for us! We look for peace, and there is no good, For a time of healing, and behold, terror!
20 Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
We acknowledge, O Jehovah, our wickedness, And the iniquity of our fathers; For we have sinned against thee.
21 Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
Do not spurn us, for thy name's sake! Do not dishonor thy glorious throne! Call to mind, break not, thy covenant with us!
22 Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.
Are there among the vanities of the nations any that can cause rain? Or can the heavens give showers? Art not thou he, O Jehovah, our God? Therefore in thee will we trust, For thou hast made all these things!

< Yeremia 14 >